amina ngalo
JF-Expert Member
- Jun 13, 2013
- 309
- 170
*Hali si hali Jiji la Arusha*
Hali ya mambo katika halmashauri ya Jiji la Arusha inaonekana kuwaendea vibaya madiwani wa chama cha demokrasia na maendeleo ambao ndio wengi katika baraza la madiwani.
Katika kikao cha Finance kilichofanyika katika ukumbi wa Jiji, vyanzo vyetu vya kuaminika vinatunyetisha kwamba madiwani hao wameendelea kulalamikia ubabe wa mkurugenzi wa Jiji la Arusha bwana Athumani Kihamia na mpaka kufikia hatua Meya wa Jiji hilo Kalisti Lazaro kufikia hatua ya kutishia kumwaga damu ili kufikisha ujumbe ya kwamba ilani yao ya Chadema inapuuzwa na mkurugenzi huyo na kila wanapompa maelekezo huyapuuza. Hii ni kufuatia sakata la maduka ya stendi ndogo yanayogombaniwa na wapangaji ambao inadaiwa ni wanachadema.
Wanadaiwa kupokea rushwa toka kwa wapangaji kuvuruga utaratibu wa vikao ni diwani wa Levolosi Ndg Efatha Nanyaro na wa Ngarenaro Mhe. Doita pamoja na Naibu meya.
Sisi kama wapenda amani katika jiji hili tunaviomba vyombo vya ulinzi na usalama kufuatilia kauli kama hizi kwani zina viashiria vya uvunjifu wa amani hasa ukizingatia historia ya CHadema kuvuruga amani jijini Arusha.
Pili tunapenda kuwakumbusha madiwani wa Chadema ya kwamba ilani inayotekelezwa kwa sasa ni ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwani ndicho chama kilichopewa ridhaa na wananchi mpaka mwaka 2020.
Hali ya mambo katika halmashauri ya Jiji la Arusha inaonekana kuwaendea vibaya madiwani wa chama cha demokrasia na maendeleo ambao ndio wengi katika baraza la madiwani.
Katika kikao cha Finance kilichofanyika katika ukumbi wa Jiji, vyanzo vyetu vya kuaminika vinatunyetisha kwamba madiwani hao wameendelea kulalamikia ubabe wa mkurugenzi wa Jiji la Arusha bwana Athumani Kihamia na mpaka kufikia hatua Meya wa Jiji hilo Kalisti Lazaro kufikia hatua ya kutishia kumwaga damu ili kufikisha ujumbe ya kwamba ilani yao ya Chadema inapuuzwa na mkurugenzi huyo na kila wanapompa maelekezo huyapuuza. Hii ni kufuatia sakata la maduka ya stendi ndogo yanayogombaniwa na wapangaji ambao inadaiwa ni wanachadema.
Wanadaiwa kupokea rushwa toka kwa wapangaji kuvuruga utaratibu wa vikao ni diwani wa Levolosi Ndg Efatha Nanyaro na wa Ngarenaro Mhe. Doita pamoja na Naibu meya.
Sisi kama wapenda amani katika jiji hili tunaviomba vyombo vya ulinzi na usalama kufuatilia kauli kama hizi kwani zina viashiria vya uvunjifu wa amani hasa ukizingatia historia ya CHadema kuvuruga amani jijini Arusha.
Pili tunapenda kuwakumbusha madiwani wa Chadema ya kwamba ilani inayotekelezwa kwa sasa ni ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwani ndicho chama kilichopewa ridhaa na wananchi mpaka mwaka 2020.