Halima Mdee punguza ulaghai, unadanganyaje umma kuwa akaunti za benki za wabunge waliofungwa zilikuwa na kiwango chini ya Tsh. Milioni 1?

MAFILILI

JF-Expert Member
Apr 28, 2011
2,377
1,194
Jana katika tukio liliofanyika makao makuu ya CHADEMA, Mheshimiwa Halima Mdoe alikaririwa akitamka serikali imezifunga akaunti zote za benki za Mwenyekiti wa CHADEMA, Mheshimiwa Mbowe kwa vile walitarajiwa yeye akiwa na ukwasi mkubwa wa pesa ataweza kulipa faini kwa wote, hivyo muafaka ni kuzifunga akaunti zake pamoja na M-PESA.

Kimsingi sina tatizo na ukwasi wa Mheshimiwa Mbowe, lakini kizungumkuti ni pale Mheshimiwa Halima Mdee alipotutangazia umma ya kuwa yeye binafsi na waheshimiwa wengine Bulaya, Esther Matiko, Mnyika, Msingwa na Heche ambao wote ni wabunge kwenye akaunti zao zina pesa chini ya shilingi milioni moja.

Kwa kifupi serikali ilijua waheshimiwa husika watashindwa kulipa faini na hatimaye kuishia magerezani hatahivyo wananchi wamefanikisha kutoa michango ya kuwalipia wao.

ULAGHAI wa Mheshimiwa Halima Mdee unakuja pale anapoomba michango ya pesa kutoka kwa walala hoi huku waheshimiwa wabunge wakiwa na pato kubwa wao wenyewe hata akaunti zao za benki na raslimali wanazomiliki zina thamani zaidi ya milioni 200 kwa kila mmoja.

Waheshimiwa wabunge wa CHADEMA msitumie umbumbumbu wa wananchi kuwaibia kidogo walichonacho ili kulipia faini zenu, wakati waheshimiwa mna ukwasi mkubwa na pia chama chenu kinapata ruzuku kubwa kila mwezi.

Wananchi wa Tanzania tuachane na michango ya kilaghai badala yake tuwahoji kwanini wao wenye kiasi kikubwa cha pesa leo hii wanalazimisha sisi walalahoi kuwachangia faini kwa wao ambao wana kipato kikubwa kuliko walalahoi!!!
 
Kinakuum nn wananchi wakiungana nao wakati wa shida wamechanga wao kwa mapenzi yao baada ya account za wahusik kufungiwa ili wasote jela hakujawahi kuwa na faini kubwa kwa kesi kama hio tangu tupate Uhuru soma history, thus mashinji haraka wakamlipia either kwa cash au Mali kauli wanajua wao.Cha msingi cdm waanzishe bank zao ili kuepuka yote haya
 
Hiyo harambee aliitisha nan? Kama ni wenyewe hao basi ni ufisadi mkubwa..., else kama ni wananchi wenyewe walidhamiria sioni shida hapo.
 
Zile za Msigwa zilizolipwa na CCM kwa mgongo wa rais unaweza kutupatia control namba zake? Na Kama conrol number kwa ajili ya faini ya Msigwa imetolewa kwa CHADEMA na wakalipa, je, inaweza kutengezwa control number nyingine kwa bill ambayo haipo?

WATANZANIA SIO WAJINGA- mwenye TZS 100 alichanga na hata mwenye TZS 10M alichanga.

Hii ilikuwa marathon ambayo hamkupenda kushiri but at last mmejikuta mnakimbia nusu marathon-AHSANTENI KWA USHIRIKI WENU
 
Jana katika tukio liliofanyika makao makuu ya CHADEMA, Mheshimiwa Halima Mdoe alikaririwa akitamka serikali imezifunga akaunti zote za benki za Mwenyekiti wa CHADEMA, Mheshimiwa Mbowe kwa vile walitarajiwa yeye akiwa na ukwasi mkubwa wa pesa ataweza kulipa faini kwa wote, hivyo muafaka ni kuzifunga akaunti zake pamoja na M-PESA.

Kimsingi sina tatizo na ukwasi wa Mheshimiwa Mbowe, lakini kizungumkuti ni pale Mheshimiwa Halima Mdee alipotutangazia umma ya kuwa yeye binafsi na waheshimiwa wengine Bulaya, Esther Matiko, Mnyika, Msingwa na Heche ambao wote ni wabunge kwenye akaunti zao zina pesa chini ya shilingi milioni moja.

Kwa kifupi serikali ilijua waheshimiwa husika watashindwa kulipa faini na hatimaye kuishia magerezani hatahivyo wananchi wamefanikisha kutoa michango ya kuwalipia wao.

ULAGHAI wa Mheshimiwa Halima Mdee unakuja pale anapoomba michango ya pesa kutoka kwa walala hoi huku waheshimiwa wabunge wakiwa na pato kubwa wao wenyewe hata akaunti zao za benki na raslimali wanazomiliki zina thamani zaidi ya milioni 200 kwa kila mmoja.

Waheshimiwa wabunge wa CHADEMA msitumie umbumbumbu wa wananchi kuwaibia kidogo walichonacho ili kulipia faini zenu, wakati waheshimiwa mna ukwasi mkubwa na pia chama chenu kinapata ruzuku kubwa kila mwezi.

Wananchi wa Tanzania tuachane na michango ya kilaghai badala yake tuwahoji kwanini wao wenye kiasi kikubwa cha pesa leo hii wanalazimisha sisi walalahoi kuwachangia faini kwa wao ambao wana kipato kikubwa kuliko walalahoi!!!
Wewe ulipitia kwenye account zao na kuona kilichomo mpaka unasema anaulaghai umma?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom