Uchaguzi 2020 Hali si shwari ndani ya CCM, Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Bashiru Ally amekemea vikali baadhi ya wanachama wanaopanga kukisaliti chama

Wewe unaamini shazi la mikutano ya Jiwe??? Watu wanapiga pesa jombaa si unajua mzunguko wa hela ulivyo mbovu mikoani na nchini kwa ujumla???

Alafu kama mtu kumuona Ali Kiba kwenye fiesta hadi alipie 10,000 Kwa nini asiende kumuona bure kwenye mkutano wa Ccm??

Yaani mtu unalipwa kwenda kuwaona wasanii wa sanaa na wasanii wa siasa... kwanini usiende?? Na ikibidi unazomea kabisa...!!
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ameeleza kuwa baadhi ya wanasiasa mpaka kuisha kipindi hiki cha Kampeni, wataokota makopo kwa kukosa uelekeo wa siasa.

ameyasema hayo leo tarehe 19 Septemba, 2020 katika kikao cha Halmashauri kuu ya wilaya ya Kyerwa.

"Wanaohama kutoka CCM wakidhani wananguvu, wakitoka wanageuka kama vichaa, wafuatilieni wote waliohama CCM, hakuna mwanaCCM maarufu kuliko CCM,"

Aidha Dkt. Bashiru amefafanua kuwa "Ukiona we maarufu ujue umeazimwa umaarufu huo na CCM , siku Chama kikikutupa ama ukikitupa umaarufu unakoma hapo hapo. Wapo watakaookota makopo ninawahakikishia."

"Kuna watu wapo miguu juu kama mende, tena miguu juu kwa raundi moja ya kampeni wakati zipo sita, wamejileta wenyewe, wajanja kama mzee Mrema na Cheyo wakasema hapa tunamuunga mkono Magufuli, waliobaki wote tusilaumiane, tutatumia nguvu zote za CCM bila kujali udhaifu wao, tutatumia uwezo wetu wote bila kujali udhaifu wao, tutawashinda, hadharani kwa kishindo.." Katibu Mkuu ameeleza

Aidha, Katibu Mkuu ameeleza namna Chama kilivyojipanga kuhakikisha kinaboresha maslahi ya wakulima na kukata mirija ya wanyonyaji katika biashara ya mazao ikiwemo zao la Kahawa.

"Tunataka kufanya utafiti badala ya kutegemea zao moja la kahawa. Hatumaanishi kwamba tunaliacha, tunataka pia kujenga viwanda vya kusindika, kile kiwanda kilichokufa cha TANICA tunataka kukifufua, tunataka kuimarisha ushirika kwa kuwa na viongozi wenye uweledi, waaminifu na waadilifu."

Katibu Mkuu amefafanua pia kwa kueleza kuwa, "Tunataka muwe na sauti kuhusu bei ya kahawa yenu, lakini tunataka kukata mirija ya unyonyaji wa jasho lenu , kama mirija ipo kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya tutaikata, kama ipo kwenye polisi tutaikata, kama ipo kwa walanguzi tutaikata, kama ipo kwenye Chama tutaikata, sasa si kutumbua majipu, zamu inayokuja ni kukata mirija ya unyonyaji."

Kikao hiko, kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali, wakiongozwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Ndg. Wilbroad Mutabuzi

Kikao hiko ni mfululizo wa vikao vya ndani vinavyoendelea nchi nzima, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha umoja, mshikamano, nidhamu na ushirikiano, kuhakikisha ushindi mkubwa unapatikana katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020.

Imetolewa na;
Said Said Nguya
Afisa Habari
Ofisi ya Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
Katibu wa ccm anahangaika kama kuku anataka kutaga
 
Hivi wewe kwa jinsi magufuli alivyowatukana wahaya kwenye tetemeko na jinsi alivyowatesa kabendera na mama yake hadi mama yake akafariki kwa akili zako unategemea magufuli aungwe mkono na wahaya????

Magufuli akipata hata kura 100 za wahaya iyo October 28 a Shukuru sana Mungu!
Bravo Wahaya. Ngoma inogile. Kura yenu mmeshaanza kupiga. Bwana yule OUT.
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ameeleza kuwa baadhi ya wanasiasa mpaka kuisha kipindi hiki cha Kampeni, wataokota makopo kwa kukosa uelekeo wa siasa.

ameyasema hayo leo tarehe 19 Septemba, 2020 katika kikao cha Halmashauri kuu ya wilaya ya Kyerwa.

"Wanaohama kutoka CCM wakidhani wananguvu, wakitoka wanageuka kama vichaa, wafuatilieni wote waliohama CCM, hakuna mwanaCCM maarufu kuliko CCM,"

Aidha Dkt. Bashiru amefafanua kuwa "Ukiona we maarufu ujue umeazimwa umaarufu huo na CCM , siku Chama kikikutupa ama ukikitupa umaarufu unakoma hapo hapo. Wapo watakaookota makopo ninawahakikishia."

"Kuna watu wapo miguu juu kama mende, tena miguu juu kwa raundi moja ya kampeni wakati zipo sita, wamejileta wenyewe, wajanja kama mzee Mrema na Cheyo wakasema hapa tunamuunga mkono Magufuli, waliobaki wote tusilaumiane, tutatumia nguvu zote za CCM bila kujali udhaifu wao, tutatumia uwezo wetu wote bila kujali udhaifu wao, tutawashinda, hadharani kwa kishindo.." Katibu Mkuu ameeleza

Aidha, Katibu Mkuu ameeleza namna Chama kilivyojipanga kuhakikisha kinaboresha maslahi ya wakulima na kukata mirija ya wanyonyaji katika biashara ya mazao ikiwemo zao la Kahawa.

"Tunataka kufanya utafiti badala ya kutegemea zao moja la kahawa. Hatumaanishi kwamba tunaliacha, tunataka pia kujenga viwanda vya kusindika, kile kiwanda kilichokufa cha TANICA tunataka kukifufua, tunataka kuimarisha ushirika kwa kuwa na viongozi wenye uweledi, waaminifu na waadilifu."

Katibu Mkuu amefafanua pia kwa kueleza kuwa, "Tunataka muwe na sauti kuhusu bei ya kahawa yenu, lakini tunataka kukata mirija ya unyonyaji wa jasho lenu , kama mirija ipo kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya tutaikata, kama ipo kwenye polisi tutaikata, kama ipo kwa walanguzi tutaikata, kama ipo kwenye Chama tutaikata, sasa si kutumbua majipu, zamu inayokuja ni kukata mirija ya unyonyaji."

Kikao hiko, kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali, wakiongozwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Ndg. Wilbroad Mutabuzi

Kikao hiko ni mfululizo wa vikao vya ndani vinavyoendelea nchi nzima, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha umoja, mshikamano, nidhamu na ushirikiano, kuhakikisha ushindi mkubwa unapatikana katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020.

Imetolewa na;
Said Said Nguya
Afisa Habari
Ofisi ya Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
Upuuzi mtupu.
 
Quinine,
Unawatishia wanachama? Waliotia Nia kugombea ccm na kukosa kura au kukatwa majina yao 100% wapo upinzani. Watumishi wa Umma wako upinzani 100% watumishi wa umma walio tia Nia kugombea na kukatwa mishahara yao,kutolipiwa madeni ya bank na kuwachangia uchaguzi fedha zaidi ya milion moja kila mjumbe wako upinzani 100% vyeti feki wako upinzani 100% wafanyabiashara wako upinzani 100% waliokuwa na maduka yakubadilishia fedha wako upinzani 100% walio hitimu vyuo wako upinzani 100% wakulima na wafugaji usiseme. Tafuteni suluhu na haya makundi mkitaka chama kiwe salama. Hali sio shwari.

Siyo hayo tu, kuna watu hawajaathiriwa moja kwa moja na mfumo mbovu wa uongozi wa magu lakini roho zao zipo upinzani, hata kama hujaguswa ile kuona wapinzani wananyanyaswa na kupewa kesi za kubambikiwa, Mpinzani mmoja amenusurika kuuawa kwa risasi nyingi na uchunguzi haujafanyika hadi leo, kuona watu wakifilisiwa kwa sababu ambazo ni petty ambapo zingetumika njia zisizo na madhara kumuadhibu mhusika (Manji) badala ya kuharibu biashara zake zilizotoa ajira za maelfu ya watu, kuona Rais akiisigina katiba kwa miaka mitano mfululizo, kuona Rais amejigeuza mungu-mtu kila mtu anamwabudu, kuona kuna sehemu zikididimizwa kimaendeleo na zingine zikipendelewa, na madudu mengine mengi, haya mambo yamechosha watu lazima sote tuwe upinzani.

WaTz tuache ubinafsi tujifunze kupaza sauti na kufanya maamuzi kwaajili ya wengine, kwa yanayoendelea nchini haihitaji uathiriwe moja kwa moja ndipo uone upinzani ni mbadala. Yanayoendelea ni machafu tuyapinge kwa nguvu zote hata kama unajiona uko safe kwa sasa.

Tuwachague wapinzani ili tuwadai katiba mpya ambayo itatumika kuwaondoa na wao wakiharibu. Hakuna chama kinachotakiwa kujiona kina hati miliki ya kuiongoza nchi hii pekeyao, CCM hawawezi kutupa katiba mpya kwasababu hawajawahi kuiahidi, Shime watanzania.
 
Katibu Mkuu wa CCM Ndg Bashiru Ally Kakurwa amekemea vikali tabia za baadhi ya wanachama wa CCM wanaopanga kukisaliti Chama katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu kwa maslahi yao binafsi. Ameahidi kuwachukulia hatua kali watakaobainika kusaliti Chama ikiwemo kuwafukuza Uanachama.



Maoni ya Kada wa CCM.

Wanaoitwa "wasaliti" ni wachache tu; wala Katibu Mkuu hakutakiwa kulizungumzia hilo kwani ni haki yao ya kikatiba. Sumaye, Lowassa, Kingunge na Mwapachu walikuwa ni "wasaliti" wakuu sana mwaka 2015 lakini tunajua yalivyoisha!
 
35 Reactions
Reply
Back
Top Bottom