Hali mbaya: Makampuni ya simu yaanza kupunguza wafanyakazi. ITV yasogeza mishahara mbele

Poleni sana kwa mliopunguzwa!
Muombeni Mungu zaidi huenda kuna kubwa zaidi kawaaandalia kwani maandiko yanasema mlango mmoja wa neema ukifungwa hufunguliwa milango sabini ya neema.
Maandiko yanasema wapi? Acha uzushi..
 
Mbona kama heading haiendani na content....??? Manake tumeambiwa Airtel ndo anapunguza staff lakini ukisoma huo mkeka ni iSON BP ndo waliotoa hilo tangazo na wanawataja Airtel kama client wao muhimu ambae kaathirika na call volume shortage....... Jamani, tusipende kuhabarisha umma kishabiki madhara yake n makubwa sana kuliko faida kiduchu unayoipata ww mtoa taarifa, Tanzania first (in Trump's voice)
 
Ndo wachape kazi sasa hao wachache maana walikuwa wengi walikuwa wakishinda wakisoma magazeti ukipiga cm huduma kwa wateja hadi chaji inaisha bila kujibiwa cm
 
Naona hata hujui una comment nini.Soma mada husika kama ni kweli taarifa ni rasmi lakini sio unalau Serikali.

Hakuna anayemtesa mwanainchi ndani ya nchi ila unarudishwa kuishi maisha yako halisi na siyo ya kuigiza wakati hali yako haifanani na uhalisia.

Sasa ndiyo kila mmoja aishi kama alivyotakiwa kuishi na pesa IPO ukiitafuta utapata.hakuna mteremko
Kwahiyo haya maisha ya wananchi kulia njaa ndio maisha halisi tuliyozoea kuishi siyo?
 
Sekta binafsi ndiyo kila kitu maisha yako wewe Na ndugu zako .!

Tuombee jambo hili tusifanye mzaha kwamba ni la Fulani

Ilianzishwa kwa mujibu Wa sheria Na imeajiri Watu wengi .

Isipolindwa itakufa hakuna atakayebaki hata uwe rasmi !
 
Kweli nchi yetu ilikuwa inaliwa na wachache, sasa haya makampuni kweli yalikuwa yanakua kivipi na pesa ya serikali yetu?
Ni keamba serikali imebana nao wanakumbwa, lazima kuna mteremsho walizoea kuupata na awamu hii yamewakuta.

Kuanzia kodi etc
ITV wanatarajia kupata mapato yao kutoka kwenye matangazo, biashara huku uraiani hazifanyi vizuri, serikali imebana kila kona, kuanzia raia mmoja mmoja mpaka taasisi binafsi, unadhani hayo matangazo wanapata wapi?

Makampuni ya simu yana retrench ili kupunguza gharama, wanashusha hadi viwango vya bundles na dk za kuongea kwa bei ile ile. Mpaka mwezi wa tatu makampuni mengi sana binafsi yatapunguza wafanyakazi kwa ajili ya kushusha operating costs ili kupata faida. Same to banks, zimepata faida kiduchu sana kwa mwaka ulioisha, je tutegemee nini kama si kupunguza wafanyakazi?

Afu bado kuna graduates wako mtaani ajira hazijatoka kwa muda mrefu, inaumiza kwa kweli huyu mtu aambiwe ukweli
 
fb_img_1485364106564-jpg.463774


Ina maana kampuni hii haina reserve funds? Halafu matatizo ya mwajiri na wadeni wake yanamhusu vipi mfanyakazi? Je, hao wanaodaiwa na hii kampuni ni private sector pekee?
Hata TRA ni hivi hiv
 
Hali tete hili balaa linashuka kwa wananchi magufuli kuwa na huruma sasa inatosha hizi sera zitaua nchi kaka na moral pia hakuna tena usiturudishe miaka 50 iliopita plsss
 
Si kwamba uchumi wa nchi umeathirika .... hapana .... ni kwamba uchumi wa nchi UMEBADILIKA.

Hivyo njia kuu za uchumi zilizokuwepo kama hayo makampuni tajwa lazima yatetereke na kuathirika.

Kutaanzishwa njia kuu mpya za uchumi kuendana na MABADILIKO YA KIUCHUMI.

Kiufupi tunaachana na soko huria au economic liberilasation na kuanzisha MODEL mpya ya semi - state controlled economy. Hata Trump naye amefanya hivyo huko amerika. Maana yake ni kwamba utandawazi umeshindwa kutatua changamoto za dunia hivyo lazima kuwepo na mfumo mpya.

Blaah blah blah...

Haya huo uchumi umebadirika, umebadirika vipi sasa mbona usemi?

Umeongezeka, umepanda, umesonga mbele au umerudi kinyume kinyume?

Acheni kuleta politcs wakati hata kwa asiye jua kusoma wala kuandika anajua hali ya uchumi ilivyo kwa sasa hapa nchini.
 
Haya mafanikio yametokana na mageuzi ndani ya chama na uchapakazi wa mheshimiwa.....in Hamfuraii Harakaharaka voice (mwenezi wa chamadola)
 
Inabidi wapunguzwe tu, nimekwenda kusajili laini yangu zaidi ya mara 5 na kila nikicheki kwa *106# naambiwa usajili haujakamilika, yaelekea wengine hawajui kazi zao!
Hata mimi vodacom huwa wananitumia SMS kuwa usajiri wangu ni wa awali, nilishaenda kwa mawakala kama 2 hakuna muafaka hadi nikaenda mlimani city. Hadi Leo natumiwa SMS kuwa usajiri wangu ni wa awali. Nimechoka na ujinga wao nangojea wanifungie nihamie mitandao mingine. Hakika wameajiri mizigo acha tuu itumbuke hamna namna. Ni mbaya ukiwa nayo, heri waisome namba tuu
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom