Halima Mdee: ⁦⁦Rais Magufuli hivi unajua ⁩biashara ya wabunge wa Ukonga na Monduli tu iligharimu taifa Shilingi 12,449,659,588.00 ?

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
⁦⁦@MagufuliJP hivi unajua ⁩ BIASHARA ya wabunge wa UKONGA na Monduli TU!!ililagharimu TAIFA shilingi 12,449,659,588.00 ? Halima James Mdee on Twitter
IMG_20190210_074925.jpg
Screenshot_20190210-074904.png
 
Hizo zingeenda ujenzi wa madarasa watoto wangeshindwa leo kuanza kidato cha kwanza kwa kukosa madarasa? Juha kwa kukosa akili anaweza kulazimika kutembea Dar to Moro kwa sababu 20,000/ yake ya nauli kaitumia kunywea pombe Bar ili kutaka walevi wamsifu.
Hii serikali inapenda sifa Kama za majuha
 
⁦⁦@Magufuli JP hivi unajua ⁩ BIASHARA ya wabunge wa UKONGA na Monduli TU!!ililagharimu TAIFA shilingi 12,449,659,588.00 ?
Duh! Hapa ndipo mtu unabaki unajiuliza maswali yasiyo na majibu. Idadi ya Wabunge wa CCM ndani ya Bunge la Ndugai na Tulia inawawezesha kupitisha sheria yoyote ile hata ikiwa ya hovyo namna gani. Sasa lengo la kutumia mihela yote hiyo kuongeza idadi ya Wabunge wa aina hiyo hiyo ni nini kama si kuhalalisha ufisadi na kuimarisha udikteta?

Hata kwa akili ya wastani tu, utagundua kuwa lengo ni kuhakikisha hakuna sauti zitakazohoji hili gari letu bovu linatupeleka wapi?Tumeshuhudia wale watundu wasiokubali kuuza nafsi zao kwa kipande cha fedha wakimiminiwa risasi zisizo idadi na wengine kubambikiziwa kesi zisizo na miguu wala kichwa. Je kwa staili hii, wananchi tutegemee nini?
 
Mwenzenu yupo ulaya na america anapigia chapuo demokrasia..ndio demokrasia ilivyo..kwani enzi za jk si mlimpiga chini zitto kabwe..mlidhani asingeenda mahakamani jimbo lake lingefutwa au usingefanyika tena uchaguzi?mbona hamkushtakiwa kwa kutaka kuingiza taifa kwenye hasara..
Ni nyie chadema ndio mliondoka mkagomea mchakato wa katiba mpya huku tayari zikiwa zimeidhinishwa na watu kulipwa billions of shillings, hali iliyopelekea mchakato kusimama...mbona nyie hamkushtakiwa au kama mliona hamtafikia muafaka kwa nini hamkumshauri jk asipitishe mlipokuwa mnaenda ikulu kunywa juisi.?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ina maana kila uchaguzi umetucost kama nchi 4 point kadhaa bilioni kugharamikia chaguzi hizo ambazo kimsingi hazikuwa na sababu iwapo tungekuwa na sheria ya mtu akihama ahame na ubunge wake au kutokuwa na uchaguzi wowote mpk muda wa uchaguzi ufike hata kama mbunge akihama. Nadhani tunahitajika kuliangalia hili kwa umakini kuepusha hasara hii.

Maana kwa idadi ya wabunge waliohama nadhani billion za kutosha zimepotea ambazo kama zingeelekezwa kwenye kununua vifaa vya hospital maisha ya wengi yangeokolewa, kama zingeenda kuboresha elimu wadogo zetu wangesoma Vizuri na kuongeza ufaulu, kama zingeenda kununua vifaa vya uokoaji maisha ya watz wenzetu yasingepotea Kwa excuse ya giza nk
 
Ina maana kila uchaguzi umetucost kama nchi 4 point kadhaa bilioni kugharamikia chaguzi hizo ambazo kimsingi hazikuwa na sababu iwapo tungekuwa na sheria ya mtu akihama ahame na ubunge wake au kutokuwa na uchaguzi wowote mpk muda wa uchaguzi ufike hata kama mbunge akihama. Nadhani tunahitajika kuliangalia hili kwa umakini kuepusha hasara hii.

Maana kwa idadi ya wabunge waliohama nadhani billion za kutosha zimepotea ambazo kama zingeelekezwa kwenye kununua vifaa vya hospital maisha ya wengi yangeokolewa, kama zingeenda kuboresha elimu wadogo zetu wangesoma Vizuri na kuongeza ufaulu, kama zingeenda kununua vifaa vya uokoaji maisha ya watz wenzetu yasingepotea Kwa excuse ya giza nk
Ndio gharama ya demokrasia ndugu..bahati imeback fire upande mmoja ndio maana vilio vingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom