pingli-nywee
JF-Expert Member
- Sep 16, 2015
- 11,923
- 13,344
https://www.nation.co.ke/news/Kiamb...d-from-office/1056-5215838-15s680a/index.html Gavana wa Gatuzi la Kiambu Ferdinand Waititu, almaarufu kama Baba Yao, ambaye alitoweka baada ya kusikia kwamba anasakwa kwa tuhuma za ufisadi leo hii amefikishwa mbele ya hakimu kwa 'bail hearing'. Wakili wake walipata afueni baada ya hakimu Lawrence Mugambi kukubali kumpa bail(15million) ila wakapigwa na butwaa baada ya kusikia masharti ya hakimu. Hakimu amemuagiza gavana Waititu, na afisa wengine wa serikali ya gatuzi la Kiambu, kutofika kwenye ofisi zao. Akisema hatua hiyo itahakikisha kwamba kesi yenyewe itabaki kuwa ya uwazi na ya heshima inayostahili. Hukumu hii ilikuwa kiendelezo cha hukumu ya hakimu mwingine, kwenye kesi nyingine tofauti. Hakimu Mumbi Ngugi ambaye alizua gumzo hivi majuzi baada ya kutoa hukumu ambayo itawasimamisha kazi kwa muda viongozi kama magavana ambao ni watuhumiwa kwenye kesi za ufisadi.