tatamajuva
Member
- Sep 11, 2019
- 74
- 83
Hili la wataalamu mbalimbali ngazi. Ya kata na Kijiji Kama afisa maendeleo, mifugo,kilimo,ustawi wa jamii wame base katika kukusanya mapato kwa maelekezo ya wakurugenzi wa miji,halmashauri,manispaa na majiji.
Kwasasa hawatekelezi majukumu yao waliyosomea na kusababisha kurudisha nyuma maendeleo ya sekta mbalimbali .
Wakulima,wafugaji,vikundi vya ujasiriamali havitembelewi /hawatembelewi na wataalamu hao.
Kwasasa Hali ni mbaya katika sekta mbalimbali kwani ukisimamia sekta moja nyengine zinakufa.
Chondechonde serikali iweke agents au iweze kuajiri maafisa biashara katika Kila kata kwa ajili ya kukusanya ushuru.
Maafisa hawakai maofisini na hawatembelei wananchi wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali.
Tutakusanya mapato lakini tutarudi nyuma sana,kwani watu watalima kienyeji,watafuga kienyeji.
Jamani hata katika masika hii hawatembelei wananchi.
Fanyeni utafiti mtagundua Hilo.
Kwasasa hawatekelezi majukumu yao waliyosomea na kusababisha kurudisha nyuma maendeleo ya sekta mbalimbali .
Wakulima,wafugaji,vikundi vya ujasiriamali havitembelewi /hawatembelewi na wataalamu hao.
Kwasasa Hali ni mbaya katika sekta mbalimbali kwani ukisimamia sekta moja nyengine zinakufa.
Chondechonde serikali iweke agents au iweze kuajiri maafisa biashara katika Kila kata kwa ajili ya kukusanya ushuru.
Maafisa hawakai maofisini na hawatembelei wananchi wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali.
Tutakusanya mapato lakini tutarudi nyuma sana,kwani watu watalima kienyeji,watafuga kienyeji.
Jamani hata katika masika hii hawatembelei wananchi.
Fanyeni utafiti mtagundua Hilo.