GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Jana (10.06.2013) kwenye kipindi cha BBC Swahili jioni , wageni mbali mbali waishio Afrika Kusini wameonyesha hali ya wasiwasi ya mustakabali wa maisha yao huko endapo Mzee Nelson Mandela atafariki. Kwani Mzee Mandela ndiye aliye rekebisha sera za Afrika kusini na kuwaruhusu wageni waishi nchini humu kama nchi yao na kuwaasa wenyeji kutowabughudhi wageni. Sera hii ilileta sintofahamu kwa wenyeji na kumuona Mzee Madiba kama msaliti wa nchi yake kwa kuwakaribisha wageni kama nchi yao. Tumuombee mzee wetu apone kwa haraka na Mungu ampe nguvu , amen.