mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,663
- 18,037
Kufundisha mtoto ni sawa na kujenga nyumba. Anayejenga nyumba huanza kujenga mstari wa Kwanza, halafu mstari wa pili hujengwa juu ya mstari wa Kwanza.
Hali kadhalika mstari wa tatu hujengwa juu ya mstari wa pili. Ikitokea siku ya kujengwa mstari wa pili kukatokea dharula na ujenzi usifanyike, bado dharula ikiisha mstari wa pili LAZIMA ujengwe kabla ya kujenga mstari wa tatu. Hakuna namna ya kujenga mstari wa tatu KABLA ya kujenga mstari wa pili.
Kwa hiyo mjenzi ni lazima aijenge nyumba ikamilike na LAZIMA alipwe malipo YOTE Kama walivyopatana awali.
Hali kadhalika, masomo na vipindi ambavyo watoto wangefundishwa mwezi wa nne na wa tano LAZIMA wafundishwe kabla ya kufundisha masomo na vipindi vilivyoko kwenye ratiba ya mwezi wa Saba. Ndiyo maana ni LAZIMA kutafuta nyongeza ya muda ili kufidia vipindi vilivyopotea wakati wa likizo ya dharula iliyotokana na mlipuko wa ugonjwa wa covid 19.
Kwa hiyo LAZIMA wazazi walipe ada ambayo hawakuilipa maana watoto wao LAZIMA wafundishwe na waalimu LAZIMA walipwe mishahara yao ambayo haikulipwa maana kazi wataifanya kikamilifu katika kuwafundisha watoto. Huo ndio utaratibu.
Sidhani Kama Kuna mzazi anategemea waalimu wataruka sehemu ya mada bila kuzifundisha kwa kuwa ilikuwa zifundishwe mwezi wa nne na wa tano.
Kwa mantiki hiyo haitegemewi mzazi kudhani kuwa hatadaiwa kulipa ada Yote.
Hali kadhalika mstari wa tatu hujengwa juu ya mstari wa pili. Ikitokea siku ya kujengwa mstari wa pili kukatokea dharula na ujenzi usifanyike, bado dharula ikiisha mstari wa pili LAZIMA ujengwe kabla ya kujenga mstari wa tatu. Hakuna namna ya kujenga mstari wa tatu KABLA ya kujenga mstari wa pili.
Kwa hiyo mjenzi ni lazima aijenge nyumba ikamilike na LAZIMA alipwe malipo YOTE Kama walivyopatana awali.
Hali kadhalika, masomo na vipindi ambavyo watoto wangefundishwa mwezi wa nne na wa tano LAZIMA wafundishwe kabla ya kufundisha masomo na vipindi vilivyoko kwenye ratiba ya mwezi wa Saba. Ndiyo maana ni LAZIMA kutafuta nyongeza ya muda ili kufidia vipindi vilivyopotea wakati wa likizo ya dharula iliyotokana na mlipuko wa ugonjwa wa covid 19.
Kwa hiyo LAZIMA wazazi walipe ada ambayo hawakuilipa maana watoto wao LAZIMA wafundishwe na waalimu LAZIMA walipwe mishahara yao ambayo haikulipwa maana kazi wataifanya kikamilifu katika kuwafundisha watoto. Huo ndio utaratibu.
Sidhani Kama Kuna mzazi anategemea waalimu wataruka sehemu ya mada bila kuzifundisha kwa kuwa ilikuwa zifundishwe mwezi wa nne na wa tano.
Kwa mantiki hiyo haitegemewi mzazi kudhani kuwa hatadaiwa kulipa ada Yote.