VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Leo, tarehe 5/12/2017, kwa mara ya kwanza tangu kuanza 'kuchalenjiwa' na mwanangu wa Chuo Kikuu, nimekubaliana naye. Alinipigia simu ya nidhamu na kunisalimu. Leo hakunilaumu. Anajua sishiriki katika mikiki inayotiki ya kuhamahama kinafiki bila urafiki. Akanipongeza kwa kutoshiriki kwangu na kunisihi kubaki na wajihi huohuo.
Mwanangu, anayemalizia Shahada yake ya kwanza ya Sheria, akaniambia jambo la maana. Nimekubaliana naye. Amenidokeza na kukoleza kuwa hii hamahama inayoendelea kutoka upinzani hasa CHADEMA kwenda CCM ni kuepusha anguko la CHADEMA na upinzani kwa ujumla. Akanikumbusha figisu za uchaguzini ambapo wagombea mamluki wanapojitoa katika kugombea katika muda wa lala salama.
Mwanangu akaniambia kuwa, yeye anaamini, wanaohama sasa CHADEMA kwenda CCM walikuwa mamluki wetu CCM. Sasa wanarudi nyumbani. Ni bahati kuwa wanarudi kabla ya uchaguzi. Wanarudi kwa wanachokiamini na kukitumikia. Mwanangu akaniongezea kuwa wanaohama sasa 'walihamia' CHADEMA wakati uliopita. Hoja yake ya haja mwanangu ni kuwa mamluki lukuki wanaotisha kuliko bunduki au mkuki wanarudi wakijaa chuki kuliko weupe wa chaki.
Tukakubaliana kiungwana kuwa hamahama inaepusha kiama na dhahama kwenye vyama. Inasafisha CHADEMA na kuchafua CCM. Kwakuwa, kuvuja kwa pakacha ni nafuu ya mchukuzi. Mwanangu akanichokoza kidogo. Eti, nipeleleze hata dau linalotumika kufanya usajili wa kimwili katika siasa za kisasa zinazosafisha kama msasa. Amini nawaambia, CHADEMA itaimarika maradufu.
Kujenga hoja bila bunduki itapendeza sana! Mambo ya expansion joints hayo!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kibiti, Pwani)
Mwanangu, anayemalizia Shahada yake ya kwanza ya Sheria, akaniambia jambo la maana. Nimekubaliana naye. Amenidokeza na kukoleza kuwa hii hamahama inayoendelea kutoka upinzani hasa CHADEMA kwenda CCM ni kuepusha anguko la CHADEMA na upinzani kwa ujumla. Akanikumbusha figisu za uchaguzini ambapo wagombea mamluki wanapojitoa katika kugombea katika muda wa lala salama.
Mwanangu akaniambia kuwa, yeye anaamini, wanaohama sasa CHADEMA kwenda CCM walikuwa mamluki wetu CCM. Sasa wanarudi nyumbani. Ni bahati kuwa wanarudi kabla ya uchaguzi. Wanarudi kwa wanachokiamini na kukitumikia. Mwanangu akaniongezea kuwa wanaohama sasa 'walihamia' CHADEMA wakati uliopita. Hoja yake ya haja mwanangu ni kuwa mamluki lukuki wanaotisha kuliko bunduki au mkuki wanarudi wakijaa chuki kuliko weupe wa chaki.
Tukakubaliana kiungwana kuwa hamahama inaepusha kiama na dhahama kwenye vyama. Inasafisha CHADEMA na kuchafua CCM. Kwakuwa, kuvuja kwa pakacha ni nafuu ya mchukuzi. Mwanangu akanichokoza kidogo. Eti, nipeleleze hata dau linalotumika kufanya usajili wa kimwili katika siasa za kisasa zinazosafisha kama msasa. Amini nawaambia, CHADEMA itaimarika maradufu.
Kujenga hoja bila bunduki itapendeza sana! Mambo ya expansion joints hayo!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kibiti, Pwani)