Halima Mdee na wenzake 18 hawana nguvu yoyote ya kimaamuzi Bungeni, wanaburuzika tu

Nauchukia sana mfumo wetu. Unawafanya wananchi wasiihoji serikali yao, hasa kwenye majukwaa yalio rasmi kama bungeni .

Huu mfumo waTz watakuja kugundua wakiwa wamechelewa sana.

Nb mtuma thread ni johnthebaptist . Haeleweki
Huku vijijini wananchi wanahoji sana bwashee.

Tatizo ni huko juu yaani bungeni nk wanakosubiria teuzi!
 
Magufuli alitenda kama tuko katika mfumo wa chama kimoja, na huo ndio ukweli vyama vingine vyote ni matawi ya CCM!
Kwa hiyo katika hili, kama mada yako inavyoainisha, Magufuli asingeweza kusema lolote maana bunge hili lililojaa wana CCM ni zao lake.
 
Huku vijijini wananchi wanahoji sana bwashee.

Tatizo ni huko juu yaani bungeni nk wanakosubiria teuzi!
Vijijini wana maamuzi gani?!. Niliwahi kuwepo Geita, wakati mzee wa ukweli na uwazi ana binafsisha migodi. Maamuzi yalitoka juu vijiji vilishirikishwa ktk hatua za mwisho tena si kwa maamuzi, bali taarifa na ushauri wafanye nini
 
Unataka wafanye maamuzi wafurushwe bungeni? Wabunge wa COVID-19 ni tatizo kwa bunge
 
Huku vijijini wananchi wanahoji sana bwashee.

Tatizo ni huko juu yaani bungeni nk wanakosubiria teuzi!

Vijijini wanamuhoji nani mzee?

Kikatiba bunge ndio baraza kuu na rasmi lenye mamlaka ya kuweza kuihoji serikali, na kuisimamia...

Hao wa vijijini sauti zao zinaishia huko huko...
 
Vijijini wana maamuzi gani ?!. Niliwahi kuwepo Geita , wakati mzee wa ukweli na uwazi ana binafsisha migodi. Maamuzi yalitoka juu vijiji vilishirikishwa ktk hatua za mwisho tena si kwa maamuzi, bali taarifa na ushauri wafanye nini
Unazungumzia miaka 20 iliyopita?

Karibu leo!
 
Mbona mzee Mgaya unakuwa na ufinyu wa kufikiri.

Bunge la sasa ni matokeo ya Uchaguzi wa 2020 na ulisimamiwa na Magufuli mwenyewe.

Tunakumbuka walivyokatwa watu, hata kina Chenge na kura za mabegi.

Matokeo yakikuwa so smooth kiasi kwamba wapinzani hawakupenyeza hata sindano.

Kazi nzuri ya Magufuli!

Tukajikuta tuna bunge ka CCM watupu isipokuwa mbunge mmoja nafikiri Katavi huko.

Tatizo sasa kuna nafasi kikatiba lazima zishikiliwe na wapinzani.

Forgeries zikaanza kati ya Tume ya Uchaguzi na Ndugai.

Wakaingizwa kimpango mpango hao 19 wa CDM, kina Mdee.

Halima Mdee si wa upinzani, naye anajua hilo.

Yeye ni zao la Magufuli.

Sasa ataongea nini cha maana watu wamwelewe.

Sasa Magufuli angekemea vipi kazi yake?
Hivi Mzee Mgaya ndiye Yohana Mbatizaji au tumngojee mwingine?
 
Vijijini wanamuhoji nani mzee?

Kikatiba bunge ndio baraza kuu na rasmi lenye mamlaka ya kuweza kuihoji serikali, na kuisimamia...

Hao wa vijijini sauti zao zinaishia huko huko...
Vijijini wanazihoji serikali zao.

Serikali inasimamiwa na CCM siyo bunge.

Spika ni mjumbe wa kamati kuu ya CCM ambayo Rais ndio mwenyekiti wake.
 
Unaweza ukajiuliza uwepo wa wapinzani kiduchu bungeni una faida gani iwapo maamuzi yote muhimu yanafanywa na kamati kuu ya CCM?

Kiukweli Tanzania hatuna mfumo wa vyama vingi tuna kiini macho tu.

Na katika hili hayati Magufuli hakumung'unya maneno.

Maendeleo hayana vyama!
Kuna watu mkishalewa huwa mnajisahaulisha! Ina maana manunuzi ya wapinzani na uchafuzi wa 2020, hukuwepo Tanzani?!
 
Back
Top Bottom