Halmashauri iliyotoa lessen kwa Wakala wa Cement Ubungo

NI MTAZAMO TU

JF-Expert Member
Feb 20, 2014
1,203
998
Kilichowakuta wafanya biashara na wachuuzi wa CEMENT pale DEPOT ya Ubungo, kimenikumbusha enzi za UKOLONI kabisa.

Kisa chenyewe kiko hivi: Wajasili ya mali ,wachuuzi na wasakatonge kwa njia ya Uuzaji wa cement wamefika pale DEPOT kuanzia saa 9 alfajiri wakiwa na lengo la kuwahi namba ili wapate cement itakayo sababisha kupata tonge lake la kila siku.

Baada ya kuwahi namba ile huku MHINDI au MMILIKI wa ile DEPOT amefika saa 1:30 asubuhi watu hulazimika kuhesabu namba ili aweze kuuza cement nilipo Godown, na kukawa na Magari makubwa ya cement zaidi ya 10 mle Godown.

MHINDI au MMILIKI wa ile DEPOT akaagiza mgambo kuhesabu namba ya wataopata CEMENT wasiozidi watu 31 tu,nao kulingana na uhaba wa CEMENT kwa kipindi hiki inabidi watu hao 31 wapate si zaidi ya mifuko 100 tu kwa kila atakaye wahi kupata namba hiyo asubuhi.

Watu wakahesabiwa mpka namba 30 ilipofika namba 31 zikafungana kwa watu wawili. Ati hapo anatoka MHINDI kwa manyanyaso makubwa kufukuza watu wote watoke nje na kusema hataki tena kuuza CEMENT ile mpka kesho.

Zingatia watu wamewahi namba tangia saa 9 na 10 alfajiri kisha MHINDI/MMILIKI wa DEPOT anawafukuza kama MBWA KWENYE NCHI HURU KAMA TZ.

mpka jioni hii hakuna mfanyabiashara wa mchuuzi wa Cement aliyepata cement. kwa madai ati MHINDI/MMLIKI WA DEPOT KAKASIRIKA WATU NI WENGI WANAOTAKA CEMENT.

Swali kwa wenye mamlaka nini kimetokea
Cement kuwa dili kiasi hiki.

Na je Jeuli ya MHINDI huyu MMILIKI wa DEPOT YA CEMENT UBUNGO ANAIPATA
WAPI? KWENYE NCHI HII YA MAGU.

JE JAMBO KAMA HILI HALIWEZI KUWA CHANZO CHA UVUNJIFU WA AMAN NA KUIDHALILISHA SERIKALI?

NAANDIKA HII KITU KWA KUWA HASIRA ZA WANANCHI WALE WENYE MAHITAJI YA CEMENT ILIKUWA YA HATARI SANA .
 
Siku hizi hatusikii tena suala la sukari, kwanini same approach lisitumika kwenye cement? Tunavyo viwanda vya kutosha naamini
 
Kuna mambo kadhaa ambayo huwa yanatia hasira!!! Nadhani hili ni mojawapo.....

Kufeli kwa viongozi wa serikali katika eneo husika....
 
Mmeshindwa kutumia simu zenu vizuri.... Video yake ya hilo tukio na maelekezo ya tukio angeshikishwa adabu.... Kama hizo tambuu anavuta zinampa kiburi then anazingua...
 
Mmeshindwa kutumia simu zenu vizuri.... Video yake ya hilo tukio na maelekezo ya tukio angeshikishwa adabu.... Kama hizo tambuu anavuta zinampa kiburi then anazingua...
Hata mimi nimemshangaa Sana, Yani wangerecord, af video ikasambaa mitandaoni,tena ukizingatia nchi ipo kwenye kampeni, Wala asingemaliza hata siku mbili.
 
Hata mimi nimemshangaa Sana, Yani wangerecord, af video ikasambaa mitandaoni,tena ukizingatia nchi ipo kwenye kampeni, Wala asingemaliza hata siku mbili.
Tumewasoma ngoja tufanyie kazi ila hata jana na leo nimeambiwa ile issue ya unyanyasaji inaendelea lakini mbona vyombo husika haviendi fanyia kazi malalamiko ya wananchi au mpka mtu atolewe koo jaman ,wafike pale kama wateja wajiandae.
 
Tumewasoma ngoja tufanyie kazi ila hata jana na leo nimeambiwa ile issue ya unyanyasaji inaendelea lakini mbona vyombo husika haviendi fanyia kazi malalamiko ya wananchi au mpka mtu atolewe koo jaman ,wafike pale kama wateja wajiandae.
Huenda vyombo husika havijafikiwa na taarifa, au kama vinefikiwa na taarifa basi vimepuuzia (wanabebana).Ikiwa wanabebana, hakuna njia nyingine ya kupata msaada,isipokuwa shinikizo(pressure) kutoka kwa raia mbalimbali. Hilo litawezekana bila kuleta Shida kwa raia yeyote,Kama tu mtaamua kutumia mitandao,kifichua huo uhuni.
 
Kilichowakuta wafanya biashara na wachuuzi wa CEMENT pale DEPOT ya Ubungo, kimenikumbusha enzi za UKOLONI kabisa.

Kisa chenyewe kiko hivi: Wajasili ya mali ,wachuuzi na wasakatonge kwa njia ya Uuzaji wa cement wamefika pale DEPOT kuanzia saa 9 alfajiri wakiwa na lengo la kuwahi namba ili wapate cement itakayo sababisha kupata tonge lake la kila siku.

Baada ya kuwahi namba ile huku MHINDI au MMILIKI wa ile DEPOT amefika saa 1:30 asubuhi watu hulazimika kuhesabu namba ili aweze kuuza cement nilipo Godown, na kukawa na Magari makubwa ya cement zaidi ya 10 mle Godown.

MHINDI au MMILIKI wa ile DEPOT akaagiza mgambo kuhesabu namba ya wataopata CEMENT wasiozidi watu 31 tu,nao kulingana na uhaba wa CEMENT kwa kipindi hiki inabidi watu hao 31 wapate si zaidi ya mifuko 100 tu kwa kila atakaye wahi kupata namba hiyo asubuhi.

Watu wakahesabiwa mpka namba 30 ilipofika namba 31 zikafungana kwa watu wawili. Ati hapo anatoka MHINDI kwa manyanyaso makubwa kufukuza watu wote watoke nje na kusema hataki tena kuuza CEMENT ile mpka kesho.

Zingatia watu wamewahi namba tangia saa 9 na 10 alfajiri kisha MHINDI/MMILIKI wa DEPOT anawafukuza kama MBWA KWENYE NCHI HURU KAMA TZ.

mpka jioni hii hakuna mfanyabiashara wa mchuuzi wa Cement aliyepata cement. kwa madai ati MHINDI/MMLIKI WA DEPOT KAKASIRIKA WATU NI WENGI WANAOTAKA CEMENT.

Swali kwa wenye mamlaka nini kimetokea
Cement kuwa dili kiasi hiki.

Na je Jeuli ya MHINDI huyu MMILIKI wa DEPOT YA CEMENT UBUNGO ANAIPATA
WAPI? KWENYE NCHI HII YA MAGU.

JE JAMBO KAMA HILI HALIWEZI KUWA CHANZO CHA UVUNJIFU WA AMAN NA KUIDHALILISHA SERIKALI?

NAANDIKA HII KITU KWA KUWA HASIRA ZA WANANCHI WALE WENYE MAHITAJI YA CEMENT ILIKUWA YA HATARI SANA .
Hongereni watu wa DAR kwa ujenzi mnaoendelea nao mpaka mahitaji ya cement yanazidi uzalishaji/ugavi
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom