Nyasa Girl
Member
- Jul 11, 2017
- 10
- 19
Nikiwa kama mwanachama wa muda mrefu naandika kwa masikitiko makubwa sana, mambo yanayofanywa na uongozi wa CCM mkoa wa Tabora wakiongozwa na katibu wa CCM mkoa.
Naamini jukwaa hili ndio njia pekee ya kufikisha malalmiko ambayo yataweza kufika kwa urahisi kwenye uongozi wa CCM Taifa na hatimaye hatua stahiki zichukuliwe katika kukinusuru chama mkoani Tabora hasa, jimbo la Tabora mjini na halmashauri yake.
Nikiwa mjumbe wa mkutano mkuu wa wilaya wilaya ya Tabora ,nimeshuhudia mengi sana ambayo kimsingi chama kinatakiwa kuchukua hatua madhubuti, mchakato wa kupata wawakilishi ndani ya CCM watakaokwenda kushindana na wagombea wa vyama vingine katika uchaguzi mkuu ulikuwa na mambo mengi sana.
Mimi nitayataja mambo ambayo wanachama wengi na mimi nikiwamo tuliyoyashuhudia na yaliyotusikitisha na ambayo yamesababishwa na viongozi wa CCM mkoa wa Tabora
Mambo hayo ni yafuatayo:
Tatizo kubwa ni uongozi mzima wa CCM mkoa ambao tayari wameshakula pesa za wagombea wao ambao wameshashindwa kwenye kura za maoni na hivyo kulazimisha wawe wagombea
Tunaamini malalamiko yetu yatakifikia chama cha mapinduzi na kuhakikisha wananusuru mgawanyiko unaoletwa na viongozi wa CCM mkoa kwa kulazimisha wagombea wao na kuacha kufuata machaguo ya wajumbe ambao ni wawakilishi wa wanachama walio wengi.
Tunaomba chama taifa, chukueni hatua madhubuti kwani uongozi wa CCM mkoa hawakitakii mema chama cha mapinduzi mkoani Tabora, tunaomba machaguo yetu kuanzia ngazi ya udiwani na wabunge yazingatiwe kwani ndio machaguo yetu na ndio yanayouzika na kukubalika kwa wananchi.
Ndimi,
NYASA MALEMBEKA
Mwakilishi wa wajumbe, Wilaya ya Tabora
Naamini jukwaa hili ndio njia pekee ya kufikisha malalmiko ambayo yataweza kufika kwa urahisi kwenye uongozi wa CCM Taifa na hatimaye hatua stahiki zichukuliwe katika kukinusuru chama mkoani Tabora hasa, jimbo la Tabora mjini na halmashauri yake.
Nikiwa mjumbe wa mkutano mkuu wa wilaya wilaya ya Tabora ,nimeshuhudia mengi sana ambayo kimsingi chama kinatakiwa kuchukua hatua madhubuti, mchakato wa kupata wawakilishi ndani ya CCM watakaokwenda kushindana na wagombea wa vyama vingine katika uchaguzi mkuu ulikuwa na mambo mengi sana.
Mimi nitayataja mambo ambayo wanachama wengi na mimi nikiwamo tuliyoyashuhudia na yaliyotusikitisha na ambayo yamesababishwa na viongozi wa CCM mkoa wa Tabora
Mambo hayo ni yafuatayo:
- Katibu wa CCM mkoa , ndugu Solomon Kasaba kuwa na mgombea wake kabla ya uchaguzi ambaye ni ndugu ADEN RAGE na AMINA KABOYONGA, ambaye pia alikamatwa na TAKUKURU.
- Katibu wa CCM mkoa , mwenezi wa ccm mkoa, ndugu Majaliwa Majaliwa na Mjumbe wa kamati ya siasa mkoa ,ndugu Maimuna Abasi , kuwa wapiga kampeni za ADEN RAGE na AMINA KABOYONGA.
- Uongozi wa ccm mkoa kuanza kumuandaa mwenyekiti mpya wa halmashauri na kumkata diwani ambaye alikuwa mwenyekiti wa halmashauri ya Tabora, ambaye ndiye kashinda kiti cha udiwani.
- Uongozi wote CCM mkoa , kuwa wapiga kampeni wa baadhi ya madiwani baada ya kuwalazimisha kuwapa rushwa ya pesa kwa wanaume na rushwa ya ngono kwa viti maalum.
- Uongozi wa CCM mkoa kuwapitisha madiwani na wabunge ambao hawajashinda uchaguzi na ambao hawakubaliki kwa sababu wameshaongwa pesa
- Uongozi wa CCM mkoa, kumpitisha AMINA KABOYONGA ambaye amepata kura 1, kwa sababu ameshawanunua viongozi wa mkoa na kuwaacha washindi wote wa nafasi za awali ambao kimsingi ndio wanakubalika na wana CCM pamoja na kwa wana Tabora mjini wote
Tatizo kubwa ni uongozi mzima wa CCM mkoa ambao tayari wameshakula pesa za wagombea wao ambao wameshashindwa kwenye kura za maoni na hivyo kulazimisha wawe wagombea
Tunaamini malalamiko yetu yatakifikia chama cha mapinduzi na kuhakikisha wananusuru mgawanyiko unaoletwa na viongozi wa CCM mkoa kwa kulazimisha wagombea wao na kuacha kufuata machaguo ya wajumbe ambao ni wawakilishi wa wanachama walio wengi.
Tunaomba chama taifa, chukueni hatua madhubuti kwani uongozi wa CCM mkoa hawakitakii mema chama cha mapinduzi mkoani Tabora, tunaomba machaguo yetu kuanzia ngazi ya udiwani na wabunge yazingatiwe kwani ndio machaguo yetu na ndio yanayouzika na kukubalika kwa wananchi.
Ndimi,
NYASA MALEMBEKA
Mwakilishi wa wajumbe, Wilaya ya Tabora