Hali tete kwa CHADEMA kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015

Ritz

JF-Expert Member
Jan 1, 2011
46,555
31,876
Wanabodi.

Kuingia kwa Abdulrahaman Kinana na Philip Mangula katika timu ya uongozi wa CCM, kunasafisha kabisa matumaini ya Chadema kuingia Ikulu ifikapo mwaka 2015. Ni jambo lililo wazi Kinana, heshima aliyojijengea mkoani Arusha na mikoa mingine ya kaskazini, kila Mtanzania mkweli anajua.

Heshima aliyojijengea Mangula Iringa na mikoa mingine ya Nyanda za Juu Kusini, kila Mtanzania mkweli anajua. Kutokana na sababu hizo kiongozi au mwanasiasa yeyote makini ndani ya Chadema, atakubaliana na ukweli kwamba chama hicho sasa hakitakuwa na chake tena kanda ya kaskazini na nyanda za juu kusini mwaka 2015.

Chadema kama ina viongozi wanaona mbali wanaweza wakaanza kuitumia ruzuku wanaoipata sasa kwa umakini wa hali ya juu, ikiwa ni pamoja na ruzuku hiyo kutumika kujenga vitega uchumi vya baadae vya chama hicho baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, cha hicho hakitapata tena ruzuku. Hakuna kipindi kigumu ambacho Chadema itapitia kama kipindi hicho kwenye historia ya chama hicho.

Pamoja na kwamba hakuna kiongozi yeyote ndani ya Chadema anayeweza kwenda kinyume na amri ya Mbowe kuhusu matumizi ya ruzuku ya chama hicho, lakini mwelekeo wa sasa utakuwa tofauti, Chadema sasa wana hiyari ama kuacha hazina ya ruzuku yao kidogo kutoka serikalini inayopatikana sasa iendelee kuboresha maisha ya viongozi na familia zao, au waseme hapana, sasa tuanze kujenga ofisi za chama chetu kila mkoa na wilaya ili pindi ruzuku hiyo itakapopungua baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 walau chama kibakiwe na ofisi.

Mbowe na Dr Slaa sidhani kama watakubali wazo hilo lenye maana moja ya kupunguza maisha yao kifahari waliyonayo sasa hawatakubali kuona wanaachana na mipango yao ya kujiwekea hazina ya baadaye ya maisha ndani ya chama ambayo haitakuwa na ruzuku.
 
Vipi Kinana ile meno yetu ya tembo karudisha. Kinana tunamjua vizuri akiwa mbunge alijimilikisha mashine za kuvulia za Mt Meru Hospital kwa ajili ya Dry Cleaner yake. Kwa hiyo tunamjua vizuri na bado tutakupa data zake subiri wakati
 
Maji yakimwagika hayazoleki, CCM hata aje nani wananchi hawapo nao tena wote wameshaamia Chadema wanataka mabadiliko na serikali tofauti,so haijalishi nani wamemuweka ni kazi bure tu....

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Ni jambo lililo wazi Kinana, heshima aliyojijengea mkoani Arusha na mikoa mingine ya kaskazini, kila Mtanzania mkweli anajua.
Heshima gani alijijengea ni hii ya uvunaji wa pembe za ndovu!CCM kweli hatuwawezi kwa sababu sasa mmeamua ku 'outsource' majeshi kutoka Somalia,hakika mnatisha!
 
Ritz:Tukiachana na propaganda za kisiasa pamoja na yale mambo ya kupeana moyo ama ushabiki kwenye masuala ya kisiasa,katika hili ccm wanaweza kidogo wakawa wamejipatia Credit na JK anaweza akawa amechanga karata zake vizuri kwa sababu kama ni vuijembe kapigwa sana hadi na wanaccm wenyewe mara ameamua kuwaachia wapinzani nchi?!,mara CCM imemshinda lakini kumbe Usiomuona Kobe ameinama,anatunga sheria.

Ni ukweli usiopingika kwamba watendaji hawa wapya wa ccm wametoa mstuko kwa vyama vya upinzani na hasa cdm ambayo ilikuwa imeshakaa kwenye line kwa ajili ya kuhakikisha kwamba inachomoka mita 100 na kuindoa ccm madarakani,hakuna ubishi kwamba kwa hili lililofanyika ni lazima wakae chini wajipange upya na kuangalia waingilie mguu gani katika kama kweli wanan nia ya dhati katika kuhakikisha kwamba wanaichukua nchi.

Hata hivyo kwa ccm sio tu kwa sababu kinana na Mangula wapo basi wajisahahu waache kufanya kazi ka sababu majina ya watu hao ni makubwa,hakuna kitu kama hicho,ni lazima,ni lazima watumie nafasi hiyo na majembe hayo katiika kuhakikisha kwamba wanakisafisha chama kama ambavyo alisema mangula siku ile Dar!!!!!!!!!.

Ni ukweli usiopingika kwamba ndani ya ccm bado kuna mzizi ya uharibifu inayotakiwa kung'olewa ili imani ya wananchi na wanachama wake iliyokuwa imetoweka irejee.

Otherwise ni azi kwamba hali si shwari saana kama ilivyokuwa hapo awali kwa cdm kwa vyovyiote ni lazima wastac,wakae warudi nyuma wajipange.
 
Maji yakimwagika hayazoleki, CCM hata aje nani wananchi hawapo nao tena wote wameshaamia Chadema wanataka mabadiliko na serikali tofauti,so haijalishi nani wamemuweka ni kazi bure tu....

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

Unaposema wananchi unamaanisha nini hapa,kwa uhakika gani ulio nao ambao unao mkononi,kwa Bicons zipi?!,Tangible ipo kweli???!!
 
Wanabodi.

Kuingia kwa Abdulrahaman Kinana na Philip Mangula katika timu ya uongozi wa CCM, kunasafisha kabisa matumaini ya Chadema kuingia Ikulu ifikapo mwaka 2015. Ni jambo lililo wazi Kinana, heshima aliyojijengea mkoani Arusha na mikoa mingine ya kaskazini, kila Mtanzania mkweli anajua.

Heshima aliyojijengea Mangula Iringa na mikoa mingine ya Nyanda za Juu Kusini, kila Mtanzania mkweli anajua. Kutokana na sababu hizo kiongozi au mwanasiasa yeyote makini ndani ya Chadema, atakubaliana na ukweli kwamba chama hicho sasa hakitakuwa na chake tena kanda ya kaskazini na nyanda za juu kusini mwaka 2015.

Chadema kama ina viongozi wanaona mbali wanaweza wakaanza kuitumia ruzuku wanaoipata sasa kwa umakini wa hali ya juu, ikiwa ni pamoja na ruzuku hiyo kutumika kujenga vitega uchumi vya baadae vya chama hicho baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, cha hicho hakitapata tena ruzuku. Hakuna kipindi kigumu ambacho Chadema itapitia kama kipindi hicho kwenye historia ya chama hicho.

Pamoja na kwamba hakuna kiongozi yeyote ndani ya Chadema anayeweza kwenda kinyume na amri ya Mbowe kuhusu matumizi ya ruzuku ya chama hicho, lakini mwelekeo wa sasa utakuwa tofauti, Chadema sasa wana hiyari ama kuacha hazina ya ruzuku yao kidogo kutoka serikalini inayopatikana sasa iendelee kuboresha maisha ya viongozi na familia zao, au waseme hapana, sasa tuanze kujenga ofisi za chama chetu kila mkoa na wilaya ili pindi ruzuku hiyo itakapopungua baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 walau chama kibakiwe na ofisi.

Mbowe na Dr Slaa sidhani kama watakubali wazo hilo lenye maana moja ya kupunguza maisha yao kifahari waliyonayo sasa hawatakubali kuona wanaachana na mipango yao ya kujiwekea hazina ya baadaye ya maisha ndani ya chama ambayo haitakuwa na ruzuku.



Nawashauri CDM waje na List ya Wauza Pembe za Nduvu na wasafirishaji wa Pembe za Nduvu.

pili list ya Waandishi wa Vimemo vya Epa
 
Vipi utata wa uraia wa Kinana mmeshatatua?

Mi nadhani ungejikita kwenye hoja zaidi ungeliwasaidia san watu wengine kuelewa kwa sababu hii ni sehemu ya kujifunzia zaidi ukiachilia yale ya kule darasani ambapo wengi wamepita,lakini kama utaendekeza ajenda za kishabiki na kejeli bado hatuwezi kuleta ukombozi fungukza zaidi ili watu waelewe na mwisho wa siku wafunguke.
 
Nawashauri CDM waje na List ya Wauza Pembe za Nduvu na wasafirishaji wa Pembe za Nduvu.

pili list ya Waandishi wa Vimemo vya Epa

Ili isaidie nini wakati hata baadhi ya wanacdm wamo humo!!au unatafuta kuabishana tu na ndugu zako,twende kwenye hoja ya msingi ili wasioelewa waelewe zaidi na kufanya maamuzi.
 
Arusha kinana namjua peke yangu..heshima ipi ya Huyu Ja.ngili? Madhara ya alcohol zako za tandale kwa mtogole.
 
Arusha kinana namjua peke yangu..heshima ipi ya Huyu Ja.ngili? Madhara ya alcohol zako za tandale kwa mtogole.

Kumjua wewe tu inatosha mimi nilikuwa nahani hafahamiki kabisa,kwa sababu kama wewe unamfahmu lazima watu wako wa karibu nao watkuwa wanamjua,na hao watu wako wa karibu nao watu wao wa karibu watakuwa wanamjua kwa sababu hii ni cheni ambayo inasambaa.Ahante Mkuu.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom