Halmashauri mkoani Mara zagomea fedha za mrabaha kutoka mgodi wa CATA Mine

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,483
54,853
Halmashauri mkoani Mara zagomea fedha za mrabaha kutoka mgodi wa CATA Mine kwa kukiuka mkataba.
mine.jpg

Picha inayoonekana hapo juu kwa hisani ya Mtandao.

Uongozi wa Halmasdhauri mbili za mkoa wa Mara,zimekataa kupokea kiasi cha Shilingi Milioni 40 kama mrabaha kutoka Mgodi wa dhahabu wa CATA Mine kwa madai ya kukiukwa kwa mkataba uliowataka kulipwa dola laki tano kama mrabaha kwa Halmashauri hizo za butiama na musoma vijijini.

Hatua hiyo imechukuliwa na viongozi wa halmashauri hizo mbili za musoma vijijini na Butiama ulipo mgodi huo, ikiwa ni siku moja tu baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kuagiza kupitiwa upya kwa mikataba yote ya sekta ya madini katika kuhakikisha raslimali hiyo inawanufaisha watanzania.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Butiama Bi. Annarose Nyamubi,amewaagiza madiwani hao kuchukua hatua ya kudhibiti mianya yote ya upotevu wa fedha ili kuhakikisha fedha zinazopatikana zinatumika kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Chanzo: ITV
 
Duuuh walipwe na wao malimbikizo yao yote!
Nikikumbuka mgodi wa Buhema musoma vijijin yaliyotokea, nalia zaodi ya magu jana
 
Meremeta na Tangold viliishia wapi?maana eti meremeta ilikua ya usalama inachimba madini
 
kwahiyo hadi rais aseme mikataba ipitiwe ndip mnajidai eti mkataba umekiukwa, siku zote mlikuwa mnashirikiana nao kuiba hizo 500,000$, leo ndio mnajidai mnakataa..., watumbuliwe tu.
 
Halmashauri mkoani Mara zagomea fedha za mrabaha kutoka mgodi wa CATA Mine kwa kukiuka mkataba.
mine.jpg

Picha inayoonekana hapo juu kwa hisani ya Mtandao.

Uongozi wa Halmasdhauri mbili za mkoa wa Mara,zimekataa kupokea kiasi cha Shilingi Milioni 40 kama mrabaha kutoka Mgodi wa dhahabu wa CATA Mine kwa madai ya kukiukwa kwa mkataba uliowataka kulipwa dola laki tano kama mrabaha kwa Halmashauri hizo za butiama na musoma vijijini.

Hatua hiyo imechukuliwa na viongozi wa halmashauri hizo mbili za musoma vijijini na Butiama ulipo mgodi huo, ikiwa ni siku moja tu baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kuagiza kupitiwa upya kwa mikataba yote ya sekta ya madini katika kuhakikisha raslimali hiyo inawanufaisha watanzania.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Butiama Bi. Annarose Nyamubi,amewaagiza madiwani hao kuchukua hatua ya kudhibiti mianya yote ya upotevu wa fedha ili kuhakikisha fedha zinazopatikana zinatumika kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Chanzo: ITV
Janja janja toka 1b mpaka 40mil
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom