Ibanda1
JF-Expert Member
- Jul 18, 2015
- 705
- 1,092
Wasalaam wanajamvi,
Halmashauri ya Mbozi inapatikana katika mkoa mpya wa Songwe na ni moja kati ya HJalmashauri kongwe sana lakini pia Wilaya ya Mbozi imejizolea umaarufu kutokana na uwepo wa kimondo ambapo tulikuwa tukiisoma tangu shule ya msingi.
Niende kwenye hoja moja kwa moja, katika ofisi za halmashauri ya Mbozi idara ya utumishi pamekuwa na watumishi wasio waadilifu wapenda rushwa na wanajisifu kuwa ukiwa na mkono mfupi utaishia kupigwa kalenda.
Kuna utaratibu wa taasisi za fedha kwenda kuingiza makato ya mikopo ya waajiri kupitia mfumo wa Lawson, kiutaratibu bank officer kazi yake ni kwenda kuthibitisha kama makato yameingizwa kwa usahihi lakini katika hali ya kushangaza hawa maafisa utumishi wamejitengenezea mradi wa kujipatia fedha kwa njia isiyo rasmi kwani bank officer ukienda kufanya capturing kama hujawapatia pesa utazungushwa hata mwezi mzima huku ukiambiwa network hamna ila wanaingia watu wa benki nyingine, kazi wanawahudumia baada ya kuwapa rushwa tena wanajipangia kiasi kabisa wanahitaji elfu hamsini aisee imagine una application moja tu ya mteja haizidi hata million tano na umesafiri kutoka Tunduma alafu mtu anakuomba rushwa ya 50k?
Kibaya zaidi DED pamoja DHRO wanafahamu huu uozo wa hawa watumishi ila wanawafumbia macho, huu mchezo mmeucheza kwa muda mrefu nadhani mnatakiwa kuuacha mara moja la sivyo mtapoteza kazi kwa sababu ya elfu hamsini.
Halmashauri ya Mbozi inapatikana katika mkoa mpya wa Songwe na ni moja kati ya HJalmashauri kongwe sana lakini pia Wilaya ya Mbozi imejizolea umaarufu kutokana na uwepo wa kimondo ambapo tulikuwa tukiisoma tangu shule ya msingi.
Niende kwenye hoja moja kwa moja, katika ofisi za halmashauri ya Mbozi idara ya utumishi pamekuwa na watumishi wasio waadilifu wapenda rushwa na wanajisifu kuwa ukiwa na mkono mfupi utaishia kupigwa kalenda.
Kuna utaratibu wa taasisi za fedha kwenda kuingiza makato ya mikopo ya waajiri kupitia mfumo wa Lawson, kiutaratibu bank officer kazi yake ni kwenda kuthibitisha kama makato yameingizwa kwa usahihi lakini katika hali ya kushangaza hawa maafisa utumishi wamejitengenezea mradi wa kujipatia fedha kwa njia isiyo rasmi kwani bank officer ukienda kufanya capturing kama hujawapatia pesa utazungushwa hata mwezi mzima huku ukiambiwa network hamna ila wanaingia watu wa benki nyingine, kazi wanawahudumia baada ya kuwapa rushwa tena wanajipangia kiasi kabisa wanahitaji elfu hamsini aisee imagine una application moja tu ya mteja haizidi hata million tano na umesafiri kutoka Tunduma alafu mtu anakuomba rushwa ya 50k?
Kibaya zaidi DED pamoja DHRO wanafahamu huu uozo wa hawa watumishi ila wanawafumbia macho, huu mchezo mmeucheza kwa muda mrefu nadhani mnatakiwa kuuacha mara moja la sivyo mtapoteza kazi kwa sababu ya elfu hamsini.