Halmashauri ya Temeke mnatia aibu wananchi wenu wana umasikini wa kutupwa na kero nyingi amjazifanyia kazi mnabaki kupambana na Amba Rutty

TheDreamer Thebeliever

JF-Expert Member
Feb 26, 2018
2,490
3,534
Habari wadau..!

Katika moja ya Halmashauri ambazo zina changamoto nyingi sana ni hii Temeke kwa hapa Dar es Salaam.

Temeke ina kero nyingi sana zikiwapo matumizi ya madawa ya kulevya kwa vijana,upungufu wa madarasa, utoro wa wanafunzi, umasikini, uporajwi wa ardhi za wananchi, upungufu wa madarasa na vifaa vya kufundishia, zahanati zipo chache sana ukilinganisha na idadi ya wananchi,rushwa n.k.

Kero zipo nyingi sana lakini hii Halmashauri imejikita kumshambulia msanii Ammber Rutty ambaye naye ni binadamu lakini kitendo wanachokifanya ni kama kumshushia heshima yake katika jamii.

Sidhani kama kuna ubaya kwa msanii huyu kutembelea shule ambayo ana mtoto pale anasoma, hapo hakuna kosa lolote alilofanya.

Si kweli kwamba baada ya kosa alilofanya la kuliwa msambwanda na kuhukumiwa moja ya hukumu aliyopewa ilimfanya kuzuiwa kutoshiriki maswala ya kijamii.

Kwa nn tu iwe kwa Ammber Rutty tu na wala sio kina Mwijaku,Bell Nas,Nandy na wengine wengi ambao walishawai kufanya matukio yanayofanana na ya Amber Rutty.

Binafsi nasimama na Ammber Rutty na ikiwezekana Ammber Rutty aifungulie mashitaka Halmashauri hii kwa kumchafulia jina lake pasipo sababu za msingi.
 
Back
Top Bottom