Hali halisi ya barabara zetu hapa Tanzania

Mmawia

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
121,918
95,201
#KIBONDO
Wakati wa mvua, wakati wa masika hali ya barabara inakuwa ni ngumu sana kupitika kutokana na mvua zinazonyesha, eneo hili lina udongo wa kunata sana jambo ambalo ikichanganyikana na mvua inakuwa ni mtelezo wa tope.

Hili ni bus la kampuni ya Adventure mnamo Dec 4 mwaka huu katika eneo la Kumwambu Kibondo mjini barabara ya Kasulu, Kigoma Tanzania. Mbunge wa hapa ni ndugu Atashasta Nditiye (MB), ambae pia ni Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano.

Tunaomba serekali mtufikirie kwa jicho la tatu Kigoma mmetuacha sana.

Ni wakati muafaka sasa viongozi wetu mlitupie jicho la tatu suala la barabara na ikibidi punguzeni bajeti za kununulia ndege ili mtujengee barabara sisi walala hoi.

FB_IMG_1575809471808.jpeg
 
Kuna watu wachache sana wanafaidi mema ya nchi na akili yao imekomea buza ambako mabaharia wanaita nyuma ya airport ila wakiambiwa maisha wanayoishi robotatu ya wananchi hawawezi kuelewa kabisa..hapo ndipo napopata kigugumizi kila nisikiapo mtawala akilalamika na mwananchi naye akilalamika...labda tusubiri tena arudi mkoloni mara ya pili kisha tutafute uhuru huenda mambo yakawa tofauti na ya sasa!
 
Back
Top Bottom