muhosni
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 1,108
- 152
Dar es Salaam kuna kituo cha basi huitwa Gongo la Mboto mwisho wa lami. Zamani hapo ndipo lami ya kutoka mjini ilikuwa inaishia na kwa hiyo daladala pia zilikuwa zinaishia hapo. Siku hizi kuna maendeleo zaidi Gombolamboto siyo tena mwisho wa Lami.
Uteuzi wa baraza kivuli la mawaziri wa leo tunaweza kusema ni Gongolamboto kwa akina David Kafulila na Hamad Rashid kwa maana ya kwamba katika safari yao ya kushirikishwa kwenye kambi rasmi ya upinzani hapo ndo mwisho wa lami. Hakuna uwezekano huo kwa sasa, LABDA baadaye, kama hiyo baadaye na wao watakuwemo.
Hawakupata uongozi wa kamati hata moja wala uwaziri kivuli. Lakini walihemshwa na support ya wabunge wa ccm na kusahau kwamba hawawezi kulazimisha uhusiano kwa kutumia kanuni za bunge. Sasa ccm wameshapata walichotaka, yaani kamati ya PAC kuongozwa na mtu wao (Cheyo). Habari imekwisha, Kafulila na Hamad wanauguza maumivu, Chadema wanachekelea na kusonga mbele.
I love politics, who loughs last loughs longer!!
Uteuzi wa baraza kivuli la mawaziri wa leo tunaweza kusema ni Gongolamboto kwa akina David Kafulila na Hamad Rashid kwa maana ya kwamba katika safari yao ya kushirikishwa kwenye kambi rasmi ya upinzani hapo ndo mwisho wa lami. Hakuna uwezekano huo kwa sasa, LABDA baadaye, kama hiyo baadaye na wao watakuwemo.
Hawakupata uongozi wa kamati hata moja wala uwaziri kivuli. Lakini walihemshwa na support ya wabunge wa ccm na kusahau kwamba hawawezi kulazimisha uhusiano kwa kutumia kanuni za bunge. Sasa ccm wameshapata walichotaka, yaani kamati ya PAC kuongozwa na mtu wao (Cheyo). Habari imekwisha, Kafulila na Hamad wanauguza maumivu, Chadema wanachekelea na kusonga mbele.
I love politics, who loughs last loughs longer!!