Hakuna tofauti kati ya Iphone 12 na Iphone 13

Cinematic ya 1080p. Thats trash.

Akiweka cinematic ya 4k hiyo simu itawaka moto.

Sio trash mzee we call it progress... sasa wewe ulitaka aanze na kuweka Cinematic Mode ya 8K halafu hiyo video ungeangalia kwenye Tv ipi kama ww ni super rich sio mbaya.technology yetu bado kama Movie ya 8K ilisumbua kuonyesha kwenye cinemas kuwa mpole tu, hivi vitu vinahitaji time na resources...tutafika huko tu.
 
Kuna watu wanasema Steve Jobs alikufa na Ubunifu wake pale Apple. Hii inaweza kuwa kweli.

Angalia, leo Apple wamezindua simu mpya ya Iphone 13, ukiiangalia simu na hata matangazo yake yameionyesha hakuna tofauti na Iphone 12 ya mwaka jana. Watu wengine wanasema ni bora Apple wangeiita Iphone jina la Iphone 12s badala ya Iphone 13.

Specifications sheet haina tofauti yoyote na spec sheet ya mwaka jana.

Hadi sasa Samsung Galaxy S21 Ultra amezifunika zote, Iphone 12 line na Iphone 12s line aka Iphone 13.

Apple kwenye ubunifu alishaachwa nyuma na simu hizi za android kitambo sana.

Tusubiri labda mwaka kesho tukiwa wazima, inasemekana Apple atakuja na Iphone yenye muundo mpya kabisa ya kila kitu under display na kuondoa lile dirisha pale juu ama notch.
Sisi wa simu zinazopiga kelele wakati zinaita, hakuna hata pa kupunguza sauti tunaruhusiwa hapa?
 
Sio trash mzee we call it progress... sasa wewe ulitaka aanze na kuweka Cinematic Mode ya 8K halafu hiyo video ungeangalia kwenye Tv ipi kama ww ni super rich sio mbaya.technology yetu bado kama Movie ya 8K ilisumbua kuonyesha kwenye cinemas kuwa mpole tu, hivi vitu vinahitaji time na resources...tutafika huko tu.
Mkuu kama umegundua humu watu hawatoi maoni kitaalam bali wana kitu kama Chuki hivi dhidi ya Apple Products as if wamelazimishwa kutumia. Kingine ujuaji ni mwingi mnoo yaani.
 
Sio trash mzee we call it progress... sasa wewe ulitaka aanze na kuweka Cinematic Mode ya 8K halafu hiyo video ungeangalia kwenye Tv ipi kama ww ni super rich sio mbaya.technology yetu bado kama Movie ya 8K ilisumbua kuonyesha kwenye cinemas kuwa mpole tu, hivi vitu vinahitaji time na resources...tutafika huko tu.
Ila mtu anaye afford iphone 13 tv ya 4k ama 8k haimshindi, siku hizi 4k chini ya milioni unapata.
 
Mkuu kama umegundua humu watu hawatoi maoni kitaalam bali wana kitu kama Chuki hivi dhidi ya Apple Products as if wamelazimishwa kutumia. Kingine ujuaji ni mwingi mnoo yaani.

Kweli wengine wanachukia Apple products kisa wameskia watu wanaiponda tuwe objective katika ku reason. kiukweli Apple enzi za steve jobs walikuwa ahead of time na ndio kitu kinachohitajika kwenye Technology Microsoft alivyoleta window alikuwa mbele ya mda wake, Elon Musk na Tesla zake Kawa mbele ya mda he’s dominating the Market... zaman iPhone used to be that..Leading innovation na uniqueness. Siku hizi Not so much
 
Ila mtu anaye afford iphone 13 tv ya 4k ama 8k haimshindi, siku hizi 4k chini ya milioni unapata.
Tv za 4k resolution hata 400k unapata hizi Hisense inchi 32 ama tcl. Watu tumeanza kuangalia tv za 4k muda mrefu na ndio zimedominate soko la tv kwa sasa hata za bei ya chini kabisa.

Nashangaa mtu kusema eti 4k ama 8k tv zinasumbua
 
Tv za 4k resolution hata 400k unapata hizi Hisense inchi 32 ama tcl. Watu tumeanza kuangalia tv za 4k muda mrefu na ndio zimedominate soko la tv kwa sasa hata za chini kabisa.

Nashangaa mtu kusema eti 4k ama 8k tv zinasumbua

Sijasema hivyo elewa nilichokiandika nimeongelea kwamba 8K Movie inasumbua Cinema sio Kwenye Tv nimesema Cinema umenisoma sijui. Mfano Will smith’s Movie Gemini Man wali shoot kwa Camera za 8K baadhi ya Theatre ikiwemo za nje zilisumbua kuonyesha...Kwahiyo kama unaendelea kushangaa wewe shangaa
 
Tv za 4k resolution hata 400k unapata hizi Hisense inchi 32 ama tcl. Watu tumeanza kuangalia tv za 4k muda mrefu na ndio zimedominate soko la tv kwa sasa hata za bei ya chini kabisa.

Nashangaa mtu kusema eti 4k ama 8k tv zinasumbua
Hizo 4K za laki 4 ni kanjanja! 4K has to do with pixels ambazo ziko kwenye screen! Kioo cha 32 inches ni kidogo kupack hizo pixels atleast kuanzia 50 inches au zaidi ndio zinaweza kuwa na true 4K pixels!
 
Sijasema hivyo elewa nilichokiandika nimeongelea kwamba 8K Movie inasumbua Cinema sio Kwenye Tv nimesema Cinema umenisoma sijui. Mfano Will smith’s Movie Gemini Man wali shoot kwa Camera za 8K baadhi ya Theatre ikiwemo za nje zilisumbua kuonyesha...Kwahiyo kama unaendelea kushangaa wewe shangaa
Halafu haya mambo ya 8k wewe ndio umeyaleta.

Mimi nilizumza Cinematic 4K ambazo tayari nimeshaziona kwenye makampuni mengine mengi tu.
 
Hizo 4K za laki 4 ni kanjanja! 4K has to do with pixels ambazo ziko kwenye screen! Kioo cha 32 inches ni kidogo kupack hizo pixels atleast kuanzia 50 inches au zaidi ndio zinaweza kuwa na true 4K pixels!
Ni kweli ngumu kukuta 4k ya inch 32, ila zipo, wapo wachina wanaochakachua ila pia zipo 4k za ukweli.

Mfano samsung QN32Q60AAFXZA
 
Halafu haya mambo ya 8k wewe ndio umeyaleta.

Mimi nilizumza Cinematic 4K ambazo tayari nimeshaziona kwenye makampuni mengine mengi tu.

Na kwahiyo 4K Cinematic Mode unayoitaka itabid kununua Model ya 1TB kwa maana 128Gigs base model itakuwa ni kuleta kisu kwenye gunfight
 
Na kwenye simu wanapack vipi pixel za 4k kwenye display ambayo ni less than 7 inch?
Wanadanganya tu sababu hutaziona yani! Ile clarity ya 350 ppi kwenye simu inatosha mno mtu kukwambia simu ni ya 4K na usijue!
 
Kuna watu wanasema Steve Jobs alikufa na Ubunifu wake pale Apple. Hii inaweza kuwa kweli.

Angalia, leo Apple wamezindua simu mpya ya Iphone 13, ukiiangalia simu na hata matangazo yake yameionyesha hakuna tofauti na Iphone 12 ya mwaka jana. Watu wengine wanasema ni bora Apple wangeiita Iphone jina la Iphone 12s badala ya Iphone 13.

Specifications sheet haina tofauti yoyote na spec sheet ya mwaka jana.

Hadi sasa Samsung Galaxy S21 Ultra amezifunika zote, Iphone 12 line na Iphone 12s line aka Iphone 13.

Apple kwenye ubunifu alishaachwa nyuma na simu hizi za android kitambo sana.

Tusubiri labda mwaka kesho tukiwa wazima, inasemekana Apple atakuja na Iphone yenye muundo mpya kabisa ya kila kitu under display na kuondoa lile dirisha pale juu ama notch.

Pamoja na yote nitainunua tuu
 
Wanadanganya tu sababu hutaziona yani! Ile clarity ya 350 ppi kwenye simu inatosha mno mtu kukwambia simu ni ya 4K na usijue!
Sasa simu itakuwaje na display ambayo siyo 4k halafu iplay video za 4k.

Maana mfano mimi simu yangu inashoot 4k ila hizo video haziplay kwenye simu yangu nyingine wala kwenye laptop wala kwenye TV.
 
Sasa simu itakuwaje na display ambayo siyo 4k halafu iplay video za 4k.

Maana mfano mimi simu yangu inashoot 4k ila hizo video haziplay kwenye simu yangu nyingine wala kwenye laptop wala kwenye TV.
Rendering tu inafanyika! Zinakuja kwenye full HD quality ambayo ni ndogo kuliko 4K ila still ni clear
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom