CHIEF MASALAKULANGWA
JF-Expert Member
- Apr 8, 2021
- 794
- 646
Hizo nchi ulizozitaja zina uongozi gani bora, hasa hasa kabla ya kujitambua, kutambua wezi wao na kuamua kujitegemea, uongozi wao ulikuwa kama wa kwetu tu!Mataifa mengi yaliyowahi kuwa makoloni ni pamoja na China, Korea Kusini, India, Indonesia, Vietnam, Singapore, Brunei, Malaysia.
Haya ni baadhi ya mataifa yaliyowahi kuwa makoloni kwa muda mrefu ila yameshaachana na ujinga wa kusingizia wakoloni badala yake yanachuana kiuchumi na wakoloni wao kwa sasa.
Tatizo la Africa kudumaa kimaendeleo ni uongozi mbaya, usio na maona, unaotanguliza maslahi binafsi ya watu wachache.Tusiendelee kujificha kwenye kichaka cha ukoloni, tunaonekana wajinga tu.