Hali ya Taifa letu: Mwezi mmoja pasipo Hayati Dkt. John Magufuli

Mwanza kuna mgao wa Umeme wa hatari, yaani imefika hatua ukienda kwa kinyozi inabidi uende na kofia maana haifahamiki TANESCO watakata Umeme muda gani!
Hapa ninapoandika Umeme umekatika tangu saa moja asubuhi!
Kabla ya kifo cha Mzee mbona Ujinga huu ulikuwa hakuna?
Huku nilipo tangu mama aingie umeme umetulia kabsa yaaani leo imepiga mvua kubwa ila umeme umekatka nusu saa tu na sio kawaida ingekuwa enzi za mwendazake ni siku mbili ndio ungerudi
 
Mgao wa umeme ulianza tangu February na Tanesco wakawa wanasema Kunguru wanaharibu miondombinu.
Mwanza kuna mgao wa Umeme wa hatari, yaani imefika hatua ukienda kwa kinyozi inabidi uende na kofia maana haifahamiki TANESCO watakata Umeme muda gani!
Hapa ninapoandika Umeme umekatika tangu saa moja asubuhi!
Kabla ya kifo cha Mzee mbona Ujinga huu ulikuwa hakuna?
 
Wananchi, Watanzania,bala visiwani wanafuraha. Chuki aliyoipandikiza merehemu, chuki kati ya wanasiasa wa chama tawala na wapinzani inapungua sana. Polisi wameanza kujirekebisha kwa maana kulinda raia na mali zao ndiyo jukumu lao marehemu iliwapa jukumu lingine la kuilinda CCM.

Sera za uchumi zimeonyesha dalili ya kubadilika, mfano maduka ya kubadilishia fedha mazungumzo yanaendelea yarudishiwe leseni zao, Bank kuu mazungumzo yanaendelea ianze kukopesha bank zingine ndogo( NMB,CRDB,EXISM Bank) ili wateja wakope hele ziingie mitaani.

Serikali imeanza kukodi kumbi za mahotelini. mfano hapa ni MORENA hotel Dodoma. hii inasaidia wenye mahoteli kulipa kodi stahiki, sasa marehemu akawa anasema wizara zitumie kumbi zao , kisha wenye kumbi za mahotelini wakawa wanakosa kazi kisha wanadaiwa kodi kubwa mwisho wake ni kama NGURUDOTO.

1618729818940.png
 
Kiuhalisia muda bado sana kuweza kusema nini kinapungua au kukimiss, ngoja kidogo hapo mbele as mwaka hivi.
 
Rushua imeanza kuchipua kwa watendaji wa serikali.

Juzi nilikuwa naingia Bandarini kuelekea Zenji mimina Mzee wangu ambaye ni mtu mzima anayetumia wheel chair., Kuomba kuingia getini,askarikadai chochote kinywa kipana.,tukatazamana machoni, kiukweli tulishaga sahau ujinga kama huu.
 
Kesi za uhujumu uchumi zimepungua kwa kasi, bila shaka yeye ndo alikuwa mhujumu uchumi.

Wale waliohukumiwa uhujumu uchumi wamenza kupata haki yao.

Hajatekwa mtu mpaka sasa, vyama vya siasa vimeanza kutekeleza majukumu yao kidogo kidogo.

Tumeokoa mabilion ya Tshs na mengine tunataraji kuyaokoa ambayo meko alihusika na wizi wake.

Vyombo vya habari vimeanza kuwa huru, watu wameanza kuenjoy freedom of expression.

Furaha imezidi miongoni mwa watanzania, (watu wameanza kunenepa).

Tanzania imerudi katika misingi yake
 
Back
Top Bottom