Hakuna aliyekosea?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,927
Miezi kadhaa huko nyuma niliandika makala isemayo "viongozi wasiokosea, na Taifa la wasiokasirika". Nilipoandika nilionesha mifano kadhaa ya jinsi gani viongozi wameboronga na hakuna aliyekubali makosa. Nilitumaini basi labda pole pole tunajifunza. Nikasema kuwa wananchi wasipoonesha kukasirishwa na vitendo vya watawala wao basi watawala huweza kufanya watakalo.

Sakata la Richmond ni ushahidi mwingine wa viongozi "wasiokosea". Nasikitika karibu mwezi sasa hakuna kiongozi hata mmoja aliyekubali kuwa amefanya makosa kuhusu Richmond. HAKUNA. Wote wanalaumu mtu mwingine na kukwepa kuwajibika na hata wale waliowajibika kwa kujiuzulu hawakukubali makosa yoyote yale.

Je nani alikosea? Naona baada ya watu kuisoma ripoti hii tunaweza kuwasaidia kuwaonesha ni nani alikosea.

a. Rais Jakaya Kikwete alikosea wapi au hakukusoea?
b. Waziri Mkuu Lowassa alikosea wapi au hakukusoea?
c. Waziri Ibrahim Msabaha alikosea wapi au hakukusea?
d. Waziri Nazir Karamagi alikosea wapi au hakukusoea?
e. Mkurugenzi wa TIC alikosea wapi au hakukusoea?
f. Usalama wa Taifa walikosea au hawakukosea?
g. Mwanasheria Mkuu alikosea au hakukosea?
h. BRELA walikosea wapi au wahakukosea?

Au inawezekana kabisa kuwa mkataba wa Richmond uliingiwa na baadaye kugundulika mapungufu yake na utapeli wake na hakuna mtu aliyekosea? Inawezekana kuwa ni kweli wote hawa wamesingiziwa na Kamati ya Mwakyembe na wameonewa tu.? Ni kwanini ni vigumu kukubali makosa na kuomba radhi? Je Kikwete atakuwa kiongozi wa kwanza kuomba msamaha Watanzania kwa makosa yake yeye mwenyewe au na yeye ataomba radhi kwa makosa ya "waliochini yake".? Au Rais naye huwa hakosei?

I don't know nimechanganyikiwa!!! hivi viongozi huwa wanakosea nisije kuwa nimeanza na wrong assumptions..
 
Chief Mwanakijiji,

Hii inawezekana kuwa kutokana na hulka yetu watu tusio kwenye madaraka kuwaona kuwa viongozi ni malaika na hawawezi kukosea kwani si binadamu. Hii ni unrealistic expectation. Lakini, pia ni jukumu la viongozi hawa kuonesha kuwa wao ni binadamu na wana majukumu makubwa waliokabidhiwa na wananchi kwani tunaamini kuwa hawatakuwa na makosa ya kijinga au makosa mengi kama watu wa kawaida. Hii ni sifa ya kiongozi, kuwa mfano kwa wengine.

Tatizo nilionalo ni kuwa viongozi wengi tulionao wana ubinafsi na kujifanya miungu-mtu. Kwa upande wa ubinafsi, viongozi hawa hawataki kukubali lawama na kutaka kila kinachoandikwa au kusemwa kuhusu wao, kiwe ni heko, shangwe na wasifu mzuri. Kwa upande wa umungu-mtu, wanasahau (na kuchangia kuwapotosha wananchi) kwa kujifanya kuwa hawafanyi makosa; iwe ni utendaji au hata mambo binafsi kama vile ufuska.

Katika suala hili la Richmond (na hata EPA), viongozi wetu, nasikitika kuwaambia (kama hawana taarifa hii) wameshindwa kuwajibika. Kuwajibika, ni pamoja na kukubali kuwa "Wandugu, japo jambo A,B,C na D lilifanywa kwa nia njema ya kunufaisha taifa, tulipotoka, hatukufanya uhakiki unaotakiwa na tulichemsha. Tunaomba mtuwie radhi, tunahakikisha kuwa kilichoharibika kinatengenezwa, baada ya miezi mitatu, tutawapa mrudisho nyuma wa kinachoendelea". Hali hii ingekuwa rahisi, muda na pesa zisingepotezwa, na mimi kama binadamu ningeelewa na kama mwananchi ningekuwa satisfied. Ukweli ni kwamba, tatizo la Richmond halikufanywa kwa nia njema ya kusaidia taifa. Ubinafsi, uroho, uchu wa kujitakia utajiri kwa mgongo wa Taifa ndivyo vitu vilivyopelekea kwa sakata lote hili.

Zaidi ya hapo, viongozi wetu, wakiongozwa na Waziri Mkuu mjiuzulu Lowassa, wamedhihirisha kuwa si wawajibikaji. Yaani Lowassa hata baada ya kujiuzulu ametoa sababu ambazo zimefanya hata kujiuzulu kwake kulikoonekana kuwa na maana kuwa ni bure kabisa. Lowassa baada ya kujiuzulu, ameishia kutupia lawama mawaziri wake badala ya kujihoji na kusema kuwa mimi kama Waziri Mkuu nilikuwa mtawala mbovu (assuming he is innocent in the whole deal as he claims). Hii pia tulioona wakati Meghji alipomruka Ballali na kusema alidanganywa na gavana mtenguliwa. Je, ni lini viongozi wetu wataacha kutupia lawama watu wengine na kukubali uongozi ikiwa ni pamoja na uwajibikaji? Ni mabilioni mangapi Tanzania itapoteza kabla ya kiongozi mmoja kukubali makosa?

Kukubali makosa si jambo baya kwani wote tu wanadamu. Tatizo ni pale mtu haoni kuwa amekosa na anang'ang'ania kujihusisha na uongozi wa nchi. Nafikiri hata Mh. Rais Kikwete angeimarisha nafasi yake ya urais na hata historia ya nchi yetu pale ambapo angetamka hadharani kuwa alifanya makosa kumwamini sana rafiki yake Lowassa. Rais alishaanza hili pale aliposema kuwa aliamini sana wasaidizi waliomghilibu na kumshurutisha amfukuze kazi mtumishi mmoja wa nchi wakati mtumishi huyo hakuwa na makosa bali ni wasaidizi wake ndio walikuwa wanajaribu kujikosha.

Chief Mwanakijiji, shukrani kwa topic nzuri na nina imani wanaJF watajitoa katika kuichangia. We seriously need to revisit the concept of responsibility (individual na collective), na jinsi inavyounda/chukua nafasi katika serikali yetu.
 
Hili ndilo swali; ndio maana hata bingwa wa kujitetea Bill Clinton alipobanwa na ushahidi wa gauni la Bluu alijikuta akisema "I'm sorry". Hata meya wetu hapa Detroit aliyekuwa na uhusiano wa kimapenzi uliothibitishwa na vi sms licha ya kukana kwenye kiapo cha mahakama na yeye alijikuta akisema "I'm sorry". Hata yule Seneta aliyejipongeza uwanja wa ndege na mwanamme mwenzie pamoja na kukataa kwake kuachia ngazi lakini alisema "I'm sorry".

Hivi hawa viongozi wetu sisi kwanini wanafikiri hawawezi kukosea?
 
Chief Ndorobo,

Naheshimu kuwa hii ni post yako ya kwanza lakini pengine ungetakiwa kujua kuwa Jambo Forums ni sehemu ya heshima. Japo tuna uhuru wa kuandika tunachopenda, matusi ya nguoni si jambo la busara kutumia na inaharibu reputation yetu. Kama jambo limekukuna sana jaribu kutumia tafsida!
 
Hili ndilo swali; ndio maana hata bingwa wa kujitetea Bill Clinton alipobanwa na ushahidi wa gauni la Bluu alijikuta akisema "I'm sorry". Hata meya wetu hapa Detroit aliyekuwa na uhusiano wa kimapenzi uliothibitishwa na vi sms licha ya kukana kwenye kiapo cha mahakama na yeye alijikuta akisema "I'm sorry". Hata yule Seneta aliyejipongeza uwanja wa ndege na mwanamme mwenzie pamoja na kukataa kwake kuachia ngazi lakini alisema "I'm sorry".

Hivi hawa viongozi wetu sisi kwanini wanafikiri hawawezi kukosea?

Mzee wa kijijini,

Kwa kweli watu kama Mh. Kwame ndio wanaume washoka kinamna. Umefanya kosa, umebambwa, kiri na watu watakusamehe. Inasemekana kuna uthibitisho wa utafiti uliofanywa huku Yu Es Ei ambapo wananchi walikuwa radhi kusamehe na kusahau pale mlengwa atakapokiri.

Mfano ni kwa marais wao...Clinton alipobanwa kwenye kona na ushahidi, alikiri, akaaibika na watu wakaendelea. Leo hii ni mmoja wa marais popular baada ya Kennedy na Reagan. Kwa upande mwingine, Mh. Bush alikataa kukubali kuwa kwenda Iraq ilikuwa ni makosa na akajipigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza kwa ile hotuba iliyopambwa na bango lisemalo "Mission Accomplished". Matokeo yake? Mpaka leo hakuna plan hata moja iliyofaa, pesa zimepotea isivyostahili na anabakia kuwa very unpopular.

Natumaini Rais Kikwete na wengineo hawaangalii haya kama maigizo tu, bali wanajifunza. Ningependa Rais Kikwete atamke kitu kama "Najuta kwa nini sikumfukuza kazi Edward/Nazir/Msabaha"
 
MMM na wachangiaji wenzangu, angalia mistari hii:

"Kosa sio kosa, kosa ni kurudia kosa"

"We goofed up...."

Haya zote zimo kwenye threds humu ndani ni maneno yaliyosemwa....

Na Morani anasema "It wasn't Me"
 
Ndorobo ,asijekuwa wale wale waliosema kuwa hapa JF kuna matusi na inatoa lugha za matusi ...mods watch out this please.

Viongozi wetu huwa hawakosei ,ndio maana Afrika ikawa inaongozwa na machifu na wafalme ,kwani ukishazaliwa kwenye ukoo huo basi wewe ni mtu usiyejua kukosea wala kuomba radhi.......
 
..watu wakiwa na kawaida ya kukosea,hata wakosee mara ngapi hawataona wamekosea! ni kama uzinzi! wengi tunatenda na hatuoni tunakosea!
 
DsL, hivyo tusipoona kuwa tumekosea ndio maana tunaamini kuwa hatujakosea hata kama makosa yetu yanatukodolea macho na kuita "mimi mimi"?
 
Mheshimiwa Mpanda Merikebu,
Asante sana kwa ushauri hasira zinazidi ukereketwa siku zote nimekuwa msomaji jana nimeamua na mimi nijitose kutoa michango yangu.
Thanks
 
Na imani,wahusika wakuu wanapita hapa na kupata mawazo haya safi. Hata lowasa anadai hakukosea bali watendaji wake wa chini ndiyo walikosea na hivyo anawajibika kwa kile alichodai ni "collective responsibility". Ni kawaida kwa viongozi wetu huwa hawakosei,hasa kule ndani ya chama tawala,watu huwa hawakosei,lakini swali ni kwamba mbona kulindana kwingi kama hakuna kukosea,eti mkubwa hakosei.
 
Miezi kadhaa huko nyuma niliandika makala isemayo "viongozi wasiokosea, na Taifa la wasiokasirika". Nilipoandika nilionesha mifano kadhaa ya jinsi gani viongozi wameboronga na hakuna aliyekubali makosa. Nilitumaini basi labda pole pole tunajifunza. Nikasema kuwa wananchi wasipoonesha kukasirishwa na vitendo vya watawala wao basi watawala huweza kufanya watakalo.

Sakata la Richmond ni ushahidi mwingine wa viongozi "wasiokosea". Nasikitika karibu mwezi sasa hakuna kiongozi hata mmoja aliyekubali kuwa amefanya makosa kuhusu Richmond. HAKUNA. Wote wanalaumu mtu mwingine na kukwepa kuwajibika na hata wale waliowajibika kwa kujiuzulu hawakukubali makosa yoyote yale.

Je nani alikosea? Naona baada ya watu kuisoma ripoti hii tunaweza kuwasaidia kuwaonesha ni nani alikosea.

a. Rais Jakaya Kikwete alikosea wapi au hakukusoea?
b. Waziri Mkuu Lowassa alikosea wapi au hakukusoea?
c. Waziri Ibrahim Msabaha alikosea wapi au hakukusea?
d. Waziri Nazir Karamagi alikosea wapi au hakukusoea?
e. Mkurugenzi wa TIC alikosea wapi au hakukusoea?
f. Usalama wa Taifa walikosea au hawakukosea?
g. Mwanasheria Mkuu alikosea au hakukosea?
h. BRELA walikosea wapi au wahakukosea?

Au inawezekana kabisa kuwa mkataba wa Richmond uliingiwa na baadaye kugundulika mapungufu yake na utapeli wake na hakuna mtu aliyekosea? Inawezekana kuwa ni kweli wote hawa wamesingiziwa na Kamati ya Mwakyembe na wameonewa tu.? Ni kwanini ni vigumu kukubali makosa na kuomba radhi? Je Kikwete atakuwa kiongozi wa kwanza kuomba msamaha Watanzania kwa makosa yake yeye mwenyewe au na yeye ataomba radhi kwa makosa ya "waliochini yake".? Au Rais naye huwa hakosei?

I don't know nimechanganyikiwa!!! hivi viongozi huwa wanakosea nisije kuwa nimeanza na wrong assumptions..

Mkuu hapa naona umemsahau TAKUKURU Edward Hosea!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom