Hali mbaya Mlima Kilimanjaro

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,448
154,313
Barufu yayeyuka kwa kasi.

201710_10152026152545416_738045738_o.jpg
 
inasikitisha sana, sijui tufanyeje.
tuwekeane sheria ya kupanda miti kila mwaka as individuals sio kusubiri serikali.
Nakumbuka wakati nasoma secondary school, tulikuwa tunabeba kila mtu mche mnapandisha milimani kwenda kupanda. Huu ni utaratibu mzuri sana kw maoni yangu. Na unajenga uzalendo wa kutunza mazingira kwa vijana wadogo
 
nasikia kuna ndege za wazungu zinapita hapo kileleni na kumwaga magunia ya chumvi ili barafu iyeyuke
 
Mbona hiki hakionyeshi kama ni kilele cha mlima kilimanjaro? Kwani hiyo barafu ikiwepo au isiwepo inaathiri nini kwenye utalii wa mlima kilimanjaro?
 
Wanaoutunza ule mlima ni watu wanaouzunguka ie Rombo, Marangu etc! Je serikali inatambua mchango wa hawa watu? Pato la utalii wa huo mlima limewanufaisha wenyeji kivipi? Yanapotokea majanga kama ya moto ni nini chanzo na serikali imereact vp? Uharibifu wa mazigira nao je? Wanaoharibu ni wenyeji au ni kinaa nan? Na y waharibu?.....i think soon huu mlima utabakia history kama hatutafanya kitu!
 
Lawama kwa serikali na wananchi hatuna utamaduni wa kutunza mazingila yetu:confused2:
 
Dahh... yaani ile barafu imegeuka nusu jangwa. Zile mbwembwe kama Mlima wenye kilele cha barafu n.k zitakoma.
Je TANAPA, Warombo, Wakibosho n.k wapo wapi? Au mnataka tujisingizie ni tabia ya nchi. Sioni fahari ya kurudi Moshi, siwezi kuona kilele cha barafu asubuhi na jioni.
 
Acha kudanganya watu. hiyo siyo picha ya kilele cha mlima Kilimanjaro. nitajitahidi nikuwekee picha halisi ya kilele cha mlima Kilimanjaro.
 
nasikia kuna ndege za wazungu zinapita hapo kileleni na kumwaga magunia ya chumvi ili barafu iyeyuke

Ina maana hazionelani kwenye rada???? Au ni za kijajusi zaidi????

Suala mlima Kilimanjaro barafu kuyeyuka linaendana sana na mabadiliko ya tabia nchi.
 
giLESi - hiyo picha uliyopost siyo ya "kilele cha mlima Kilimanjaro"...! Nadhani ilikuwa posted na "wahalifu" Fulani wakati wa shindano la kutafuta "maajabu ya dunia" mwaka jana ili kudanganya "wapiga kura"...!
 
Last edited by a moderator:
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom