Hali yetu ya maisha sisi mashabiki wa Yanga na Man united

coyyote

Member
Aug 12, 2018
53
87
Sisi mashabiki wa izi timu mbili maisha yamekuwa ya ovyoovyo sana kwa sasa, sijui team zetu zinakosea wapi.

wengine mpaka tunatamani kuomba ruhusa kazini baada ya matokeo mabovu ya tim zetu kwa kuhofia utani na majungu uko makazini

Kwa upande wa man U najua walikosea kwenye usajili, walirekebisha eneo la ulinzi lakini wakaacha wachezaji muhimu wa kati na mbele kuondoka bila kuleta mbadala i.e lukaku na Herrera

Kwa upande wa Yanga ndio bado nang'amua ni nini tatizo mpaka kuanza msimu vibaya ivi

Wadau wanaopitia hali kama yangu ebu mwagika apa, Tim zetu zinakosea wapi
 
Msipokubali kufungwa mtakuwa sio
wanamichezo.
Mbona ndio timu pekee ambayo mpo kimataifa mkiiwakilisha nchi.
 
Sisi mashabiki wa izi timu mbili maisha yamekuwa ya ovyoovyo sana kwa sasa, sijui team zetu zinakosea wapi.

wengine mpaka tunatamani kuomba ruhusa kazini baada ya matokeo mabovu ya tim zetu kwa kuhofia utani na majungu uko makazini

Kwa upande wa man U najua walikosea kwenye usajili, walirekebisha eneo la ulinzi lakini wakaacha wachezaji muhimu wa kati na mbele kuondoka bila kuleta mbadala i.e lukaku na Herrera

Kwa upande wa Yanga ndio bado nang'amua ni nini tatizo mpaka kuanza msimu vibaya ivi

Wadau wanaopitia hali kama yangu ebu mwagika apa, Tim zetu zinakosea wapi
Ndugu vumilia hiyo ni kawaida kwenye soka
Sisi arsenal tulishazoea hiyo

Ila tukija nyumbani simba inatubeba
Sasa rejea kipindi simba imeyumba na arsenal kama ulivyokuwa ukiifahamu misimu iliyopita basi inabidi ukaze roho hiyo
 
Kwanza ulianzaje kuishabikia yanga (chura na man u hii combination unaona iko sawa?? Ndio maana team zinapata mikosi (Natania) , angalia wenzako tuko Wekundu wa Msimbazi + Vijoo wa Jiji (London) tunakalala tunaamka shwari japo pressure huwa zinapanda sometimes Mko katika kipindi cha mpito, nafikiri kwa Man U mpaka Mzee Fagy atangulie mbele za haki mzimu wake upite, Yanga mtoeni huyo Mkongomani tu.
 
Eti Olesendeka anategemea Martial na Rashford pamoja na mjusi Lindgard
Sisi mashabiki wa izi timu mbili maisha yamekuwa ya ovyoovyo sana kwa sasa, sijui team zetu zinakosea wapi.

wengine mpaka tunatamani kuomba ruhusa kazini baada ya matokeo mabovu ya tim zetu kwa kuhofia utani na majungu uko makazini

Kwa upande wa man U najua walikosea kwenye usajili, walirekebisha eneo la ulinzi lakini wakaacha wachezaji muhimu wa kati na mbele kuondoka bila kuleta mbadala i.e lukaku na Herrera

Kwa upande wa Yanga ndio bado nang'amua ni nini tatizo mpaka kuanza msimu vibaya ivi

Wadau wanaopitia hali kama yangu ebu mwagika apa, Tim zetu zinakosea wapi
 
Tatizo la Yanga kocha Zahera ana kazi nyingi sana kwa wakati mmoja, uenyekiti, ukatibu, udaktari wa timu, usemaji wa timu, uhamasishaji wa timu na zilizo kuu ukocha na uwakala wa wachezaji wa kikongo. Kipindi kilichopita ilikuwa sawa kufanya kazi zote hizo kwa wakati mmoja kwa sababu Yanga ni kama ilikuwa haina viongozi kabisa. Lakini sasa Yanga ipo vizuri Mwenyekiti yupo tena msomi wa kiwango cha juu kabisa, Katibu yupo, daktari wa timu yupo, msemaji wa timu yupo, mhamasishaji wa timu yupo na wa kujitolea Jimmy Kindoki yupo.

Ni wakati muafaka sasa kwa viongozi wamfunge gavana ili yeye Zahera abakie na jukumu moja tu la kufundisha timu hayo mengine awaachie viongozi na wenye taaluma zao. Na sio kila akiona "mic" tu basi mdomo unamuwasha anaanza kubwabwaja. Ule uhuru wa kuongelea kila kitu cha Yanga yeye kauona kama haki yake mpaka anasahau majukumu yake ya msingi ya kuaandaa timu wakati hakujua kuwa wakati ule timu ilikuwa chini ya kamati tu mpito ya akina Nyika. Ajikite kwenye kuandaa timu mengine awaachie wakina Nugaz wenye kazi zao yeye Zahera ahusike kwenye press zile zinohitajika kocha aende basi. Kwa hili najua lipo ndani ya uwezo wa Dk. Msola na Mwakalebela
 
Pale manyu mpaka kibaraka wa Glazers ed Woodward aondoke na aje boss anayejua mpira labda ndo patatulia
 
Back
Top Bottom