Uchaguzi 2020 Hakuna Mbunge CHADEMA anayeweza kushauri kugomea uchaguzi mkuu 2020

Ndugu zangu,

Ikitokea mtu awe kiongozi au mwana-CHADEMA akamshauri Mbowe na wabunge wake wagomee uchaguzi mkuu 2020 ajiandae kufukuzwa au watagawana mbao na kukizika chama.

Siasa ni ajira na wengi ni wachumia tumbo sasa itakapotokea eti mtu kwa mfano anamshauri Lema au Mbowe kutogombea ubunge mwaka 2020 ajiandae kuitwa msaliti. Uongozi wa Chadema umeamua kuweka mpira kwapani kwa sababi hakuna mtu kwenye kamati kuu ambaye ni mgombea hivyobasi wajumbe wa KK na wabunge hawana maslahi binasfi na uchaguzi huu.

Nimalize tu kwa kusema kuwashauri Mbowe na wabunge wengine Chadema kugomea uchaguzi mkuu 2020 ni sawa na ''kumnyang'anya tonge mwenye njaa'' ama zako ama zao.

Ukweli huchukiwa lakini lazima usemwe.
tatizo ni wananchi hawataenda kupiga kura kama tume haitakuwa huru so wagombea wa upinzani watagombea hatuendi kupoteza muda kupiga kura wakati tunajua hatushindi
 
Back
Top Bottom