Hali yangu kiafya si nzuri. Maombi yenu Wakuu

Puna

JF-Expert Member
Oct 9, 2013
2,334
3,781
Tatizo lilianzia Jumamosi kichwa kilianza kuuma gafla. Jumapili nikawahi Zahanati wakanipa Mseto nikaanza kupiga siku hiyo hiyo,jumanne nikamaliza. Jumatano nikawa nashindwa kugeuka miguu na mgogo pmoja na shingo hatari Sana, ukiniita nageuka Kama robot.

Nikaona isiwe shida nikaenda Zahanati Dr ananiambia malaria inaisha. Alhamisi nikaona na hema kama mtu mwenye Asthma nikaenda Tena wakaniambia ni UTI nikapewa Cipro wakuu Ijumaa hali si hali nakumbuka nilichangia thread moja humu ya mtu kuuguliwa na mkewe the same case. Nikajifanya asubuhi kupasha kifua kilifunguka kidogo.

Jioni hali si hali nakumbuka Jioni mkuu BAK Aliniambia nikafanye vipimo. Sasa Leo nikaingia Hosp kufanyiwa checkup siumwi chochote. Hapa Sasa napumua kwa shida nakohoa kikohozi kikavu kichwa kinapasua si mchezo nimepoteza hamu ya kula. Kibaya zaidi Shemeji yenu Yuko migombani huko. Nimetoka Hosp ikabidi nijisalimishe Kanisani kwa Katunzi. Mara ya mwisho kuingia church ilikuwa 2010.

Hakika maisha matamu na kifo kinatisha nimejikuta Niko Mtoni mtongani.

Wakuu maombi tafadhali.
 
Tengeneza mchamganyiko wa malimao,tangawizi,vitunguu saumu,vitunguu maji,umimine maji kiasi chap zi blend.
Wife akija ataosha hiyo blenda.Gonga glasi mapema iwezekanavyo.
Nimescreen short hii you Asante.
 
Loving God.

Please heal this broken heart. Fill him with the peace and joy I know can only come from You during this hard time. Walk closely beside him during his journey to healing and recovery that I know is possible through Your power alone. In Jesus' Name

Amen....🙏
 
Back
Top Bottom