Elections 2010 Halmashauri zilizo chini ya upinzani

Haika

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,348
559
Chonde chonde, wana wa mageuzi, japo dalili zinaonekana kuwa uraisi haujashinda, mimi naona umeshinda SANA. Halmashauri nyingi sana, zenye nguvu ya watu na rasilimali ziko mikononi mwenu.
Fanyeni hima mujipange, mufanye kazi, ionekane, hii ndio sehemu inayojenga au kubomoa maendeleo ya mwananchi mmoja mmoja, kama kweli tuna lengo la kuinua hali ya wananchi mmojammoja, hapa ndio kwa kuanzia,
kuhakikisha halmashauri zinafanya kazi vizuri, matumizi, mipango, ushirikishwaji, huu ndio wakati wa kutekeleza kwa vitendo.
Tuko nyuma yenu.
Mfano mzuri ni wa halmashauri ya Moshi mjini, asilimia kubwa ya wafanyakazi wana nidhamu ya kazi, rushwa iko chini kiasi.
jamani, haya ndio maandalizi ya kampeni ijayo.
TANGU MWANZO HALMASHAURI ZILIZO CHINI YA UPINZANIA ZIONYESHE UTOFAUTI.

DR Wetu, KAzi kubwa mnayo kusimamia hawa waliochaguliwa, kufanya kazi ya watu. Najua baadhi yao ni wageni sana kwenye siasa, ila wana moyo sana. Chonde chonde haya isiwepo ya kukosoana, kuangalia udini au ukabila au jinsia, kama kawaida, tunasema.

PEOPLES!!!!
POWER!!!
 
Back
Top Bottom