Hakuna jambo baya kama kuhisi umeathirika na unaogopa kwenda kupima

Kipenseli

JF-Expert Member
Feb 9, 2020
800
1,050
Usiombe hii kitu uwe nayo kwenye mawazo yako na sana sana uwe unaingia kwenye platform mbalimbali kusoma dalili za huo ugonjwa (VVU na UKIMWI) au tabia zake baada ya kuambukizwa na ukawa una shaka juu ya hizo dalili.

Binafsi niliwahi kudumbukia kwenye haya mawazo (hata ukipitia thread zangu za kitambo utagundua hiko kitu)

Matokeo yake nilipata vidonda vya tumbo na kukonda sana na niliamini kweli nimeupata.

Lakini nilichogundua ni kwamba yale mawazo yalikuwa ni source ya mimi kupata vidonda vya tumbo na kukonda. Nikaacha hayo mawazo en nowdays nanenepa tu despite sikuenda kupima na niko na msimamo wa kutokwenda kupima.

Ushauri Wangu Kwa Vijana Wenzangu: 1. Tutake Risk huu ugonjwa upo jamani

2. Hakuna kitu kibaya cha kukiogopa kama uoga wenyewe

Am done unaweza kuongezea
 
Kama unafurahia kunenepa kwako, ukienda kupima utanenepa zaidi na utakuwa na amani kuliko ulivyo sasa
 
Umenikumbusha mbaliii, hata Mimi kuna kipindi Fulani miaka ya nyuma kidogo kabla sijawa mama, nilikuwaga na boy friend baada ya kuachana naye nikasikiaga wanamsema eti ana ngoma bwana, hiyo hali ilinitesaa sanaaa Kwa muda mrefu, halafu kupima nikiwa naogopa, kweli kidogo niwe chizi sababu ya mawazo, ikatokea tu siku moja najisikia vibayaaa, nikaenda hospital, Dkt akanichukua vipimo vingi vingi kumbe alichukua na cha HIV ila hakuniambia,

Majibu yalivyokuja akawa ananisomea sikuwa na wazo kabisa kama atakuwa amepima na HIV, basi akanisomea kisha akasema tumepima pia na HIV huna, weuweeee,nilitamani nimrukieee Kwa furahaaa, baada ya hapo nikapona kabisa hata sikuendelea kuumwa, jamani kumbe stress ni mbaya aisee inatesaa maana nilikuwa naumwa vitu havieleweki na nilipima vipimo vingii hawakuona ugonjwa wowote. Cha ajabu baada ya Majibu hayo nikawa nimepona kabisaaa ,na nikawa nimejijengea utaratibu wa kupima kila wakati...Yule Dr aliniokoa bana.
 
umenikumbusha mbaliii,hata Mimi kuna kipindi Fulani miaka ya nyuma kidogo kabla sijawa mama, nilikuwaga na boy friend baada ya kuachana naye nikasikiaga wanamsema eti ana ngoma bwana,hiyo hali ilinitesaa sanaaa Kwa muda mrefu,halafu kupima nikiwa naogopa,kweli kidogo niwe chizi sababu ya mawazo,ikatokea tu siku moja najisikia vibayaaa,nikaenda hospital,Dkt akanichukua vipimo vingi vingi kumbe alichukua na cha HIV ila hakuniambia,Majibu yalivyokuja akawa ananisomea sikuwa na wazo kabisa kama atakuwa amepima na HIV, basi akanisomea kisha akasema tumepima pia na HIV huna,weuweeee,nilitamani nimrukieee Kwa furahaaa,baada ya hapo nikapona kabisa hata sikuendelea kuumwa,jamani kumbe stress ni mbaya aisee inatesaa maana nilikuwa naumwa vitu havieleweki, na nilipima vipimo vingii hawakuona ugonjwa wowote.Cha ajabu baada ya Majibu hayo nikawa nimepona kabisaaa ,nanikawa nimejijengea utaratibu wa ku pima kila wakati...Yule Dr aliniokoa bana.
Asee story zetu zinafanana kidogo mdada....Mi pia nilipita kwa mschana mmoja ambae huko mtaani kwao anasifika vibaya na nilienda bila kinga
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom