Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ofisi ya Kata ya Mpera yawatoza Tsh 2000 Vijana wanaotuma barua za maombi ya kazi za ukusanyaji wa Anuani za Makazi

kimadui

Member
Jun 13, 2021
32
46
Habari za wakati huu wana jamvi,

Billa kupoteza wakati Kuna kitu jana nimekishuhudia nikabaki kinywa wazi. Kuhusu hizi nafasi ambazo serikali imekuwa ikitangaza hivi karibuni Katika halmashauri na wilaya mbali mbali nchini kuhusu kazi ya kukusanya na kuweka vibao vya ANWANI ZA MAKAZI.

Jambo la kusikitisha nililoliona Katika halmashauri ya manispaa ya Tabora ofisi ya kata ya Mpera ni kwamba watu wakipeleka barua zao Ili zisainiwe na watendaji wa kata na mtaa baada ya kusainiwa wanaambiwa watoe shilingi elfu 2000/=.

Kijana mmoja akajaribu kuhoji "mbona kwenye maelekezo ya tangazo hakuna mahali tumeambiwa tulipe hio elfu 2000/=?"

Akaambiwa "hayo ndo maelekezo tuliyopewa" na akaoneshwa orodha ya waliotoa hio pesa idadi ni kubwa kidogo.

Basi yule kijana akamwambia "mimi sina hio pesa maana sikuona maelekezo yake"

Akaambiwa "wewe una kiasi gani hapo ulipo Ili tukusaidie?"

Yule kija akawajibu "Sina kiasi chochote,"

Akaambiwa "haya kama huna basi katoe hio barua yako copy ulete copy ya hio barua."

Nikabaki najiuliza.

1. Ina maana serikali imetoa maelekezo watu walipie pesa kuomba hizo nafasi?

2. Je, waliotoa pesa hizo pesa zinapelekwa wapi?

3. Je, ambao hawajatoa pesa kama huyo kijana atakuwa na ukakika wakupata hio kazi hata kama anakidhi vigezo?

4. Inawezekana waliotoa pesa ndo wakapewa priority kuliko ambao hawajatoa?

5. Ikiwa ajira hii ya siku chache hivi mtu analipishwa je zile kazi za muda mrefu huwa watu wanatozwa kiasi gan?

Maswali ni mengi itoshe kusema inasikitisha sana.

Wasalaam
 
Fursa mtu wangu watu wanachangamkia fursa, mishahara yenyewe haitoshi unataka wafe njaa..kila mtu atakula mezani pake, hata mkuu wa nchi kasema watu wale kwa urefu wa kamba zao.

Kama vile mwendazake alivyoruhusu polisi wapate za kiwi.

Halafu mkono mtupu haulambwi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Naona mnanishambulia tu kumbe mimi ndo nipo nyuma ya wakati Ina maana Siku hizi hata kazi za serikali mpaka utoe kitu kidogo? Haya mambo tulizoea huko kwenye sekta binafsi sio serikalini
 
Hela inayoombwa na weo au veo ni ya nje ya ofisi na sio maelekezo. Wanaomba ila ukiwaambia huna hawana namna watapitisha tu barua yako kwa mhuri wao. Cha kufanya ukikutana na changamoto kama hiyo katika eneo lako,washirikishe viongozi wako wa mtaa na uzuri wake wote wanakaa jengo moja. Mtaarifu mwenyekiti wa mtaa/kijiji au duwani wako wa kata.
Awamu hii Ccm ipo imara kuliko nyakati zote, Ahsante
 
Kuna watu wanna vipaji vya ubishi na ubush lower.

Hawajui hali halisi.

Haya, kakataa kukupitishia barua yako na huna kitu cha kumfanya
Nyie ndo Huwa hamjielewi hivi nani anatakiwa ajue Hali halisi kati ya anayetafuta ajira na aliye ndani ya ajira? Mwenye ajira si ndo anatakiwa amhurumie ambae Hana maana uhalisia wa maisha unamuumiza Sana asie kua nacho.

Wala hii sio ishu ya ubush lawyer kutambua haki zako na mipaka ya kazi ya mtu mwingine sio ubush lawyer ni jukumu lako na ni haki yako zinduka ndugu
 
Hiyo mbona kawaida huyo jamaa nae anazingua kutoa elfu 2 wakati ww unaenda kupata zaidi ya hizo .
 
Nyie ndo Huwa hamjielewi hivi nani anatakiwa ajue Hali halisi kati ya anayetafuta ajira na aliye ndani ya ajira? Mwenye ajira si ndo anatakiwa amhurumie ambae Hana maana uhalisia wa maisha unamuumiza Sana asie kua nacho.

Wala hii sio ishu ya ubush lawyer kutambua haki zako na mipaka ya kazi ya mtu mwingine sio ubush lawyer ni jukumu lako na ni haki yako zinduka ndugu
Na nyie jifunzeni kuheshimu muda wa watu.

Hivi unafikiri kazi ya WEO Ni kukaa tu ofisini kusubiri watu walete barua zao ugonge mihuri?

Watu kama nyie ningekiwa Mimi, Wala hata nisingepitisha barua yako.
 
Back
Top Bottom