Hali ya Mheshimiwa Mwakanjuki inaendeleaje?

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
wakuu ni muda mrefu tokea tupate habari kuwa mheshimiwa ADam Mwakanjuki ambaye ni waziri wa mawasiliano na UChukuzi ktk serikali ya Zanzibar na miongoni mwa wanasiasa mashuhuri nchini kwetu kupata maradhi ya baridi hatujapata kujua au kuelezwa hali yake inaendeleaje?


nnaomba wale wenye kujua hali yake inaendeleaje na yuko wapi kwa sasa watuhabarishe

maana katika kipindi hiki kigumu inayopita zanzibar tungesikia sauti yake na kwa hakika mchango wake unahitajika sana
 
kwa habari za uhakika kutoka kwa mtoto wake ni kwamba mzee Mwakanjuki amepooza na hataweza kutembea tena,,,,alikua South Africa kwa matibabu lakini alirejeshwa katikati ya March na yuko Dar nyumbani kwake masaki ameshahama Upanga na anaendelea kupata matibabu,,,

Pia mwanae alining'ata sikio kwamba ""SIASA MCHEZO MCHAFU""

Hayo ndo nafahamu kwa sasa kuhusiana na comrade huyo wa siasa za bongo na mapinduzi ya zenji,,,
 
amekun'gata sikio siasa mchezo mchafu una maana gani?

halafu huyu hadi sasa ni waziri kule zanzibar ikiwa hataweza kutembea na kufanya kazi tena kama ulivyoeleza sheria inasemaje kuhusu kuendelea kubakia kuwa waziri?
 
amekun'gata sikio siasa mchezo mchafu una maana gani?

halafu huyu hadi sasa ni waziri kule zanzibar ikiwa hataweza kutembea na kufanya kazi tena kama ulivyoeleza sheria inasemaje kuhusu kuendelea kubakia kuwa waziri?

kuhusu kung'atwa sikio umeshaelewa alichomaanisha so mengine kuyaelezea inakua ngum ila kama vipi naomba kufuta kauli yangu

kuhusu sheria hata mie sielewi inakuaje hapo,,but umuhim wa Mwakanjuki ndani ya CCM unafahamika kwa wafuatilianji wote wa siasa za bongo so hawawezi kumtoa eti kwa vile anaugua inabidi tuwe wapole ndio siasa zetu hizo kaka,,,Otherwise mwakanjuki get well soon bro...
 
Ameshadokeza kuwa siasa mchezo mchafu, hata akipona hivi anaweza kurejea kwenye mchezo huo?
 
maana na nyepesi nyepesi komandoo na yeye kapoteza macho haoni kabisa ? au ndio mambo ya siasa?

nnaomba mkuu kama huwezi kuyaweka hadharani uniwekee kwenye pm ndio kupeana habari kaka
 
siasa hawezi kuacha kutokana na umuhim wake....ukitaka kujua siri ya mapinduzi+muungano wa zanzibar....Mwakanjuki ndie pekee aliebaki anaefaham undani wake...yeye ni mtu wa Mbeya nadhani hata jina lake linajionyesha sema siasa mambo mengi na nisingependa kwenda huko....

Mtu wa pwani ninachokimaanisha ushakifaham lakini najua hata wewe unafaham siwezi kwenda deep
 
mwa.jpg

naam mkuu mwakanjuki na mzee lowassa alipokuwa akimjulia hali hospitalini
 
Natumai anaendelea vizuri na karibu atarudi Zenj...
 
Last edited:
Back
Top Bottom