HAMAD RASHID katika Njama za Kumng'oa Maalim Seif?

CDM siyo dampo la wanasiasa wabovu kama akina Hamad Rashid, tamaa yake ya madaraka imemponza. kama vp ajiunge na Chama cha Magamba.
 
Umetokea kutoka kichaka kipi!!!?Kama ni mgonjwa utakuwa unatafuna meno yako mwenyewe.
 
Hamad si mwanasiasa makini kuwa Chadema . Uwezo wake wa kuongoza unawafaa wapemba tu n CUF Chadema hapawezi hata kidogo .Ila wacha waumane ndiyo chama chao kitakomaa
 
Siasa za TZ zimesheheni fitna, majungu, ubinafsi na kumsahau Mwenyezi Mungu kwa kukimbilia/kutegemea shirk.
 
ili kuwe na mabadiliko ya kimaendeleo lazima kuwe na msigishano wa mawazo na ikiwezekana physical mnyukano ndo inaleta heshma na maendeleo na mawazo sahihi.
Hamadi ni mlaini sana hiwezi ngoma ya CDM
 
Tayari mgogoro mkubwa wa kimaslahi binafsi umeikumba Cuf baada ya hamad Rashid kumpinga waziwazi maalim seif na sasa anamkakati wa kumngoa ktk nafasi ya katibu mkuu wa cuf na pia kutaka kuiteka kambi ya maalim seif huko Pemba. Mkakati huo umekuja baada ya hamad rashid na kundi lake kutumia muda mwingi kutembelea kisiwa cha Pemba ili kumkosanisha maalim seif na wakazi wa Pemba ambao idadi yake kubwa ni Cuf.
Hamad rashid amechukua hatua hiyo baada ya kugonga mwamba kupata nafasi ktk bunge kama mmoja ya viongozi wa kambi ya Upinzani bungeni baada ya CDM kumwekea vikwazo. pia hatua ya rashid inakuja baada ya kuongolewa nafasi ya mkuu wa kambi isiyorasmi bungeni ambapo habib mnyaa ameichukua.
habari amabazo zimeenea eti Mpango huo wa hamad rashid kutaka kutafautiana na Maalim unatoka na mpango hamad rasdhid kutaka kuahmia chadema. rashid licha ya kuonekana waziwazi kutomshinda maalim seif . mapngo huo unafanywa ili hamad aone ameonewa na apate sababu ya kuhamia cdm. kwani cdm ilihusishwa na hamad rashid kutaka kuwa mgombea mwenza wa dk slaa 2010

Source!?
 
CCM wamefanikiwa kuua upinzani Zanzibar na CUF kwa ujumla. Baada ya uchaguzi 2015 CUF itakuwa historia tu, na Maalim Seif atastaafu kama 1st Vice President kwa heshima zote na marupurupu ya CCM akiwa mzee wa miaka 72!

Tukumbuke kwamba Maalim Seif na wenzake walianzisha CUF 1992 baada ya kutofautiana na serikali/CCM (yeye akiwa waziri kiongozi - No.2). Alifukuzwa serikalini na kwenye CCM, akakosa jukwaa la kisiasa kwani Tanzania ilikuwa nchi ya chama kimoja tu mpaka 1992 tuliporuhusiwa vyama vingi. Kimsingi Maalim Seif, japo amejenga upinzani kwa kiasi kikubwa, nguvu yake kubwa ilitokana na chuki binafsi aliyokuwa nayo dhidi ya waliomyang'anya tonge mdomoni.

Baada ya kuukosa kosa uraisi wa Zanzibar 1995, 2000, 2005, 2010 kwa chini ya asilimia 1 (49.xx% vs. 50.xx%) huku umri ukiwa unakwenda mbio na afya kudorora, akaamua kuwalengesha Wazanzibari kwenye GNU (government of national unity), na kupewa tena cheo cha No.2 (1st Vice President). Huu ulikuwa mkakati wa CCM kumrudisha Maalim kundini kinyemela na kujisafishia wenyewe njia kwenda 2015. Ndio maana kauli zake za hivi karibuni kwamba sera zingine si zake ni utata (au uzee?) mtupu. Huyu sasa anaganga njaa tu na kutumia fedha za walipa kodi kuangalia afya yake. Ameshapata kile alichokipoteza 1988.

Prof Lipumba ana wakati mgumu kuifufua CUF bara kwa sababu hawezi kutofautiana na maamuzi ya serikali na mawaziri wake (collective responsibility). Wenye akili CUF watimkie vyama vingine ili hoja zao zipewe kipa umbele.

Huu ulikuwa wakati mwafaka wa kuimaliza CCM ya Vikongwe wanaotaka kuendesha nchi kijeshi. Wakati CHADEMA wanasambaratisha magamba bara, CUF wangekuwa wanaponda kichwa huko Zanzibar!

TLP na Mrema ni yale yale (NCCR-Marando, then TLP). Mrema anatafuta kiinua mgongo tu sasa hivi.

Anayejua mengine atuletee hapa jamvini na anayebisha leta hoja zako hapa :dance:
 
CDM siyo dampo la wanasiasa wabovu kama akina Hamad Rashid, tamaa yake ya madaraka imemponza. kama vp ajiunge na Chama cha Magamba.

Unajua unachokisema? Wapo wanasiasa wengi ndani ya Chadema si wanasiasa ni watu wa madeal tu tunajua ukipenda unageuka kiziwi na kipofu, hebu iangalie hiyo safu yako utajua nani mwanasiasa nani mfanyibiashara, GAMBA limeanza kuota ndani ya Chadema kumbuka 99.9% ya viongozi wenu ni wametokana na CCM na hawakuhama CCM kwa mapenzi ya uzalendo wengi walihama baada ya kushindwa kipesa, wengi wanamsingi mkubwa tu siasa za RUSHWA. TAFAKARI mwenyewe MWENYEKITI KUFANYA BIASHARA YA ZAIDI MIL. 180 NA CHAMA HUKU HATA BAADHI YA VIONGOZI HAWAJUI? Biashara za MILANGO ya UANI zimemnufaisha MBOWE na INNER CIRCLE YAKE, jielemishe kabla ya kuongea. YOU CAN NEVER TURN A ***** TO A HOUSEWIFE.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Tayari mgogoro mkubwa wa kimaslahi binafsi umeikumba Cuf baada ya hamad Rashid kumpinga waziwazi maalim seif na sasa anamkakati wa kumngoa ktk nafasi ya katibu mkuu wa cuf na pia kutaka kuiteka kambi ya maalim seif huko Pemba. Mkakati huo umekuja baada ya hamad rashid na kundi lake kutumia muda mwingi kutembelea kisiwa cha Pemba ili kumkosanisha maalim seif na wakazi wa Pemba ambao idadi yake kubwa ni Cuf.<br />
Hamad rashid amechukua hatua hiyo baada ya kugonga mwamba kupata nafasi ktk bunge kama mmoja ya viongozi wa kambi ya Upinzani bungeni baada ya CDM kumwekea vikwazo. pia hatua ya rashid inakuja baada ya kuongolewa nafasi ya mkuu wa kambi isiyorasmi bungeni ambapo habib mnyaa ameichukua.<br />
habari amabazo zimeenea eti Mpango huo wa hamad rashid kutaka kutafautiana na Maalim unatoka na mpango hamad rasdhid kutaka kuahmia chadema. rashid licha ya kuonekana waziwazi kutomshinda maalim seif . mapngo huo unafanywa ili hamad aone ameonewa na apate sababu ya kuhamia cdm. kwani cdm ilihusishwa na hamad rashid kutaka kuwa mgombea mwenza wa dk slaa 2010
<br />
<br />
Another PASUA KICHWA in JF
 
Hongera Malaria Sugu kwa taarifa hiyo. Duh! Umebadilika sana siku hizi!

Ndivyo wenye magamba wanakuwa na wanatakiwa kuwa mara wakijivua magamba. Lakini kama gamba ni gumu sana na linawashinda kulivua, waweza kuvuliwa na watu wengine.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom