Hakuna kanuni ya kufanikiwa, ni mipango yako tu

Requal

JF-Expert Member
Jun 5, 2020
1,025
1,905
Aisee vijana wenzangu

Unajua watu tunashindwa kuelewa uvivu ni nini in such au tunajitia kutokuelewa?

Kuna uvivu wa kutenda (kufanya kazi kwa vitendo na ule uvivu wa kufikiri sasa ndugu yangu wewe endelea kusema mwenzio mvivu kutwa kushinda hapa JamiiForums, wakati yawezekana mwenzio ni mvivu wa kutenda haonyeshi kujishughulisha tu

Lakini kumbe mwenzio genius wa kufikiria na kupanga karata zake kichwani anashinda analala ,yuko mtandaoni 24/7hrs, anakula bata na ana mingle kila kijiwe na life linatembea kwa reli kama mtoto wa chifu huwezi jua hatufanani.

Ukiwa nyuma ya keyboard epuka kuona wenzako maskini, kisa unawaona hapa kwa kila comment..ohoooo

Narudia,usiige mtu hatufanani fuata njia yako. Utakufa unalaumu kama mfuasi wa kibwetele

Shauri yako.
 
Wengine kazi zao zinawaruhusu kukaa humu off akiwa anakula tu na akilala tu.
 
Wengine humu wapo 24/7 wanakomenti uharo kumbe wapo kwenye payroll za buku 7 FC a.k.a Mataga.
Ngoja sisi wazee wa Koromije tupambane wanetu wasije kukosa kwenda chooni.
 
Ipo sahihi mafanikio hayaji kwa kuonekana unafanya kazi, kila mtu aliye Duniani anafanya na atafanya kazi hata Mzee unayemuona hana maendeleo leo sio kwamba hakufanya kazi.

Naamini Success ni akiri kubwa ya kuweka malengo, Plans na Deadline na Focus...mtu wa aina hiyo hata akilala ndani mwezi mzima afanyi kazi huku kuna kijana mwengine masaa 24 anafanya kazi nita-beti kwa aliyelala.
 
Ipo sahihi mafanikio hayaji kwa kuonekana unafanya kazi, kila mtu aliye Duniani anafanya na atafanya kazi hata Mzee unayemuona hana maendeleo leo sio kwamba hakufanya kazi.

Naamini Success ni akiri kubwa ya kuweka malengo, Plans na Deadline na Focus...mtu wa aina hiyo hata akilala ndani mwezi mzima afanyi kazi huku kuna kijana mwengine masaa 24 anafanya kazi nita-beti kwa aliyelala.
Umenikumbusha shule kuna kijamaa prepo ya usiku haingii kazi yake ni kulala tu yaan ukitaka kumpata iwe usiku au mchana we zungukia vitandani utamkuta kalala cha kushangaza kila mitihani ukija katusua kuzidi hata wanaokesha kusoma, Sasa wewe jifanye kumgeza uone. ila nilikuja kugundua jamaa ni mtu wa mipango sana na sio kwamba hasomi kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom