Halima Mdee: Mimi pamoja na timu yangu (Wabunge 19) tutabaki kuwa WanaCHADEMA kindakindaki. Tutaenda kuyajenga ndani kwetu

Kwa maelezo yake ni kwamba Katibu Mkuu na Mwenyekiti walikurupuka na kamati kuu ilitoa maamuzi Kwa mhemuko.
Ushauri wangu ni kuwa Mdee na wwnzako shikilieni msimamo huo huo msikubali kufukuzwa Kwa uonevu.
 
Ukiambiwa utoe uthibitisho wowote wa wao kushawishiwa na CCM huna. Hivyo usipende kuongea vitu vya kubuni. Hiyo ni mojawapo wa viashiria vya upungufu wa uelewa.

Swala hili halikutakiwa kuamuliwa haraka kama walivyoamua. Kulikuwa na kila sababu kwa watuhumiaa kupewa nafasi ya kujitetea ili kutoa uamuzi wa haki.

Kitendo cha watuhumiwa kutopewa nafasi ya kujitetea nacho ni kiashiria cha kuwa kuna ukweli unafichwa. Usiwaone wamama hao kuwa ndiyo wanaostahili kukosea ukajisahau kwamba hata viongizi wa chama nao wanaweza kukosea. Why hawakukubali kuwasikiliza kabla ya kutoa hukumu? Ni sheria gani inayoruhusu kumhukumu mtu pasipo kujitetea?

Iruhusu akili yako kufanya uchambuzi. Ni kwa nini watuhumiwa hao hawakuruhusiwa kujitetea?
Hakuna kitu chochote utanishauri mkuu kuhusu hawa wadada kushawishiwa na CCM na kama umechukia basi acheni kuwarubuni watu
 
Wewe umeligundua hilo vyema maana kwa hali ilivyo sasa wangesema wamekubali na hawakati rufaa basi ubunge ungekuwa shakani ila kwa kusema watakataa rufaa wanabuy time ndiyo maana wamegoma kuliongelea hilo

Hawa bado waendelee kuchunguzwa move zao na chama chao kuna hidden agenda au script ya awali imebadilishwa
Yes wasingekurupuka kama ni uamuzi wao binafsi basi wako smart sana.

Kama siyo uamuzi wao basi kuna move inasukwa CCM wako desperate kuhakikisha CHADEMA wapo bungeni ili kuhalalisha hoja zao kuwa nchi ina demokrasia, ili wapate misaada huko nje
 
Halima anazunguka mbuyu., Swali ni kwanini wameenda bungeni kuapa? Kwanini Nusrat hanje katolewa jela saa 1:30 usiku siku ya pili moja kwa moja bungeni kuapa??
Anazunguka mbuyu Kwa sababu hataki kuwa mbuzi wa kafara Kwa Mbowe, amempa chance mwenyekiti wake kabla ya kumwaga ugali..... Mbowe na Mdee ni top brand kwenye chama maswala ya kudhalilishana kwa shinikizo toka kwa watoto akina Mnyika sio pouwa, inshort Mbowe anajua what is going on.... Akishindwa kunetralize mambo, wataenda kuvuana mahakamani.....
 
Sasa ndio amezungumza kitu gani, hao ndio mwal nyerere aliwaita " Mercenary " yaani "wanasiasa wenye tabia za kimalayamalaya tu" wako tayaari kuuza nchi ili wapate pesa, yaan wao ni pesa tu hakuna kingine

Hawa wako kama Tundu Lissu.. pesa kidogo wanauza utu.😅
 
Mimi ni mwanachi na mfuasi wa CHADEMA! Au unataka uninyang'anye haki yangu ya kutoa maoni?
Na yeye ni Mbunge na ana kinga yake! Je unalijua hilo? Toa maoni yako jinsi utakavyo, ila zingatia vigezo vyote vya utu na heshima
 
"Nusrat [Hanje] aligombea na alikuwa kwenye mchakato halali. Nusrati ametokeaje [gerezani], katolewa na nani, hilo suala mnatakiwa muende kwenye ofisi ya DPP mumuulize ama mkurugenzi wa magereza ama mahakamani. Mimi sihusiki na habari za barabarani."- Halima Mdee
 
Kwa vyovyote vile chama kingeandika barua ya kutowatambua Kyle bungeni kwa kuwavua uanachama kisha kikateua wengine wao wangekuwa looser at the same time aliyewashawishi nae angekuwa looser.
Sielewi una maana gani hapa: chama kiteuwe wengine? Kwani CHADEMA wamekwishakubali ushindi wa CCM kwenye uchafuzi uliopita?
CHADEMA wanachotakiwa kufanya ni kuandika barua bungeni inayoonyesha hao sio wanachama wa chama hicho tena baada ya kuwafukuza ndani ya chama.
 
Halima anakuja na maneno laini laini Bashiru alikukaribisheni kwa nguvu zote lete majibu kwanini mlienda bungeni kuapa? Au Katiba ya CHADEMA inaruhusi mjipeleke wenye na kujichagua wewe muape?
 
Mpaka Hapa Kwa namna alivyoongea Mdee, naiona busara yake na anastahili kuwa MK Chama ama KM Chama, kawazidi wote waliopo kwenye nafasi hiyo,

Wliopo ni wakurupukaji na si waonyesha njia, Uongozi si mihemko, Uongozi ni Hekima na kiongozi hupimwa ktk kutatua Changamoto na si vinginevyo
Yes atakuwa Mwenyekiti wa UWT maana tayari tumeshamfukuza CHADEMA kwa utovu wa nidhamu.
 
Bwashee mtaendelea kuweweseka tu,khabar yake imeshakwisha
Kuna watu hapa Jf waliamini na bado wanaamini Halima Mdee anaweza kwenda kinyume na Mbowe.

Siyo rahisi.

Halima Mdee hawezi kuiacha Chadema hata akikumbatiwa na nani nje ya Chadema.

Mungu wa mbinguni awabariki.

Maendeleo hayana vyama!
 
Back
Top Bottom