Halmashauri ya Bunda tafakarini hili la fedha zinazoletwa kwa ajili ya maendeleo ya shule.

proff g

Senior Member
Jul 16, 2016
113
55
Katika mwaka huu wa masomo 2020 serikali imejitahidi kuleta fedha kwa ajili ya maendeleo hasa maboresho katika miundombinu ya shule pamoja na kujenga miundo mbinu mipya ya shule hizi hasa za Halmashauri ya wilaya ya Bunda. changamoto iliyopo, pamoja nakuletwa fedha hizi bado halmashauri imeshindwa kutoa ushauri kwenye matumizi ya fedha hizi kwa mfano ipo shule x iliyo ingiziwa kiasi cha sh milioni 80 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni. chakushangaza shule hii haina maabara, haina maktaba madarasa ya kujifunzia hayatoshi, walimu hawana meza na viti vya kukalia. Ombi langu mkuregenzi wa Halmashauri ya wilaya Bunda pitieni upya mahitaji ya msingi ya shule hizi kwasababu kuto kukamilishwa kwa mahitaji haya shule hizi zimekuwa na maendeleo hafifu ya kitaaluma.
 
Hii wilaya inamatatizo inahitaji kufumuliwa upya hasa DEO na DED
Mkuu hii wilaya inachangamoto sana usimamizi katika idara ya elimu sekondari na msingi kunachangamoto kubwa lakini cha kushangaza hakuna hatua madhubuti zinazochukuliwa
 
Back
Top Bottom