naggy
Member
- Apr 27, 2011
- 97
- 152
kama mwalimu, ninaeipenda kazi yangu, nimesikitishwa na tamko la serikali bungeni hivi leo kupitia waziri wa utumishi wa umma-Hawa Ghasiah, akijibu swali la mbunge aliyetaka kujuwa kwa nini serikali inatoa viwango vya mshahara kwa upendeleo. Waziri huyu amekanusha na kusema kwamba serikali inatumia vigezo vitano vya kimataifa kufikia uamuzi wa kada ipi ipewe viwango vipi vya mishahara. Baadhi ya vigezo hivyo ni ugumu wa kazi, muda wa kutumia kusomea hiyo kazi,mazingira ya kufanyia kazi na umuhim wa kazi yenyewe kwenye jamii. Kama nitakuwa nimevikosea wanajamvi mtanirekebisha.
Kwa upande wangu, naungana na huyo mbunge aliyetoa mfano wa madaktari na walimu kwamba madaktari wanapendelewa richa ya kutumia vigezo hivyo vya kimataifa. Haiingii akilini mshahara wa mwalimu graduate anyeanza kazi uwe laki nne na sitini elfu hivi (469000) wakati wa daktari graduate ni laki tisa na usheee, yaani mara mbili na robo ya ule wa mwalimu!!!!!!!!!!!!!. HAPANA, hii siyo haki. Ni sawa, kazi ya udaktari inaweza kuwa ngumu na masomo yake ni magumu, yanachukua muda mrefu. Lakini sio kwa kiasi cha mara mbili ya uwalimu! Serikali itasemaje pia kuhusu ma T.A. yaani tutorial assistances wanaomaliza degree ya kwanza na kuajiriwa vyuo vikuu? Hawa TAs wanalipwa mshahara (take home) kwenye LAKI TISA hivi, sawa na madaktari wanaoanza. Je, na wao kazi yao ni ya muhim sana katika jamii sawa na madaktari? TAs wanakazi gani kubwa inayomzidi mwalim aliyeko shuleya kata tena vijijini, kwa jamii isiyopenda elimu kama wasukuma? Tutorial assistances nao ni walim kama hawa graduates walioko shule za kata. HUU SIO UPENDELEO? Hakika ni upendeleo.
NAFIKIRI TUKIGOMA KWA WIKI MOJA HIVI, SERIKALI ITAONA UMUHIM WETU. Najuwa tutaathiri walipa kodi maskini wanaosomesha watotowao shule za serikali na sio haowanao enjoy national cake ya taifa hili. Watatusamehe kwa muda, tunawapenda sana na ndio maana tunavumilia kwa ujira mdogo kiasi hiki. There is NO OTHER CHOICE!
Kwa upande wangu, naungana na huyo mbunge aliyetoa mfano wa madaktari na walimu kwamba madaktari wanapendelewa richa ya kutumia vigezo hivyo vya kimataifa. Haiingii akilini mshahara wa mwalimu graduate anyeanza kazi uwe laki nne na sitini elfu hivi (469000) wakati wa daktari graduate ni laki tisa na usheee, yaani mara mbili na robo ya ule wa mwalimu!!!!!!!!!!!!!. HAPANA, hii siyo haki. Ni sawa, kazi ya udaktari inaweza kuwa ngumu na masomo yake ni magumu, yanachukua muda mrefu. Lakini sio kwa kiasi cha mara mbili ya uwalimu! Serikali itasemaje pia kuhusu ma T.A. yaani tutorial assistances wanaomaliza degree ya kwanza na kuajiriwa vyuo vikuu? Hawa TAs wanalipwa mshahara (take home) kwenye LAKI TISA hivi, sawa na madaktari wanaoanza. Je, na wao kazi yao ni ya muhim sana katika jamii sawa na madaktari? TAs wanakazi gani kubwa inayomzidi mwalim aliyeko shuleya kata tena vijijini, kwa jamii isiyopenda elimu kama wasukuma? Tutorial assistances nao ni walim kama hawa graduates walioko shule za kata. HUU SIO UPENDELEO? Hakika ni upendeleo.
NAFIKIRI TUKIGOMA KWA WIKI MOJA HIVI, SERIKALI ITAONA UMUHIM WETU. Najuwa tutaathiri walipa kodi maskini wanaosomesha watotowao shule za serikali na sio haowanao enjoy national cake ya taifa hili. Watatusamehe kwa muda, tunawapenda sana na ndio maana tunavumilia kwa ujira mdogo kiasi hiki. There is NO OTHER CHOICE!