Hakuna dawa za hospitali zinazoweza kutibu tatizo la nguvu za kiume?

MBUTAIYO

JF-Expert Member
Nov 15, 2010
681
391
Habari wana taaluma,
Heri ya mwaka mpya. Kuna ndugu yangu ana tatizo ambalo ameshughulika nalo kupitia tiba mbadala lakini mafanikio bado. Ni kwamba hapati hamu ya kufanya tendo la ndoa, ingawaje uume una weza kudinda vizuri.

Tiba mbadala walimpima na vipimo vyao wakamwambia tatizo ni hormone iitwayo testrosterone (kama sijakosea) ambayo iko chini. Amepewa dawa dose mara tatu, lakini tatizo liko palepale.

Nauliza kwamba, kama ni kweli tatizo ndio hilo, je, hakuna dawa za hospital zinazoweza kutibu tatizo hilo?
 
Katika bodybuilding hua testosterone inahitajika sana hivyo kuna vyakula hua vinachochea uzalishwaji wake ambavyo hua vinatumika sana.
Mfano vyakula vyote kutokea baharini pweza, samaki, papa na supu zake.

Mbegu za maboga, mboga nyingi za majani.

Ila kwenye bodybuilding hua wanatumia supplement ya kuongezea testosterone ninayoijua inaitwa vitrix.
 
Mkuu huyo ndugu yako mwambie ajitahidi kufuata yafuatayo mambo yatakuwa safi
1.Aache kabisa kupiga punyeto
2.Apate lishe bora ya vyakula vya asili
3.Ajitahidi kula mchanganyiko wa matunda kwa wingi
4.Anye maji mengi kila siku
5.Afanye mazoezi

Hapo kwenye red tafadhali sio kwa ubaya narekebisha tuu, ni Anywe!!!
 
Habari wana taaluma,
Heri ya mwaka mpya.
Kuna ndugu yangu ana tatizo ambalo ameshughulika nalo kupitia tiba mbadala lakini mafanikio bado.
Ni kwamba hapati hamu ya kufanya tendo la ndoa, ingawaje uume una weza kudinda vizuri.
Tiba mbadala walimpima na vipimo vyao wakamwambia tatizo ni hormone iitwayo testrosterone (kama sijakosea) ambayo iko chini. Amepewa dawa dose mara tatu, lakini tatizo liko palepale.
Nauliza kwamba, kama ni kweli tatizo ndio hilo, je, hakuna dawa za hospital zinazoweza kutibu tatizo hilo?

HILI TATIZO HALINA TIBA YA MOJA KWA MOJA au ya UHAKIKA (iwe HOSPT wala TIBA MBADALA) uwe makini sana wengi ni kukutafunia pesa tu ni ushauri wangu tu
 
Ukisema ni wewe kuna Tatizo ?
Hakuna tatizo mkuu,
Huyo ni ndugu yangu, hata mimi nimeshamsaidia kwa namna moja au nyingine lkn bado, ndo maana nimeleta huku kwenye wengi tusaidiane.
Huwezi kuficha ugonjwa.
 
Mkuu huyo ndugu yako mwambie ajitahidi kufuata yafuatayo mambo yatakuwa safi
1.Aache kabisa kupiga punyeto
2.Apate lishe bora ya vyakula vya asili
3.Ajitahidi kula mchanganyiko wa matunda kwa wingi
4.Anywe maji mengi kila siku
5.Afanye mazoezi
Asante mkuu kwa ushauri,
Naona hayo ni mambo ya msingi kabisa!
 
Katika bodybuilding hua testosterone inahitajika sana hivyo kuna vyakula hua vinachochea uzalishwaji wake ambavyo hua vinatumika sana.
Mfano vyakula vyote kutokea baharini pweza, samaki, papa na supu zake.

Mbegu za maboga, mboga nyingi za majani.

Ila kwenye bodybuilding hua wanatumia supplement ya kuongezea testosterone ninayoijua inaitwa vitrix.
Asante mkuu,,
 
Back
Top Bottom