Hamad Rashid Mohammed naye kuondoka CUF!

Nilisha sema huko nyuma kwanba hakuna wapnzani isipokuwa watu wana malengo yao lakini Hamadi Rashidi hawezi kwenda Chadema kwa kuwa wapenba wana ubaguzi wa dini na ukabila maana wao wanajifanya ni waarabu
 
Hata ikiwa ni tetesi. Mimi nampongeza Bw. Hamad Rashid kama atachukua hatua hiyo. Anaweza kuwa kiongozi wa "the alternative Party" na tukaiendeleza Zanzibar (ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) . Ni Mwanasiasa mahiri sana huyo!

Hicho chama atakachoanzisha mfadhili wake mkuu atakuwa RA maana tayari huyu jamaa alishaonyesha kuwa kibaraka wa RA (kumbuka reaction yake kwa Mengi wakati wa issue ya mafisadi papa). Na kama atataka kujiunga vyama vingine, chama kama CHADEMA wasimkubali maana atakwenda kuwamaliza. Labda aende huko CCM kwa RA wake.
 
Last edited:
Karibu sana kwenye chama cha maendeleo na demokrasia mheshimiwa hamad rashid.njoo ukajiunge na wanaharakati wenzako wenye hari na bidii ya kunyoosha maisha ya watanzania kama wewe.
 
Kuna kipindi RTD kinaitwa "mazungumzo baada ya habari". If wishes were horses, beggars would ride. Ndoto muanaota.Nani aende CCM?.
 


Mimi siamini kama hii habari ya kuhama ni kweli, lakini pia sikubaliani iwapo Hamad Rashid ata-make a good leader in CUF. Alinichomoka pale alipomuuliza Pinda Bungeni kuhusu suala la Mengi kuwataja mafisadi papa -- yaani serikali ichukue hatua gani dhidi ya Mengi -- yaani yale yale ya Profesa yaliyompotezesha hadhi alipojitokeza hadharani kuwatetea "mapapa" wa ufisadi na kumponda Mengi..

Nadhani jibu la Pinda -- kwamba "mapapa" wale wana uhuru kwenda mahakamani wakipenda -- bila shaka lilimkata Hamad Rashid maini, na kuonekana a little bit silly.

Alichouliza HAMAD RASHID ni sahihi kabisa kama Mengi alikuwa na ushahidi wa hujuma za Mapapa angezipeleka kwenye vyombo stahiki.hivi wewe umewahi kumuona mmiliki wa CNN akitumia CNN kuwasakama wenzake? hata muuaji ana haki zake kama Mfungwa n.k.

Hamad RASHID alimkosoa waziri mkuu aliposema kuwa atakayeua ALBINO naye auliwe.yeye PINDA kama nani anawahukumu watu wakati vyombo vya sheria vipo?HAMAD RASHID ni katika wabunge makini bungeni na mwenye uwezo mkubwa kisiasa.Nyerere alikuwa akimtegemea sana HAMAD RASHID na kumpenda sana kwa uwezo wake wa siasa.Slaa hana hata nusu ya uwezo wa HAMAD RASHID.

HUYU jamaa siasa iko kwenye Damu yake na elewa kuwa wanasiasa hasa wa PEMBA kwao rushwa ni adui namba moja,hata viongozi wanaotokea ZNZ mara nyingi wamekuwa wakweli na waaminifu,huwezi kumkuta DR.Shein kwenye dili ya vitambulisho vya TAIFA kama MEMBE,MASHA,LOWASSA n.k

au uzalendo na kufuata maadili ya kazi kwa MAREHEMU DR.OMAR ALI JUMA. ulinganishe na SUMAYE,LOWASSA,MRAMBA,YONA,MAGUFURI,MKAPA n.k

HAMAD RASHID HANA SPEA YAKE BUNGENI.
 
Hicho chama atakachoanzisha mfadhili wake mkuu atakuwa RA maana tayari huyu jamaa alishaonyesha kuwa kibaraka wa RA (kumbuka reaction yake kwa Mengi when wakato wa issue ya mafisadi papa). Na kama atataka kujiunga vyama vingine, chama kama CHADEMA wasimkubali maana atakwenda kuwamaliza. Labda aende huko CCM kwa RA wake.
Kaka ndiyo tuseme Mengi ndiyo anaye sponsor Chadema? maana kwa mujibu wa RA yeye ni Nyangumi! kumbe heri nyangumi bora awe mchaga Khaa!
 
Ulijiunga ukiwa na miaka mingapi? kwani sifa ya kujiunga na chama sio umri wa miaka 18?

Habari ya kuacha ubunge mimi bado hujanishawishi mara useme unaenda SomaliLand mara unataka kuongeza elimu n.k
Mwenyekiti wako naye alisema anaenda kuongeza Elimu kwenye vyuo vitatu duniani haiku WORK OUT hujajifunza?bunge gani lenye PhD duniani nipe mfano? kuanzia Africa hadi ulaya na Marekani.

Waziri Pinda kasema kuwa mambo magumu jimboni kwako sasa labda umeshapiga ramli ukaona bora uondoke,kwani Mwalimu Nyerere alipoona amekoswakoswa kupinduliwa ndio akaja na gea ya kung'atuka.
Tushike lipi Mheshimiwa?


Zitto anataka kuvunga tu lakini ukweli ndio huu. Hata majibu yake yanaonyesha kama ameshikwa pabaya. Yaani anathubutu kukanusha kama Amani Kaboru hakuwa the man behind him katika kujikita kwenye siasa za CHADEMA.

Anakuja na hoja za ajabu eti alijiunga CHADEMA akiwa kidato cha tatu.... miaka 17. Mdogo wangu Zitto wake up. Mimi nakukubali sana kama mwana siasa. Lakini mwenendo wako wa siku za mwisho unaashiria the beginning of the end. Tena hasa pale ulipohitimisha kushawishi serikali kununua mitambo ya Dowans.

RA Hoye!
 
ninavofahamu mimi kwa historia iliyopo ukitoka Cuf kama umejilani mwenyewe.... kwa upande wa znz wananchi kule wana uhakika na baadhi ya watu wao ktk Cuf kwa upande wa znz
Ina maana CUF tu ndio inaweza kutetea maslahi ya ZNZ?
 
Alichouliza HAMAD RASHID ni sahihi kabisa kama Mengi alikuwa na ushahidi wa hujuma za Mapapa angezipeleka kwenye vyombo stahiki.hivi wewe umewahi kumuona mmiliki wa CNN akitumia CNN kuwasakama wenzake? hata muuaji ana haki zake kama Mfungwa n.k.

Hamad RASHID alimkosoa waziri mkuu aliposema kuwa atakayeua ALBINO naye auliwe.yeye PINDA kama nani anawahukumu watu wakati vyombo vya sheria vipo?HAMAD RASHID ni katika wabunge makini bungeni na mwenye uwezo mkubwa kisiasa.Nyerere alikuwa akimtegemea sana HAMAD RASHID na kumpenda sana kwa uwezo wake wa siasa.Slaa hana hata nusu ya uwezo wa HAMAD RASHID.

HUYU jamaa siasa iko kwenye Damu yake na elewa kuwa wanasiasa hasa wa PEMBA kwao rushwa ni adui namba moja,hata viongozi wanaotokea ZNZ mara nyingi wamekuwa wakweli na waaminifu,huwezi kumkuta DR.Shein kwenye dili ya vitambulisho vya TAIFA kama MEMBE,MASHA,LOWASSA n.k

au uzalendo na kufuata maadili ya kazi kwa MAREHEMU DR.OMAR ALI JUMA. ulinganishe na SUMAYE,LOWASSA,MRAMBA,YONA,MAGUFURI,MKAPA n.k

HAMAD RASHID HANA SPEA YAKE BUNGENI.


I agree with you totally! Wazanzibari meaning wote wa Pemba na Unguja tangu enzi ni watu waaminifu na waadilifu sana. Kama wapo ambao wamejiingiza kwenye masuala ya ulaghai na ufisadi watakuwa wanaiga kutoka Bara!

Hamad Rashid is a cool rational person, anaweza kuwa Rais mzuri na makini atakayeweza kuliokoa taifa hili kutokana na janga tulilonalo sasa hivi na kulirudishia Taifa heshima iliyokuwepo huko nyuma.
 
Zitto anataka kuvunga tu lakini ukweli ndio huu. Hata majibu yake yanaonyesha kama ameshikwa pabaya. Yaani anathubutu kukanusha kama Amani Kaboru hakuwa the man behind him katika kujikita kwenye siasa za CHADEMA.

Anakuja na hoja za ajabu eti alijiunga CHADEMA akiwa kidato cha tatu.... miaka 17. Mdogo wangu Zitto wake up. Mimi nakukubali sana kama mwana siasa. Lakini mwenendo wako wa siku za mwisho unaashiria the beginning of the end. Tena hasa pale ulipohitimisha kushawishi serikali kununua mitambo ya Dowans.

RA Hoye!

Hakuna sheria inayompa nafasi mtoto wa miaka 17 kuingia mkataba.uanachama wake ni batili.

hakuna anayeweza kupinga mchango wa Kaburu kwa Chadema,huyu ndiye aliyeipeleka Chadema Kigoma na kufanya watu wa familia moja kupigana kwa misingi ya CCM na Chadema labda mtu ambaye kaijua Chadema kupitia JF ndio anaweza kudanganywa.Alipokuwa Kaburu akihutubia mikutano ya Chadema na kampeni nzito,MBOWE alikuwa akishika mikoba ya Kaburu sembuse Zitto.
 
Nimefurahi kusikia kuwa CUF imekimbiwa na viongozi wengi kiasi hicho! Na bila shaka na malaki ya wanachama pia na ni sababu tosha ya chama kupoteza umaarufu wake hasa kwa Chadema.

Nyie katika CUF msianze kutafuta visingizio – eti CCm inashirikiana na Chadema kukikandamiza kwa sababu ni tishio na hivyo Chadema inakwezwa ili iwe No 2 kutoka CCM.

Tishio? Labda Visiwani tu, na kama huku Bara, basi tishio hilo angalau lilikuwa kweli mwaka 2000 ikilipofanikiwa kuipiku NCCR katika nafasi ya pili kwa kura.

Lakini sasa hivi kinaporomoka kwa kasi – wazungu wanasema “free-fall” na tutegemee wengi kukihama chama hicho – ingawa siamini iwapo hamad Rashid ni mmoja wao. Ushahidi wa kuporomoka ni Busanda – CUF iliambulia kura 900 tu ni karibu asilimia 5 ya kura walizopata Chadema!

Acheni kuilaumu Chadema kwa hilo, kila chama kiweke mbinu zake za kushinda uchaguzi na kama mbinu hizo ni kinyume cha sheria basi vyenyewe vyama vitajiju. Kama huwezi kuweka helikopta – hakuna haja ya kukiponda chama chenye kuweka helikopta. Kuna baadhi ya wanaCUF wanasema eti hiyo helikpta ya Chadema ni mchango wa CCM. Kwa nini wenyewe CCm wanapata kiwewe cha helikopta iwapo ndiyo wao waliwapa?

CUf wanashindwa kujibu tuhuma kama ilivyoripotiwa kwamba kuna kigogo kimoja cha CCM kinaifadhili CUF – na inasemekana kigogo huyo ni RA Fisadi na 1. Kwa hali hii – kwanini msikimbiwe?

Ingawa hakuna ushahidi mzito kuhusu ufadhili huu, lakini upo wa kimazingira ambao una nguvu kidogo – Profesa alipojitosa kwa nguvu kuwatetea ”mapapa” waliotajwa na Mengi.

Jee aliagizwa kufanya hivyo – kwa kulipa fadhila za ufadhili? Pia kuna uhusianio wa karibu sana baina ya RA na Jussa – jee huu umeelezwa sasawa? WanaCUF wanapohoji haya wanaengulwa!

Lwakatare bila shaka ni mmoja wao na kama unavyosema kaanza kusema uongo – basi uongo huo umesadia kukomba maelfu ya WanaCUF huko Bukoba waliojiunga na Chadema.

Vita yetu ni juu ya CUF kweli? hebu tumesahau kabisa adui yetu ni nani? kitendo cha kusema eti umefurahi ni unafiki na pia wewe ni mchekeshaji, sisemi vibaya ila dhamira inanisukuma kusema haya kuwa, vyama vya upinzani tunaitaji kusemea pamoja na si kubezana, tukisikia baya limekifika chama cha CUF tusikitike wote na wala si kuombeana mabaya.
 
Katika hali inayoonekana kuwa hali si shwari katika chama cha wananchi(CUF), mmoja wa wanachama na kiongozi nguli kabisa wa chama hicho, ndugu Hamad Rashid Mohammed, mbunge wa WAWI kule Pemba na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni anafikiria kuachana na chama hicho kwa kile anachodai kuwa kuwa ni kuwa uongozi wa chama hicho kukosa mikakati thabiti ya kukiongoza, na hata kukifanya kupoteza umaarufu wake wa awali.

Imethibitika kuwa bado kuna mazungumzo anafanya na uongozi wa juu wa chama hicho ambao kama hautabadilika atafuata nyayo za aliye kuwa naibu katibu mkuu wake mh. Wilfred Rwakatare aliyejiengua katika chama hicho na kujiunga na CHADEMA.

Kama mh. Hamad naye atajiengua basi hili litakuwa pigo lingine kubwa kwa CUF.

Dah!! Kama ni kweli basi huyu ni miongoni mwa wanasiasa asiyependa ubunge!!! WAWI si Pemba? Kama ni Pemba sijui aamie chama gani atakachouzika kwavile jamaa hawachagui mtu bali Chama!!! Nazani anatakiwa kuzikumbuka KURA ZA MARUHANI kabla hajamua!!!
 
Dah!! Kama ni kweli basi huyu ni miongoni mwa wanasiasa asiyependa ubunge!!! WAWI si Pemba? Kama ni Pemba sijui aamie chama gani atakachouzika kwavile jamaa hawachagui mtu bali Chama!!! Nazani anatakiwa kuzikumbuka KURA ZA MARUHANI kabla hajamua!!!
HR hawezi kuhama CUF.
 
Hakuna sheria inayompa nafasi mtoto wa miaka 17 kuingia mkataba.uanachama wake ni batili.

hakuna anayeweza kupinga mchango wa Kaburu kwa Chadema,huyu ndiye aliyeipeleka Chadema Kigoma na kufanya watu wa familia moja kupigana kwa misingi ya CCM na Chadema labda mtu ambaye kaijua Chadema kupitia JF ndio anaweza kudanganywa.Alipokuwa Kaburu akihutubia mikutano ya Chadema na kampeni nzito,MBOWE alikuwa akishika mikoba ya Kaburu sembuse Zitto.


Umechemsha! walau ungeuliza basi alijiunga vp. Kwa ntaarifa Zitto kaingia Chadema katika umri huo (17) kupitia umoja wa vijana wa Chadema ambao sharti la kujiunga ni kijana mwenye umri wa miaka 12-17.

Rejea katika ya chadema sura ya tano 5.1.7


V. SURA YA TANO
5.0 UANACHAMA
5.1 Sifa za kuwa MwanaChama/Wafuasi wa Chama
5.1.1 Awe raia wa Tanzania.
5.1.2 Awe na umri wa miaka 18 au zaidi
5.1.3 Awe na akili timamu
5.1.4 Awe anakubaliana na katiba, sera, kanuni na maadili ya Chama.
5.1.5 Awe anakubaliana na Itikadi na falsafa ya Chama.
5.1.6 Asiwe mwanaChama wa Chama kingine cha siasa baada ya kujiunga na CHADEMA.
5.1.7 Vijana wa umri wa miaka 12-17 ambao wanatimiza sifa 5.1.1, 5.1.3, 5.1.4, 5.1.5, na 5.1.6

 
Last edited:
Mh hana lolote huyo anatikisa kiberiti,siku zote alikuwa wapi ,tutawaona na kuwasikia tena wakila matapishi yao,siasa ni mchezo wa kuigiza ndugu zanguni,wanasiasa hawaaminiki
 
Back
Top Bottom