Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,516
Mwaka 2008, wakati wa mjadala wa Ripoti Richmond Bungeni, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini na Mbunge wa Kibaha, Dr. Ibrahim Msabaha alijiuzulu pamoja na Waziri Mkuu wa wakati huo, Mzee Edward Ngoyai Lowassa.
Katika mchango wake juu ya Ripoti hiyo na kabla ya kuachia ngazi, Dr. Msabaha alisema, pamoja na mambo mengine, kuwa katika njia ya kuelekea kuwajibika yeye ni Chilongola. Kwa tafsiri yake kutoka lugha yake mama ya kizaramo, Chilongola ni muonyesha na muongoza njia. Ni kusema, Chilongola ni kiongozi.
Dr. Msabaha alikuwa Chilongola kwakuwa alikuwa Waziri wa kwanza kuwajibika kutokana na kadhia ya Richmond. Alikuwa muonyesha njia ili wengine wamfuate. Na ikawa hivyo. Msururu wa viongozi ulifuata kwa kujiuzulu au kuwajibishwa vinginevyo.
Kuhusu kujitoa kwa vyama vya upinzani kwenye Uchaguzi wa Serikali ya Mitaa, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman A. Mbowe ni Chilongola. Mara baada ya kutangaza kuwa CHADEMA haitashiriki uchaguzi huo, viongozi kadhaa wa vyama vingine vya upinzani walijitokeza na kutangaza kuwa vyama vyao vimejiondoa kwenye uchaguzi. Chilongola Mbowe akapata uungwaji mkono.
Hata enzi ya Bunge la Katiba, Mbowe alikuwa Chilongola kwa kutoka na kususia vikao vya Bunge hilo hadi kupelekea kuundwa kwa 'hayati' UKAWA. Hakika, Mbowe ni Chilongola. He deserves to be a long-term political target!
Katika mchango wake juu ya Ripoti hiyo na kabla ya kuachia ngazi, Dr. Msabaha alisema, pamoja na mambo mengine, kuwa katika njia ya kuelekea kuwajibika yeye ni Chilongola. Kwa tafsiri yake kutoka lugha yake mama ya kizaramo, Chilongola ni muonyesha na muongoza njia. Ni kusema, Chilongola ni kiongozi.
Dr. Msabaha alikuwa Chilongola kwakuwa alikuwa Waziri wa kwanza kuwajibika kutokana na kadhia ya Richmond. Alikuwa muonyesha njia ili wengine wamfuate. Na ikawa hivyo. Msururu wa viongozi ulifuata kwa kujiuzulu au kuwajibishwa vinginevyo.
Kuhusu kujitoa kwa vyama vya upinzani kwenye Uchaguzi wa Serikali ya Mitaa, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman A. Mbowe ni Chilongola. Mara baada ya kutangaza kuwa CHADEMA haitashiriki uchaguzi huo, viongozi kadhaa wa vyama vingine vya upinzani walijitokeza na kutangaza kuwa vyama vyao vimejiondoa kwenye uchaguzi. Chilongola Mbowe akapata uungwaji mkono.
Hata enzi ya Bunge la Katiba, Mbowe alikuwa Chilongola kwa kutoka na kususia vikao vya Bunge hilo hadi kupelekea kuundwa kwa 'hayati' UKAWA. Hakika, Mbowe ni Chilongola. He deserves to be a long-term political target!