Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,494
- 41,002
Sasa hivi hasira ya Watanganyika ni kubwa juu ya Hamad, Mzanzibari aliyeamua kushirikiana na CCM kuzuia mabadiliko yoyote ambayo watanganyika wanayataka katika Taifa lao.
Ukweli ni kuwa vyama vikuu vya siasa kwa Zanzibar ni CCM na CUF, licha ya kwamba vyama vingine kama CHADEMA, NCCR, UDP, n.k. navyo vipo Zanzibar. Hivi vyama vingine kwa upande wa Zanzibar vinajitambua kuwa siyo popular, na ndiyo maana CUF kule Zanzibar inafanya mambo yake bila kuvishirikisha hivi vyama vingine vya upinzani kwa namna yoyote ile. Hivi vyama vingine vinaifahamu nafasi yao kule Zanzibar, na ndiyo maana hata pale CUF wanapofanya mambo yao kama vile hakuna vyama vingine vya upinzani, hatujasikia jitihada za hali ya juu za kukwamisha malengo na mipango ya CUF kule Zanzibar. Kinachoshangaza kwa upande wa Hamad Rashid, ni kwa nini busara ya namna hiyo hana inapokuja kwa masuala ya mwungano?
Kwa upande wa Tanganyika vyama vikuu vya siasa ni CCM na CHADEMA. Hivi ndivyo vyama vinavyoungwa mkono na Watanganyika walio wengi. Kwa nini Hamad, asiye Mtanganyika, baada ya kufanya anayoyataka kule Zanzibar bila ya kuingiliwa na Mtanganyika yeyote, awe na ujasiri wa kuja kuzuia matakwa ya Watanganika zaidi ya milioni 43? Huyu Hamad amekosa hekima, staha na busara ambayo binadamu yeyote mstaarabu alistahili kuwa nayo.
Serikali inayotamkwa kuwa ni ya mwungano, kiutendaji ni serikali ya Tanganyika. Wazanzibar wana serikali yao na bunge lao kule Zanzibar ambalo kila siku wanapitisha mambo yao yote wanayoyataka bila ya kuingiliwa na Mtanganyika yeyote, na tena wakihojiwa kidogo wanapokiuka katiba ya Mwungano wanakuwa wakali sana.
Mambo yanayojadiliwa kwenye bunge la Mwungano, zaidi ya 95% yanahusu Tanganyika lakini mbunge wa Zanzibar anayewakilisha wazanzibari 5,000 anampinga mbunge wa Sengerema anayewakilisha Watanganyika 800,000. Mbunge huyo huyo anayewakilisha wazanzibari 5,000 anapewa posho, VX na kila kitu na serikali ya Mwungano, huku diwani wa Tanganyika anayewakilisha watanganyika 100,000 hapewi hata pikipiki. Mbaya zaidi, mbunge kama Hamad ambaye anapata kisicho stahili yake bado anakuwa kikwazo kwa wale wanaomfadhili.
Tukiacha porojo na misemo ya kiswahili kuwa umoja ni nguvu, hivi Tanganyika inafaidika nini kuwa katika kiini macho hiki cha mwungano, zaidi ya maudhi yanayofanywa na Wazanzibari dhidi ya Watanganyika? Tunatumia gharama kubwa kuishi katika mwungano usio na faida. Gharama tunazozipata ni pamoja na kuhudumia ofisi ya makamu wa Rais ambayo hatuhitaji, wabunge wa Zanzibar; na mbaya zaidi ni sychological cost ambayo kila mara tunasababishiwa na Wazanzibari kama hili la kuingilia masuala yasiyowahusu huku kule kwao wamefanya bila kuingiliwa. Hawa akina Kafulila, Lipumba, Mrema, ni haki yao kuingilia maumuzi yeyote ya Tanganyika lakini siyo Hamad na wabunge wenzake wa Zanzibar kutaka kutuamulia sisi Watanganyika wakati wao tumewapa haki hiyo kule kwao Zanzibar.
Wabunge Wazanzibari washiriki kutoa hoja kuhusiana na wizara zile za mwungano tu na si vinginevyo.
Ifike wakati Watanganyika tutoe kauli juu ya hawa Wazanzibari ambao wameanza kupitiliza mipaka ya uvumilivu. Tuliungana kwa kuamini kuwa umoja huo ungetusaidia, na hasa wakati wa vita baridi. Kama hatuwezi kutaja faida tunazozipata Watanganyika kwa kuungana na Zanzibar lakini tukaweza kuorodhesha hasara, basi mwungano huu hauna utashi.
Ninachojiuliza hasa ni kuwa huyu Hamad Rashid ni nani kwa Watanganyika, na Tanganyika inamhusu nini yeye kama Mzanzibari? Pesa tunayotaka matumizi yake yadhibitiwe na upinzani, Zanzibar inachangia kiasi gani? Wizi mkubwa wa fedha ya serikali hutokea kwenye miradi ya barabara, kwenye Halmashauri, kwenye ujenzi wa shule, miradi ya maji, n.k. Wizara zote zinazosimamia mambo hayo siyo za mwungano, na Wazanzibari wanazo zao kule kwao. Sasa kwa nini Hamad anataka atuamulie juu ya mbunge gani wa upinzani awe mwenyeketi wa kamati za bunge wa kusimamia haya?
Wazanzibari wakiendelea na fitina dhidi ya Watanganyika, nina hakika Watanganyika wengi tutataka serikali tatu kwaajili ya majaribio, tukiona wanazidi kutuchokonoa, tutawaachilia, tuendelee nao kama majirani zetu na siyo kama wanandoa.
Ukweli ni kuwa vyama vikuu vya siasa kwa Zanzibar ni CCM na CUF, licha ya kwamba vyama vingine kama CHADEMA, NCCR, UDP, n.k. navyo vipo Zanzibar. Hivi vyama vingine kwa upande wa Zanzibar vinajitambua kuwa siyo popular, na ndiyo maana CUF kule Zanzibar inafanya mambo yake bila kuvishirikisha hivi vyama vingine vya upinzani kwa namna yoyote ile. Hivi vyama vingine vinaifahamu nafasi yao kule Zanzibar, na ndiyo maana hata pale CUF wanapofanya mambo yao kama vile hakuna vyama vingine vya upinzani, hatujasikia jitihada za hali ya juu za kukwamisha malengo na mipango ya CUF kule Zanzibar. Kinachoshangaza kwa upande wa Hamad Rashid, ni kwa nini busara ya namna hiyo hana inapokuja kwa masuala ya mwungano?
Kwa upande wa Tanganyika vyama vikuu vya siasa ni CCM na CHADEMA. Hivi ndivyo vyama vinavyoungwa mkono na Watanganyika walio wengi. Kwa nini Hamad, asiye Mtanganyika, baada ya kufanya anayoyataka kule Zanzibar bila ya kuingiliwa na Mtanganyika yeyote, awe na ujasiri wa kuja kuzuia matakwa ya Watanganika zaidi ya milioni 43? Huyu Hamad amekosa hekima, staha na busara ambayo binadamu yeyote mstaarabu alistahili kuwa nayo.
Serikali inayotamkwa kuwa ni ya mwungano, kiutendaji ni serikali ya Tanganyika. Wazanzibar wana serikali yao na bunge lao kule Zanzibar ambalo kila siku wanapitisha mambo yao yote wanayoyataka bila ya kuingiliwa na Mtanganyika yeyote, na tena wakihojiwa kidogo wanapokiuka katiba ya Mwungano wanakuwa wakali sana.
Mambo yanayojadiliwa kwenye bunge la Mwungano, zaidi ya 95% yanahusu Tanganyika lakini mbunge wa Zanzibar anayewakilisha wazanzibari 5,000 anampinga mbunge wa Sengerema anayewakilisha Watanganyika 800,000. Mbunge huyo huyo anayewakilisha wazanzibari 5,000 anapewa posho, VX na kila kitu na serikali ya Mwungano, huku diwani wa Tanganyika anayewakilisha watanganyika 100,000 hapewi hata pikipiki. Mbaya zaidi, mbunge kama Hamad ambaye anapata kisicho stahili yake bado anakuwa kikwazo kwa wale wanaomfadhili.
Tukiacha porojo na misemo ya kiswahili kuwa umoja ni nguvu, hivi Tanganyika inafaidika nini kuwa katika kiini macho hiki cha mwungano, zaidi ya maudhi yanayofanywa na Wazanzibari dhidi ya Watanganyika? Tunatumia gharama kubwa kuishi katika mwungano usio na faida. Gharama tunazozipata ni pamoja na kuhudumia ofisi ya makamu wa Rais ambayo hatuhitaji, wabunge wa Zanzibar; na mbaya zaidi ni sychological cost ambayo kila mara tunasababishiwa na Wazanzibari kama hili la kuingilia masuala yasiyowahusu huku kule kwao wamefanya bila kuingiliwa. Hawa akina Kafulila, Lipumba, Mrema, ni haki yao kuingilia maumuzi yeyote ya Tanganyika lakini siyo Hamad na wabunge wenzake wa Zanzibar kutaka kutuamulia sisi Watanganyika wakati wao tumewapa haki hiyo kule kwao Zanzibar.
Wabunge Wazanzibari washiriki kutoa hoja kuhusiana na wizara zile za mwungano tu na si vinginevyo.
Ifike wakati Watanganyika tutoe kauli juu ya hawa Wazanzibari ambao wameanza kupitiliza mipaka ya uvumilivu. Tuliungana kwa kuamini kuwa umoja huo ungetusaidia, na hasa wakati wa vita baridi. Kama hatuwezi kutaja faida tunazozipata Watanganyika kwa kuungana na Zanzibar lakini tukaweza kuorodhesha hasara, basi mwungano huu hauna utashi.
Ninachojiuliza hasa ni kuwa huyu Hamad Rashid ni nani kwa Watanganyika, na Tanganyika inamhusu nini yeye kama Mzanzibari? Pesa tunayotaka matumizi yake yadhibitiwe na upinzani, Zanzibar inachangia kiasi gani? Wizi mkubwa wa fedha ya serikali hutokea kwenye miradi ya barabara, kwenye Halmashauri, kwenye ujenzi wa shule, miradi ya maji, n.k. Wizara zote zinazosimamia mambo hayo siyo za mwungano, na Wazanzibari wanazo zao kule kwao. Sasa kwa nini Hamad anataka atuamulie juu ya mbunge gani wa upinzani awe mwenyeketi wa kamati za bunge wa kusimamia haya?
Wazanzibari wakiendelea na fitina dhidi ya Watanganyika, nina hakika Watanganyika wengi tutataka serikali tatu kwaajili ya majaribio, tukiona wanazidi kutuchokonoa, tutawaachilia, tuendelee nao kama majirani zetu na siyo kama wanandoa.