Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,769
- 10,649
Kuna uwezekano mkubwa pande mbalimbali za nchi zimekuwa zikiugulia maumivu ya kukosa umeme. Mimi natulia maeneo ya Gongolamboto. Hali ya umeme ni mbaya mno. Umeme unakatika hovyo wakati mwingine kwa masaa 12. Biashara nyingi zimeathirika kufuatia kukatika umeme karibu kila siku. Mbaya zaidi kwa kipindi cha wiki mbili sasa, kila ifikapo saa 2 usiku, kama umeme upo, TANESCO hubonyeza 'reset button' ambapo umeme hukatika na kuwaka hovyo kabla haujatoweka kabisa au kuwaka tena.
wakati waziri Muhongo anachukua madaraka alijigamba kwamba mgawo ulikuwa wa kutengenezwa na kuapa kuwa hautakuwepo tena. Au ndio tuseme kuwa na yeye ameingia kwenye pay roll ya wenye nchi?
wakati waziri Muhongo anachukua madaraka alijigamba kwamba mgawo ulikuwa wa kutengenezwa na kuapa kuwa hautakuwepo tena. Au ndio tuseme kuwa na yeye ameingia kwenye pay roll ya wenye nchi?