Hakuna tatizo miradi mikubwa ya kimkakati kuelekezwa Chato

Hivi hawoni aibu?Ngoja na uwanja mkubwa wa mpira wa mguu wa kimataifa uanze kujengwa hapo Chato,Pengine mataga watashtuka!
 
Nimekaa nakutafakari sasa tunakoelekea sio pazuri.

Serikali inajenga hospitali ya rufaa Chato,wafuasi wa upinzani wanazodoa na kupinga.

Kwani hii Hospitali haitawahudumia watanzania?

Kwani kujengwa Chato ndio tatizo?

Mfano, mkazi wa Dar es Salaam akiwa Runzewe anaendesha truck kwenda Rwanda,ghafla anapata ajali,Je hawezi kupelekwa Chato na kupata huduma za tiba? Huu ni mfano.

Nini hasa kinawafanya mzodoe na kupinga ujenzi wa hii hospitali muhimu? Rais JPM kuwa ametokea Chato?

Nadhani ni kipindi muafaka Askofu Bagonza na Askofu Mwamakula kuwaombea hawa vijana waliokengeuka kisiasa ili uzalendo uwarudie na kuipenda nchi yao.
HIVI HUYU MKUU ANAWALIPA KIASI GANI?
 
Ama kweli wachato mmebarikiwa nyrere alikuwa lofa Sana.

Airport chato
Referal hospital chato
Crdb chato
Pccb sijui chato
Wang yi chato
Filipe nyusi chato
National Park chato
Futuboli stadium chato
Modern VETA chato

Blesed people we Wana come chato in pilgrimage.
Eti "Filipe Nyusi......Chato"
😂😂
 
NI HASARA SANA KWA NCHI KUBWA KAMA TANZANIA KUWA NA VIONGOZI WASIO HAYA WALA SONI KAMA TULIENAE.Hata aibu haipo na wajinga wanaendelea kusifu ilhali maeneo watokayo hayana kitu chochote na ndugu zao wanakufa kila uchao kwa kukosa huduma mambo yote ni ubabe juu ya ubabe.Nakumbuka mjinga mmoja aliwahi kusema we need magufulilization of Africa,Sasa unaweza ukaona madhara ya kumsifu mtu kabla hakujakucha,yaani unamuona usiku wala hujamuona vzr kutokana na giza unaanza kumsifu na wala usisubiri kukuche.
 
Mkuu ili kufungua hospital kwabwa namna hiyo somewhere kuna factor nyingi unaconsider and one of them inaweza kuwa accessibility etc.Chato inaweza isiwe na sifa hata moja kati ya hizo
Unajua Hospital ya Rufaa ya kanda ya kusini inakojengwa?
 
Yaani hospital ya rufaa ya kanda inajengwa kijijini na still huoni tatizo? Tupe sababu za msingi on why ni chato na si mwanza,shinyanga,Tabora Geita au Kigoma mjini
Hospitali ya wilaya ya Mwanga Kilimanjaro imejengwa Usangi juu Milimani huko na ni kipindi hiko na inasaidia watu wote ni vizuri kuruhusu MAENDELEO yasambae kila corner ya nchi.

Acheni roho mbaya
 
..Wanapinga UPENDELEO.

..Magufuli alikuwa mbunge kwa miaka 20 kwanini hakupeleka miradi yote hiyo wakati akiwa mbunge na waziri?

..Kwanini miradi mingi hivyo inaibuka Chato tu na haiibuki maeneo mengine ya Tanzania?
Ina maana hujui awamu ya tano inajenva Hospital ngapi za rufaa? Inamaana hujui airport ngapi zinajenvwa mpaka leo Tanzania nzima?
 
..unapoweka veta, uwanja wa ndege, crdb, uwanja wa mpira, hospitali ya rufaa, msd, mahakama, mbuga ya wanyama, ktk jimbo moja la uchaguzi, ndani ya miaka mitatu, huo utaitwa UPENDELEO.
Jamani hivi CRDB walijenga makao makuu au walijenga tawi kama wilaya nyingine wanavyopewa matawi?
 
Hospitali ya rufaa kanda ya ziwa iko Bugando Mwanza.
Kanda ambazo hazina hospitali za rufaa za kanda ni:
1. Kanda ya magharibi: mikoa ya Kigoma, Rukwa, Katavi (hata Tabora ni mbali na Dodoma na Mwanza)
2. Kanda ya kusini mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma

Nilitarajia kama hospitali za rufaa za kanda ni kipaumbele, basi zingeanzia katika kanda hizo ambazo hazina
Lindi haina Referral Hospital aisee wewe haujui ulisemalo..
Sokoine Hospital ni hospital gani pale Lindi?

Acheni kueneza chuki.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom