Hakuna anayetukwamisha, ni ushindani wa biashara, kufaidika na keki ya dunia kunahitaji mbinu na weledi siyo siasa za kulaani majukwaani

matunge

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
442
426
Salaam,

Miaka yote tangu kupata uhuru, nchi za Africa, Tanzania ikiwemo, zimekuwa zikifanya siasa za kulaani nchi za magharibi zikiamini kuwa umasikini na matatizo ya nchi zao ni matokeo ya nchi za magharibi kuhodhi uchumi wa dunia.

Viongozi wa nchi na wanasiasa wa Africa mfano Julius Malema, Yoweri Museveni na hata Rais wetu wa Tanzania wamesikika wakilaani mbinu chafu zinazotumiwa na nchi tajiri zikiongozwa na USA kukwamisha maendeleo ya nchi zao.

Mimi naona njia wanayotumia kudai usawa siyo sahihi kwa sababu kinachotokea duniani ni ushindani wa kibiashara na uchumi na hivyo haiwezekani aliye juu kumuachia aliye chini kwa shinikizo na laana za kisiasa za majukwaani.

Uhuru wa bendera unaweza kupata kwa njia ya kulaani na kutoa matamko ya kisiasa majukwaani lakini sio ule wa kiuchumi na kibiashara.

Ili nchi masikini ziweze kunufaika na keki ya dunia tunapaswa kuwa na mikakati ya kimya kimya ya muda mrefu ambayo itahusisha kuwapatia elimu iliyo bora ya masuala ya kiuchumi na biashara ya dunia vijana wetu tukiwaandaa kuja kuwa washauri wa kiuchumi kwa mataifa yetu.

Pia mbinu nyingine yaweza kuwa kujifunza mbinu na mifumo inayotumiwa na mataifa ya magharibi kuendelea kuongoza dunia kwa undani zaidi.

Tunaweza kuchagua vijana wachache wakafanya utafiti wa sababu zinazowafanya wenzetu kuwa bora kila wakati na kila kitu kuanzia malezi ya watoto, uzalendo na uchapazi kazi.

LENGO LISIWE KUWAPITA WAZUNGU BALI WALAU NASI TUNUFAIKE NA KEKI YA DUNIA.

Wikiendi njema,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ili nchi masikini ziweze kunufaika na keki ya dunia tunapaswa kuwa na mikakati ya kimya kimya ya muda mrefu ambayo itahusisha kuwapatia elimu iliyo bora ya masuala ya kiuchumi na biashara ya dunia vijana wetu tukiwaandaa kuja kuwa washauri wa kiuchumi kwa mataifa yetu.

Na kumbuka elimu nayo ina mitaala ya huko huko Dunia ya kwanza.
 
Hakuna anayetukwamisha, ni ushindani wa biashara, kufaidika na keki ya dunia kunahitaji mbinu na weledi siyo siasa za kulaani majukwaani!
Kwakweli tumechoka na hizi 'excuses'!
.... mara oooh MABEBERU, kakaenda'kakarudi MABWANYENYEEE ...aaah, kama nyie mnachinja mabeberu yenu si muendelee tu kupeleka mbogoma na ndogosa zenu kwa jirani tu kupandisha wazee! 🤑🤑🤑🤑🤑
 
Huku kamasi zikimvuja kwa ukali wa pilipili kwenye msosi, jamaa alimuangalia mpishi huku machozi yakimlengalenga Kama mjusi kabanwa na mlango :
"Bwana mpishi, kwakweli leo umenikosha, na kama ikikupendeza tuongeze kofi lingine la bu'pilipili!"
🎃🎃🎃 😂😂 🤣🤣🤣🤣🤣🤣
NB: Kwetu, Mwamadako, mtu akisema umuongeze kofi la bu'pilipili anamaanisha uchote kiganja kizima kilichoshiba uzichochee kwenye mboga!
 
Huku kamasi zikimvuja kwa ukali wa pilipili kwenye msosi, jamaa alimuangalia mpishi huku machozi yakimlengalenga Kama mjusi kabanwa na mlango :
"Bwana mpishi, kwakweli leo umenikosha, na kama ikikupendeza tuongeze kofi lingine la bu'pilipili!"

NB: Kwetu, Mwamadako, mtu akisema umuongeze kofi la bu'pilipili anamaanisha uchote kiganja kizima kilichoshiba uzichochee kwenye mboga!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kufaidika na keki ya dunia kuna changamoto nyingi lakini angalau awamu ya tano inao wasaidizi wa Rais wenye kuifahamu vyema sana dunia na mahitaji yake.

Kero ni ule ukweli kwamba katika awamu karibu zote tatu kabla ya hii ya sasa kundi la wenye kutakiwa kuwa wazalendo ndio lilikuwa limejaa madalali wa kuiumiza nchi yao waliyozaliwa.

Sio vita ndogo, ukikaa pamoja na watu wenye ushawishi watakwambia ni kwa namna gani wanapambana na hao waliozoea kuimuza nchi ambayo Baba na Mama zao wamezaliwa!.

Hizi pesa zinazoitwa gawio la kwenda hazina katika awamu zilizopita ndizo zilizokuwa zinaishia juu kwa juu zikistawisha maslahi ya wenye vyeo na marafiki zao.

Kila mwenye kujiona mzalendo na awe wa kwanza kuumizwa kila anapoona watu wanataka kutajirika kirahisi tu huku walio wengi wakibakia malofa.
 
Salaam,

Miaka yote tangu kupata uhuru, nchi za Africa, Tanzania ikiwemo, zimekuwa zikifanya siasa za kulaani nchi za magharibi zikiamini kuwa umasikini na matatizo ya nchi zao ni matokeo ya nchi za magharibi kuhodhi uchumi wa dunia.

Viongozi wa nchi na wanasiasa wa Africa mfano Julius Malema, Yoweri Museveni na hata Rais wetu wa Tanzania wamesikika wakilaani mbinu chafu zinazotumiwa na nchi tajiri zikiongozwa na USA kukwamisha maendeleo ya nchi zao.

Mimi naona njia wanayotumia kudai usawa siyo sahihi kwa sababu kinachotokea duniani ni ushindani wa kibiashara na uchumi na hivyo haiwezekani aliye juu kumuachia aliye chini kwa shinikizo na laana za kisiasa za majukwaani.

Uhuru wa bendera unaweza kupata kwa njia ya kulaani na kutoa matamko ya kisiasa majukwaani lakini sio ule wa kiuchumi na kibiashara.

Ili nchi masikini ziweze kunufaika na keki ya dunia tunapaswa kuwa na mikakati ya kimya kimya ya muda mrefu ambayo itahusisha kuwapatia elimu iliyo bora ya masuala ya kiuchumi na biashara ya dunia vijana wetu tukiwaandaa kuja kuwa washauri wa kiuchumi kwa mataifa yetu.

Pia mbinu nyingine yaweza kuwa kujifunza mbinu na mifumo inayotumiwa na mataifa ya magharibi kuendelea kuongoza dunia kwa undani zaidi.

Tunaweza kuchagua vijana wachache wakafanya utafiti wa sababu zinazowafanya wenzetu kuwa bora kila wakati na kila kitu kuanzia malezi ya watoto, uzalendo na uchapazi kazi.

LENGO LISIWE KUWAPITA WAZUNGU BALI WALAU NASI TUNUFAIKE NA KEKI YA DUNIA.

Wikiendi njema,

Sent using Jamii Forums mobile app
Rais wangu WA majukwaani saizi ni muda wa kitembea na Pacha lako ili kupunguza stress za watu Tutahakikisha tunamjazia strategies za kuboresha maisha ya watanzania...





Saizi Maprinter tayari ndege ikitua Tu na dhana ya ujamaa itatumika ni Raha tupu kuanzia na serikali ya VIWANDA kufufua vyote Kwa fedha zetu wenyewe wenye viwanda vya stress watatujoin wenyewe..





Saizi ni kuchota hela (BOT/HAZINA) kila MTU alipwe laki 500000 Kwa mwezi fungua viwanda vyote vilivyokufa walipe Kodi na gawio KAZI imeisha pokea mishahara usifanye KAZI umetaka mwenyewe..



 
Back
Top Bottom