Hakuna dawa ya mitishamba ya kutibu pressure?

Mparee2

JF-Expert Member
Sep 2, 2012
2,572
4,245
Kuna rafiki yangu anaumri wa zaidi kidogo ya mika 30 amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa pressure ya kupanda kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

Amepata matibabu ya kila aina mahospitalini ambapo yote yamekuwa ni kupunguza tu kwa muda. Amejaribu pia miti shamba kidogo ila hajapata mtaalam sahihi wa kutibu na sio kupunguza.

Hivi hapa Tanzania hakuna wataalamu wa miti shamba wanaweza kutibu pressure ikapona kabisa?

Najua wengi wanaweza kupunguza makali ila hapa naongelea kutibu ipone kabisa
 
Pressure inatengenezwa jikoni kwako pia inatibika jikoni kwako (kupitia aina ya vyakula unavyokula)

mtu una pressure unakula ngano nafaka, unakunywa chai yenye sukari, unakunywa soda hiyo pressure utakufa nayo tu ila ukizingatia vyakula unavyokula pressure utaisikia tu kwenye magazeti na radio.
 
Pressure inatengenezwa jikoni kwako pia inatibika jikoni kwako (kupitia aina ya vyakula unavyokula)

mtu una pressure unakula ngano nafaka, unakunywa chai yenye sukari, unakunywa soda hiyo pressure utakufa nayo tu ila ukizingatia vyakula unavyokula pressure utaisikia tu kwenye magazeti na radio.
hayo ni mawazo yale yale ya kimagharibi
Hapo unatumia sababu moja kati ya 7 kutoa suluhisho kitu ambacho sio sahihi
 
hayo ni mawazo yale yale ya kimagharibi
Hapo unatumia sababu moja kati ya 7 kutoa suluhisho kitu ambacho sio sahihi
Sio lazima kiwe sahihi kwako lakini kinaweza kua sahihi kwa mwingine ninao ushuhuda wa watu waliopona bila kutumia dawa yoyote ile walipata tiba jikoni mwao tu
 
Kuna rafiki yangu anaumri wa zaidi kidogo ya mika 30 amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa pressure ya kupanda kwa zaidi ya miaka miwili sasa.
Amepata matibabu ya kila aina mahospitalini ambapo yote yamekuwa ni kupunguza tu kwa muda. Amejaribu pia miti shamba kidogo ila hajapata mtaalam sahihi wa kutibu na sio kupunguza
Hivi hapa Tanzania hakuna wataalamu wa miti shamba wanaweza kutibu pressure ikapona kabisa?
Najua wengi wanaweza kupunguza makali ila hapa naongelea kutibu ipone kabisa
Fanya test mkuu ajizuie kula vyakula vya sukari na wanga hata ndani ya mwezi mmoja Kama hataona mabadiliko aendelee na utaratibu wake wa kula kama kawaida
 
Dawa hii hapa/ lifestyle audit /fanya mazoezi punguza wanga ongeza mboga za majani au kwa kifupi ale kwa wingi vyakula vyenye nyuzi nyuzi (ufumwele) blood thinner foods.....
 
Fanya test mkuu ajizuie kula vyakula vya sukari na wanga hata ndani ya mwezi mmoja Kama hataona mabadiliko aendelee na utaratibu wake wa kula kama kawaida
Asante kiongozi; ila amekuwa kwa strict diet for more than 3months imemsaidia kiasi ila bado anatumia dawa
Baada ya kutumia muda wa kusoma na kutafiti nafikiri kwa sasa naielewa pressure kuliko ushauri wa kawaida ninaoweza kupata ndio sababu namsaidia kutafuta dawa...
 
Yote tunaweza kushauri lakini kila tatizo lina undani wake kunawakati mama watoto aliugua hospitali wakasema tatizo ni huo ugonjwa akipewa dawa hali inazidi nikaenda lugalo wakasema hivohivo nikaona nijaribu miti akapona kikubwa nashukuru alipona ila sijui kama nitatizo hilo la presha au la
 
Yote tunaweza kushauri lakini kila tatizo lina undani wake kunawakati mama watoto aliugua hospitali wakasema tatizo ni huo ugonjwa akipewa dawa hali inazidi nikaenda lugalo wakasema hivohivo nikaona nijaribu miti akapona kikubwa nashukuru alipona ila sijui kama nitatizo hilo la presha au la
unamaanisha huna hakika kama mkeo alikuwa na ugonjwa wa Presha au kama alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa mwingine?
Alikuwa mjamzito?
 
Maombi siku 3! Presha kwisha habari yake!

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Kuna rafiki yangu anaumri wa zaidi kidogo ya mika 30 amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa pressure ya kupanda kwa zaidi ya miaka miwili sasa.
Amepata matibabu ya kila aina mahospitalini ambapo yote yamekuwa ni kupunguza tu kwa muda. Amejaribu pia miti shamba kidogo ila hajapata mtaalam sahihi wa kutibu na sio kupunguza
Hivi hapa Tanzania hakuna wataalamu wa miti shamba wanaweza kutibu pressure ikapona kabisa?
Najua wengi wanaweza kupunguza makali ila hapa naongelea kutibu ipone kabisa
Nakuomba uni PM tusaidiane mkuu
 
unamaanisha huna hakika kama mkeo alikuwa na ugonjwa wa Presha au kama alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa mwingine?
Alikuwa mjamzito?
Hakuwa mjamzito hospitali walisema ana presh lakini kwenye mitishamba wakasema sio presh ndomana nikasema sijui msingi watatizo kikubwa nashukuru alipona kwahiyo hapo nikisema amepona presha kwamitishamba nawezanikawa muongo maana sikurudi hospitali kupima tena
 
Pressure inatengenezwa jikoni kwako pia inatibika jikoni kwako (kupitia aina ya vyakula unavyokula)

mtu una pressure unakula ngano nafaka, unakunywa chai yenye sukari, unakunywa soda hiyo pressure utakufa nayo tu ila ukizingatia vyakula unavyokula pressure utaisikia tu kwenye magazeti na radio.
Kama alishaanza doze ya pressure itakuaje? Mtoa mada kauliza kama kuna tiba mbadala kwa tatizo lile. Suala la jikoni ni maboresho tu.
 
Poleni. Sijui kama itamsaidia ila mimi imenisaidia sana.

**
Kitunguu swaum. Unaweza saga punje 4 na kipande kikubwa kiasi cha tangawizi, na kipande cha mdarasini weka kwenye maji lita moja; ichemshe ichemke sana then una Acha ipoe unachuja unaweka kwenye jag ya kioo yenye mfuniko uliobana husiopitisha hewa, weka kwenye fridge.
Kila siku asubuhi anakunywa kikombe kidogo cha chai anapasha moto kama ako na microwave dakika 3, kama ako na jiko la gas aangalie mpaka itokote, anaweka slice mbili za ndimu na asali mbichi kijiko kimoja cha kulia chakula.

Anakunywa as a morning routine kabla ya msosi na pia evenings after chakula ya usiku, relaxing time. (Mchana kama anaishi maeneo ya joto kali sana sio vizuri kutumia maana tangawizi inachemsha mwili!)

**
Ps; Aina ya Imani (sio dini) pia juu ya aina ya matibabu unayopata inasaidia sana.
 
Back
Top Bottom