VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Hali ni tete kwa mgombea wetu wa CCM hapa katika Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi. Katambi ambaye alikataliwa na 'Wajumbe' wakati wa kura za maoni ndani ya CCM, alipitishwa 'kibabe' na Kamati Kuu na NEC ya CCM kule Dodoma. Katambi, katika kura za maoni, aliachwa mbali mno na aliyekuwa Mbunge wa hapa Steven Masele ambaye jina lake lilikatwa Dodoma.
Katika kuonesha kinyongo kisicho na uongo, makada wa CCM hapa Shinyanga Mjini wamekuwa wakijitenga na Katambi hadharani na sirini. Katika harakati za kuokoa jahazi na kuulinda ushindi wa CCM, Mbunge wa zamani Masele 'ameombwa' na viongozi waandamizi wa CCM Taifa kumsaidia Katambi katika kampeni zake. Ameahidiwa kuwa endapo CCM ikishinda Urais atapatiwa nafasi ya Ubalozi au nyingine tamutamu.
Masele hana tatizo na hilo. Lakini, wafuasi na wasukamipango wake wamegoma 'kumruhusu' kumsaidia Katambi wakidai kuwa Katambi hauziki hata kama utapigwa na muziki. Pamoja na kwamba CCM ndiyo watetezi wa hapa Shinyanga Mjini, hali yetu si nzuri kulingana na taswira iliyochorwa ya mgombea wetu. Katambi anatajwa kama asiye na ushawishi wowote na kusemwa kuwa 'anatakiwa' tu Bungeni kwenda kuwaongelea mbovu wapinzani.
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Shinyanga Mjini)
Katika kuonesha kinyongo kisicho na uongo, makada wa CCM hapa Shinyanga Mjini wamekuwa wakijitenga na Katambi hadharani na sirini. Katika harakati za kuokoa jahazi na kuulinda ushindi wa CCM, Mbunge wa zamani Masele 'ameombwa' na viongozi waandamizi wa CCM Taifa kumsaidia Katambi katika kampeni zake. Ameahidiwa kuwa endapo CCM ikishinda Urais atapatiwa nafasi ya Ubalozi au nyingine tamutamu.
Masele hana tatizo na hilo. Lakini, wafuasi na wasukamipango wake wamegoma 'kumruhusu' kumsaidia Katambi wakidai kuwa Katambi hauziki hata kama utapigwa na muziki. Pamoja na kwamba CCM ndiyo watetezi wa hapa Shinyanga Mjini, hali yetu si nzuri kulingana na taswira iliyochorwa ya mgombea wetu. Katambi anatajwa kama asiye na ushawishi wowote na kusemwa kuwa 'anatakiwa' tu Bungeni kwenda kuwaongelea mbovu wapinzani.
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Shinyanga Mjini)