Halima Mdee: Mimi pamoja na timu yangu (Wabunge 19) tutabaki kuwa WanaCHADEMA kindakindaki. Tutaenda kuyajenga ndani kwetu

Imeisha hiyo Mkuu. Hawawezi kuwa maarufu kuliko Chama kilichowajenga kisiasa. Walisahau kuwa kilichowavutia Wanachama na Wafuasi wengi wa Chadema kuchanga fedha na kuwanusuru na kifungo siyo kwa sababu ya umaarufu/umuhimu wao bali ni Chadema.

Hivyo hakuna atajaekuwa na umaarufu kuliko Chama. Kwa muda huu mfupi tu hata wiki moja bado umaarufu wao umeanza kupukutika.
Well said. Tena aombe radhi maana aliaminiwa sana Halima, Esther B na Esther M. Hao wengine hata hatuwajui. Ila hizo no 3 zitafakari sana. Na zote 3 zilishinda 2020.
 
Ukweli ulikuwa upi zaidi ya kushawishiwa na CCM na kuwarubuni. Hawa wadada wakajisahau namna walivyokuwa wanavurumishwa na hao hao ambao leo wamewakumbatia.
Mtesi wako wa jana hawezi leo kuwa mkombozi wako( Bagonza voice)!
 
Nakupongeza kwa jinsi ulivyojibu hoja mbalimbali na kuonesha unatambua kuwa ni nani wanaokupenda na nani ni maadui lakini wanasema kuwa ndio walinzi wako. Yaani wauaji na watesaji wako leo wanakuwa walinzi na marafiki zako.
Nami niko upande wako kwa hili Halima umetumia staha sana kujibu. Of course katika watu waliofia CHADEMA wewe unaongoza among top three! Upepo ulikupitia na kama umetubu, MBOWE na kamati Kuu, let us open a new chapter! Let by gone be by gone particularaly kwa watu hawa 19.
 
Wapo watakaokulaumu kwa vyovyote utakavyofanya bila ya kujali unalolifanya sasa ni jema au baya, kwa vile mwanzoni ulikosea, utaendelea kuwa mbaya tu siku zote.

Lakini wapo binadamu watakaokulaumu kwa kile ulichofanya wakati huo. Ukifanya vyema, bila ya kujali huko nyuma ulikosea, watakupongeza. Mimi nipo kwenye kundi hili.

Sikupongezi kwa sababu ulienda kuapa kinyume na maamuzi ya chama, sikupongezi kwa sababu umekuwa mbunge wala sikupongezi kwa sababu Ndugai amesema atakulinda. Bali nakupongeza kwa namna unavyokabiliana na tatizo lililopo mbele yako.

Wengi leo walitarajia umseme vibaya Mbowe na CHADEMA. Na hao ndio wanaodhani wamekuwa marafiki zako wapya.

Halima Mdee umeteseka sana kwa sababu ya kupigania haki na demokrasia Tanzania. Umeteseka sana kwa sababu tu umekuwa CHADEMA. Waliokuwa wanakusweka ndani, waliokuwa wanakutengenezea kesi, waliokuvunja mkono, waliokuwa wanakukejeli kwa maneno mengi ya dharau, leo wanajifanya ni marafiki zako.

Kumbuka kuwa mzazi wako hata kama anavaa lubega ni dhahiri ana upendo nawe zaidi kuliko jambazi mwenye jumba la ghorofa hata kama atakutoa kwa baba yako mwenye nyumba ya nyasi akawa anakulaza ghorofani kwenye chumba cha kifahari.

Nakupongeza kwa jinsi ulivyojibu hoja mbalimbali na kuonesha unatambua kuwa ni nani wanaokupenda na nani ni maadui lakini wanasema kuwa ndio walinzi wako. Yaani wauaji na watesaji wako leo wanakuwa walinzi na marafiki zako.

Nakupongeza kwa sababu hukuitusi CHADEMA, hukuitusi Kamati Kuu, hukumtusi Mbowe. Na hapa naipongeza Kamati kuu ya CHADEMA na Mh. Mbowe maana nao hata walipokuwa wakisoma maazimio ya Kamati kuu kuhusiana na Halima Mdee na wenzake, hawakuonesha kejeli wala chuki bali upendo wa dhahiri. Ni kama mzazi anayemchapa mwanae lakini anamchapa kwa sababu anataka abadilike na kuwa mtoto mwema na msikivu zaidi.

Mengine yatabakia katika maamizi ya Chama na ninyi wenyewe, lakini mpaka hapa umevuka kiunzi cha kwanza ambacho maadui wa CHADEMA na Mbowe walikuwa wakikisuburia kwa hamu.

Kwa njia uliyopita, kwa nguvu uliyoiweka, na imani uliyoitengeneza ndani ya CHADEMA, kwa Watanzania na Jamii ya kimataifa, usikubali kuipoteza imani hiyo kwa wepesi kiasi hicho.

Tunafahamu chama kitapitia njia ngumu, viongozi wa CHADEMA watapitia njia ya miiba lakini isiwe sababu ya kujijongesha kwa wadhalimu. Tengenezeni utaratibu, watu wenye mapenzi mema tuchangie kila mwezi ili kukitegemeza chama na watendaji wake. Hakika miongoni mwenu hakuna atakayekufa njaa wala kushindwa kutibiwa alimradi kuwepo utaratibu unaoeleweka.
Umeandika vizuri, lakini wenzako ndio walikuwa mstari wa mbele kumtukana hadi kuwaita COVID 19! Sasa swali, wanamuangaliaje leo? Watajibaraguza na kujifanya wanamsifia kama wewe?
 
Hao wakiruhusiwa kurudi wataanza kuleta vurugu ndani na kujijenga zaidi, huwezi kuwa na tamaa hadi unafikia hatua ya kufoji nyaraka ukisaidiwa na CCM halafu useme wewe ni Mwana Chadema, Fukuzia mbali hao.
Zipo adhabu nyingi ikiwemo kuwafanya wanachama wa kawaida.
 
Kwa hotuba ya Halima Mdee and Co. Ltd, I am convinced kuwa wameona wapi waliteleza na kweli wana damu ya CDM! let bygones be bygones forget past offences or causes of conflict and be reconciled.

Msiwape faida Nyang'au CCM.
 
Ndani ya CHADEMA hakuna wabunge wengine zaidi ya kina Halima Mdee na Matiko? Wao washindwe ubunge hao hao wajichague wapeleke majina yao.
 
Tatizo ni vita ya ubunge ndani ya chama, wakisamehewa kuna watu hawataridhika, Mbowe ana majina yake, Mnyika ya kwake, yaani ni full vurugu.
 
Shida ni kuwa ukiaminiwa itunze imani uliyopewa, kwani kujenga imani iliyopotea ina gharama kubwa mno. Hivyo leo mwataka kuaminiwa ilhali imani mliyoijenga miongoni mwa wafuasi wenu mmeivunja?
 
Ni jambo rahisi tu la kusema mchakato wa kuwapata hao wabunge 19 ndani ya chama ulifanyikaje na majina yao pale NEC yalipelekwa na nani.

Hakuna siri ya kusubiri rufaa ndio ueleze ikiwa mchakato wote ulifuata katiba ya Chadema.

Hadi sasa picha waliyonayo wananchi ni kwamba wabunge wa viti maalumu Chadema hupatikana kwa njia za panya yaani kwa utaratibu usio rasmi.

Maendeleo hayana vyama!
 
Wafanye haya kwanza.
1. Watangaze kukubaliana na maamuzi ya kamati kuu yaliyowavua uanachama.
2. Watangaze kuachana na ubunge wa viti maalum waliojivika kihuni huni.
3. Waseme nani alikuwa anawatumia.
4. Waombe radhi watanzania wote.
5. Wakae kimya kabisa.

Wakifanya hayo yote, mimi nitakuwa miongoni mwa watu watakaotafakari namna gani wasamehewe.

Nina uhakika kwa 99% hawawezi kufanya lolote katika hayo, maana hicho walichokifanya leo kwenye Press kulikuwa staged na CCM Lumumba toka Jumapili. Kama huamini subiri kitakachofuata.
 
Ni jambo rahisi tu la kusema mchakato wa kuwapata hao wabunge 19 ndani ya chama ulifanyikaje na majina yao pale NEC yalipelekwa na nani.

Hakuna siri ya kusubiri rufaa ndio ueleze ikiwa mchakato wote ulifuata katiba ya Chadema.

Hadi sasa picha waliyonayo wananchi ni kwamba wabunge wa viti maalumu Chadema hupatikana kwa njia za panya yaani kwa utaratibu usio rasmi.

Maendeleo hayana vyama!
Sema CCM haitaki maneno, hakuna cha watanzania hapa. Sema Jiwe, Ndugai, Mahela na Mugasha (may be)
 
49 Reactions
Reply
Back
Top Bottom