Jamani naomba kushare kidogo nilichokikuta jana huko UKONGA.Nilikuta watu kama 40 ambao walikuwa wanafanya kazi ya kupiga tofali, hakika nilishangaa walivyokuwa wakijadili mambo ya siasa.Hakika kila mtu alikuwa amekata tamaa ya maisha kwa jinsi maisha yalivyokuwa magumu sasa hivi.Watu wote walieleza umuhimu wa kufanya marekebisho ya Katiba haraka iwezekanavyo ili Rais atakayechaguliwa atokane na wananchi.WALISEMA WAZIWAZI KAMA DR WILBROD SLAA HATAGOMBEA URAIS 2015 BASI HAWATAPIGA KURA KWANI NDIYE KIONGOZI PEKEE ANAYEFAA KUONGOZA NCHI HII...Nilivutiwa sana na mazungumzo yao lakini muda ulinitupa mkono nikaondoka.Nikajiuliza Slaa ana nini mbona kila kona anaungwa mkono??