Hakika walimu wote ni wakati wetu wa kugoma kuishinikiza serikali kutambua umuhimu wetu

naggy

Member
Apr 27, 2011
97
152
kama mwalimu, ninaeipenda kazi yangu, nimesikitishwa na tamko la serikali bungeni hivi leo kupitia waziri wa utumishi wa umma-Hawa Ghasiah, akijibu swali la mbunge aliyetaka kujuwa kwa nini serikali inatoa viwango vya mshahara kwa upendeleo. Waziri huyu amekanusha na kusema kwamba serikali inatumia vigezo vitano vya kimataifa kufikia uamuzi wa kada ipi ipewe viwango vipi vya mishahara. Baadhi ya vigezo hivyo ni ugumu wa kazi, muda wa kutumia kusomea hiyo kazi,mazingira ya kufanyia kazi na umuhim wa kazi yenyewe kwenye jamii. Kama nitakuwa nimevikosea wanajamvi mtanirekebisha.

Kwa upande wangu, naungana na huyo mbunge aliyetoa mfano wa madaktari na walimu kwamba madaktari wanapendelewa richa ya kutumia vigezo hivyo vya kimataifa. Haiingii akilini mshahara wa mwalimu graduate anyeanza kazi uwe laki nne na sitini elfu hivi (469000) wakati wa daktari graduate ni laki tisa na usheee, yaani mara mbili na robo ya ule wa mwalimu!!!!!!!!!!!!!. HAPANA, hii siyo haki. Ni sawa, kazi ya udaktari inaweza kuwa ngumu na masomo yake ni magumu, yanachukua muda mrefu. Lakini sio kwa kiasi cha mara mbili ya uwalimu! Serikali itasemaje pia kuhusu ma T.A. yaani tutorial assistances wanaomaliza degree ya kwanza na kuajiriwa vyuo vikuu? Hawa TAs wanalipwa mshahara (take home) kwenye LAKI TISA hivi, sawa na madaktari wanaoanza. Je, na wao kazi yao ni ya muhim sana katika jamii sawa na madaktari? TAs wanakazi gani kubwa inayomzidi mwalim aliyeko shuleya kata tena vijijini, kwa jamii isiyopenda elimu kama wasukuma? Tutorial assistances nao ni walim kama hawa graduates walioko shule za kata. HUU SIO UPENDELEO? Hakika ni upendeleo.

NAFIKIRI TUKIGOMA KWA WIKI MOJA HIVI, SERIKALI ITAONA UMUHIM WETU. Najuwa tutaathiri walipa kodi maskini wanaosomesha watotowao shule za serikali na sio haowanao enjoy national cake ya taifa hili. Watatusamehe kwa muda, tunawapenda sana na ndio maana tunavumilia kwa ujira mdogo kiasi hiki. There is NO OTHER CHOICE!
 
Ndugu yangu usipoteze md kujadili issues za watu waliokata tamaa! ualimu ni kada ya watu wasiojitambua! okay wewe ungelipaje mtu aliyepata dvs four na kwenda ualimu? acha waendelee kukonda wakati kada nyingine wananawili. its difficult to liberate teachers! think big!
 
nikiburi na kudharau taaluma za watu sasa kwa majibu kama yale aliyo toa wazir(hawa ghasia).hii ni alama tosha inayoonesha ni kwa kiasi gan mwl. anadharaurika katika jamii.hatambui yeye mwenyewe pale bila ya huo msaada wa mwalimu angefika pale? ebo
inahudhunisha sana
 
Hata mimi naunga mkono walimu kulipwa kiduchu kwani ni kazi ambayo inafanywa na wahitimu ambao wamekosa kwa kwenda kwa sababu ya kufeli mitihani.kama unabisha chukua vyeti vya walimu kumi ghafla kama utaona yeyote aliyepata division I akiwa kidato cha IV au cha VI.Wazazi/walezi hushangaa wato wao wanaposhindwa mitihani na kuwauliza, Yaani mwanangu umefeli sana hadi huwezi kupata nafasi ya kwenda kusomea ualimu! Wewe unayetaka walimu wagome, uliona wapi mgomo wa wajinga ukafanikiwa?
 
Kimsingi siyo walimu wote wamefeli mfano TSa wangu hapa amepata uper second na yupo hapa na ninamuonea huruma mwalimu wa sekondari ila kwa upande mwingine nahisi Walimu wameanza kungoma kimya kimya kwa kuzalisha mambumbumbu ktk Taifa la Tanzania itafika sehemu hata hao wanaojiita wapo juu kama sisi hakuna tena
 
Nazani badala ya kusema ajira kwa vijana ni bomu la taifa tuseme UZALISHAJI WA MAMBUMBUMBU ni bomu hatari zaidi kwa taifa miaka michache ijayo!
 
Aliye leta híi ana mantiki sana kwa taarifa tu mgomo wa walimu upo kila siku na mathara yake ni ya muda mrefu km sasa kushuka kwa taaluma tz mara watoto wa secondary hawajui kusoma wala kuandika. Wewe unaesema wacha walipwe kidogo kuna ndugu yako ama mtoto wako atakumbwa na madhara ya huu mgomo baridi. Tana njia ndefu ya mabadiliko kupingana na walevi wa madaraka na ndugu zao na marafiki zao. Bora elimu ndio ilipo kwa sasa tz kwa wingi wa shule za kata na kuitwa mitambo ya kufyatua O.
 
Elimu ni ufunguo wa maisha ila nadhani maisha labda yamebadisha kufuli tumebaki na ufunguo tu bila sisi kujau. Ndio maana watu hapo juu wanachangia bila kufikiri na dharau kwa taaluma za watu. Bila huyo mwalimu ungekuwa unajua kuchangia hata huo ***** humu ndani.
 
Ndugu yangu usipoteze md kujadili issues za watu waliokata tamaa! ualimu ni kada ya watu wasiojitambua! okay wewe ungelipaje mtu aliyepata dvs four na kwenda ualimu? acha waendelee kukonda wakati kada nyingine wananawili. its difficult to liberate teachers! think big!
Ndiyo maana Baba wa Taifa aliacha ualimu na kuingia kwenye siasa kunakolipa!
 
Kazi ya kupanga mishahara ya watumishi ni ngumu sana na inahitaji umakini mkubwa. Na serikali ya tanzania haina umakini kwenye swala hili. mtoa maada umeeleza vizuri japokuwa kuna mahali unachanganya mambo, mfano issue ya tutorial assistant wa vyuo kulipwa takehome 900,000. Hapa hakuna tatizo pia naona hizo ni chache mno, nitakupa sababu moja ya msingi. Ili mtu awe tutorial asistant ni lazima afaulu kwa kiwango cha juu. Watu wengi wanaofaulu sana kwenye degree ya kwanza wanaajiriwa kwenye sector binafsi ambapo mishahara ni mikubwa ukilinganisha na hiyo 900,000 wanayopewa huko serikalini. Hivyo basi ukilipa pungufu ya hapo utakuwa unaua elimu ya vyuo vikuu nchini. Tena inasikitisha sana kuona professors analipwa around 4 million na PhD graduates wanapata around 2.5million. Ndio maana wengi wanakimbilia rwanda na hata botwasna ambapo mishahara ni mizuri zaidi. Nadhani ni vema wakaangalia mishara ya watumishi wote.
 
Mimi nimezalisha F 187,D 23 na C 14 kati ya watoto 224!mwaka huu sisemi ntawapa rekodi!tulishagoma kitambo.ccm janga
 
Ndiyo maana Baba wa Taifa aliacha ualimu na kuingia kwenye siasa kunakolipa!

hata mimi niliupiga chini baada ya kuona ni longolongo,nilikaa miez6 bila mshahara kisa hela wamepeleka kwenye uchaguzi wa mkweeeeree 2005,kufuatilia salary wizara ya elimu nakutana na mbeba mafaili naye ananizingua naye anataka nimyenyekee yaani nilikuta hata walimu wwakuu na mvi zao wanawanyenyekea watu wa masijala,kuja kupata faili ni baada ya siku tatu tena wamelipeleka kitengo cha watu wanaoomba uhamisho,wakati sijawahi kuomba na hata kwenye payroll sijaingia. From that day niliapa ni bora nikapige job nyingine tu na si ualimu,i did it 4 1yrs nikasepa.
 
kama mwalimu, ninaeipenda kazi yangu, nimesikitishwa na tamko la serikali bungeni hivi leo kupitia waziri wa utumishi wa umma-Hawa Ghasiah, akijibu swali la mbunge aliyetaka kujuwa kwa nini serikali inatoa viwango vya mshahara kwa upendeleo. Waziri huyu amekanusha na kusema kwamba serikali inatumia vigezo vitano vya kimataifa kufikia uamuzi wa kada ipi ipewe viwango vipi vya mishahara. Baadhi ya vigezo hivyo ni ugumu wa kazi, muda wa kutumia kusomea hiyo kazi,mazingira ya kufanyia kazi na umuhim wa kazi yenyewe kwenye jamii. Kama nitakuwa nimevikosea wanajamvi mtanirekebisha.

Kwa upande wangu, naungana na huyo mbunge aliyetoa mfano wa madaktari na walimu kwamba madaktari wanapendelewa richa ya kutumia vigezo hivyo vya kimataifa. Haiingii akilini mshahara wa mwalimu graduate anyeanza kazi uwe laki nne na sitini elfu hivi (469000) wakati wa daktari graduate ni laki tisa na usheee, yaani mara mbili na robo ya ule wa mwalimu!!!!!!!!!!!!!. HAPANA, hii siyo haki. Ni sawa, kazi ya udaktari inaweza kuwa ngumu na masomo yake ni magumu, yanachukua muda mrefu. Lakini sio kwa kiasi cha mara mbili ya uwalimu! Serikali itasemaje pia kuhusu ma T.A. yaani tutorial assistances wanaomaliza degree ya kwanza na kuajiriwa vyuo vikuu? Hawa TAs wanalipwa mshahara (take home) kwenye LAKI TISA hivi, sawa na madaktari wanaoanza. Je, na wao kazi yao ni ya muhim sana katika jamii sawa na madaktari? TAs wanakazi gani kubwa inayomzidi mwalim aliyeko shuleya kata tena vijijini, kwa jamii isiyopenda elimu kama wasukuma? Tutorial assistances nao ni walim kama hawa graduates walioko shule za kata. HUU SIO UPENDELEO? Hakika ni upendeleo.

NAFIKIRI TUKIGOMA KWA WIKI MOJA HIVI, SERIKALI ITAONA UMUHIM WETU. Najuwa tutaathiri walipa kodi maskini wanaosomesha watotowao shule za serikali na sio haowanao enjoy national cake ya taifa hili. Watatusamehe kwa muda, tunawapenda sana na ndio maana tunavumilia kwa ujira mdogo kiasi hiki. There is NO OTHER CHOICE!
walimu walimu walimu walimu! lini mtazitambua haki zenu? acheni kulala bana, acheni woga, fanyeni maamuzi magumu
 
...bado tu mnasomea ualimu, fani nyngne hamzioni? Au ndo kukimbilia ajira....aaa nanyi mmezidi ni hstry kiswahili tu mnafaida gani, kazn kwnyw hamtuliii...aaa sory piga chn magamba
 
Back
Top Bottom