Hakuna popote Rais Magufuli aliruhusu Askari wapandishwe vyeo kwa kuua Raia wema!

Pia kamhanda aliyekuwa RPC wa iringa wakati ule naye alipandishwa cheo baada kumuua mwandishi wa habari kwa maelekezo,unayeleta uzi huu ww ni mchanga sana kwenye siasa hizi unajua kipi kinaendelea ccm wakipiga siasa za majukwaani na wapinzani hairuhusiwi?waliomuua akwilina walipelekwa mahakamani?
Je ni nani anayeamua mtu fulani ni jambazi au la??
Je unajua wale mapolisi walio muua mdogo wake Heche akiwa amefungwa pingu nao pia waliachiliwa kwa kauli hiyo??
Utawala wa sheria uko wapi??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kwa nini Tundu asiseme kweli kwamba Mhe Rais hakumaanisha vile na anabaki kusema uongo kwamba Magufuli karuhusu Askari waue Raia wema?

Uhakika Wa huyu sio jambazi nani anao?

Je rais amekuwa jaji?

Mini kazi ya mahakam?
 
Mleta mada umejitoa ufahamu. Inathibitisha ule usemi mnapojiunga huko hamzihitaji akili zenu.
 
Kuna upotoshaji mwingi sana anaoufanya Tundu.Hasa la Rais kuruhusu Askari wapandishwe vyeo kwa kuua Raia.

Kilichosemwa na Mhe Rais ni Askari asikamatwe kwa kosa la yeye kupambana na kuhatarisha usalama wake na jambazi!Alienda mbele zaidi katika mapambano ya aina hiyo na wahalifu ni vyema Askari wakapewa kongole na ikibidi wapandishwe vyeo kwa kutimiza wajibu wao vyema.


Sasa sijui huyo Tundu anapata wapi nguvu na ujasiri wa kutuhumu uongo kwa kiwango kile!

Anyway,malipo ya uongo wake soon yatajibu.
Ameruhusu polisi kuua na akasema wakuia wapandishwe vyeo, hiyo nyongeza ya maelezo unayotoa ni ya kwako na sivyo alivyosema.
Lakini point hapa ni ya kuwa ni mahaka peke yake iliyopewa mamlaka kisheria kumuhukumu mtu kifo na si kauli ya mkuu wa nchi, polisi wakiua lazima ichunguzwe kama kweli ilikuwa ni self-defense au wakabiliwe na kesi ya mauaji. Sheria za nchi lazima ziheshimiwe pamoja na mapungufu yake yote.
 
Unaongea utoto gani? Rais ni mahakama kwamba anajua nani ni raia mwema? Utaratibu wa mtu asiye rais mwema ni kuuliwa na polisi? Hivyo ndio sheria zetu zinavyotaka au ni utashi wa rais?
Na mimi nilitaka nimwambie hivyo ....kwa kauli ya raisi maana yake ni kwamba yeyote atayeshukiwa kwa ujambazi asipelekwe mahakamani apigwe risasi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata tutetee vipi, kauli ya Rais kuruhusu Polisi kuua watuhumiwa, ilikuwa ni kauli mbaya kabisa kuwahi kutolewa na kiongozi mkuu kama yeye ambaye alistahili kuwa mfano wa kuzingatia sheria.

Polisi wetu hawa ambao huwawekea watuhumiwa hata bangi, huua raia na kusingizia kuwa ni majambazi, huua mahabusu na kusingizia wamekufa vifo vya kawaida, leo kiongozi mkuu anawaruhusu waue watuhumiwa, na wakiua wasishtakiwe bali wapandishwe vyeo, kauli hiyo ilimshtua kila mwenye akili timamu.

Narudia tena, ile kaulinilikuwa mbaya kabisa ambayo sidhani kama kuna kiongozi mkuu yeyote, hata yule mbaya namna gani, aliwahi kuotamka dhidi ya raia wake.
Ujumbe mzuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiutaratibu, kazi ya kutoa adhabu ya kifo ni ya mahakama sio polisi. Jeshi la polisi linapaswa kufanya jitihada kuhakikisha watuhumiwa hawafii mikononi mwao, ikishindikana, wanaweza kuua. Tatizo la kauli ya mkuu ni kama anahamisha hili jambo, na wengine hawawezi kuelewa vizuri wakaanza kutumia nguvu zao vibaya. Hata jambazi ana haki.

Na sio kila anayeitwa jambazi na Polisi ni jambazi kweli, si unakumbuka ya Zombe
 
Sasa tutajuaje ni jambazi kama hawa Askari wanawaua watuhumiwa ? Watuhumiwa wengine ni raia wema kabisa...mahakama iachiwe kazi ya kuhukumu haiwezekani polisi wakaua watu karibu kumi huku binduki za majambazi zikiwa ni mbili tu sasa hapa principle ya proportionally use of force iko wapi ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi unadhani ww ndio ulimsikiliza Lissu mwenyewe? Hata Akwilina alikuwa raia mwema na aliuwawa na polisi, je hatua gani alichukuliwa polisi aliyemuua?
Waliomuua huyo binti wapo mahakamani ndg.
 
Back
Top Bottom