Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Una maana gani unaposema amemsambaratisha Magufuli?
mkuu , nimefurahishwa sana na hilo jina jipya la MH HALIMA MDEE , TANZANIAN IRON LADY !
Kuamini kumtoa Magufuli Chato ni uendawazimu!
Binafsi nilikuwepo na nipo Chato muda huu. Watu kutoka Bwina, Nyabilezi, Rubambangwe, Itale, Kasagara, Ginnery na maeneo mengi walifika kwenye mkutano huo. Watu walirudisha kadi za CCM hadharani. Kiukweli mvuto wa Magufuli na CCM hapa Chato ni mdogo sana kiasi kwamba ukiitishwa uchaguzi mnaweza msiamini kuwa Magufuli anaweza kupata 30% ukilinganisha na Dr. Lukanima (63%). Sisi ndio wazawa wa Chato na huo ndio ukweli.
bado Bavicha hawajaingia mzigoni kudadadeki magamba mtaisoma..
Mwenyekiti wa BAWACHA Taifa Halima Mdee jana alitikisa Jimboni Chato kwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara kuwahi kuhutubiwa jimboni hapo miaka ya karibuni.
Awali Mdee alilakiwa na umati mkubwa wa watu wakiwa na msururu mrefu wa magari,pikipiki,baiskeli huku akina mama wakiwa kandokando ya barabara wakipunga matawi ya miti.
Ujumbe mkubwa wa Halima Mdee kwa wanaChato ni kuikataa Katiba Haramu ya CCM na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu.
Halima Mdee maarufu kama Tanzanian Iron Lady alipokea kadi 200 za watu walioamua kujitoa CCM na kujiunga Chadema.Huku mamia ya wananchi wengine ambao hawakuwa na chama wakijiunga pia Chadema.
Ikumbukwe jimbo la Chato linaongozwa na mbunge wa CCM John Pombe Magufuli ambaye ni waziri wa Ujenzi.
Ni simulizi hapa Chato kuanzia jana mpaka asubuhi hii kumzungumzia Halima Mdee na Chadema!
Kati ya hao walioshiriki mkutano ni wangapi wapo tayari kupiga kura? Bado na sisitiza kinachowafanya watu wajae kwenye mikutano hii ni ukosefu wa ajira. Watu wangekuwa na kazi usingewaona wakijaa kwenye viwanja hivi kusikiliza watu waliopo kwenye kazi zao.
Kwa Chato siwezi kushangaa kwani jamaa hakubaliki na hana ushawishi tena kutokana na mabavu yake ktk kila kitu.
Tusidanganyane mdee hawed mots makufuli abadan