MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Kisa hujuma: Yanga Kupumzisha nyota wake
.
🗣"Tutakuwa makini zaidi kwenye mechi yetu dhidi ya Mbeya Kwanza, tunajua mipango iliyopo, tutafanya hivi kujiweka katika nafasi salama kwa sababu tunahofia kupata kadi za njano na kupelekea baadhi ya nyota kuukosa mchezo dhidi ya Simba hapo Desemba 11, hili tumeshalifanyia kazi,"
.
"Tumebaini janja janja za wapinzani wetu kuwatafutia kadi za njano wachezaji wetu nyota, au kufanyiwa rafu za makusudi akiwamo, Khalid Aucho na wengine ili kushindwa kucheza mechi ijayo dhidi ya Simba,”
.
"Tumegundua na tunatarajia mechi yetu dhidi ya Mbeya Kwanza itakuwa na mabadiliko katika kikosi, baadhi ya nyota watapumzishwa kwa ajili ya kujiandaa na pambano letu dhidi ya Simba, tunawahakikishia mashabiki wetu tutarejea na pointi tatu kutoka kwa Mbeya Kwanza halafu Desemba 11, tabu iko pale pale dhidi ya Simba," amesema Hassan Bumbuli.
Taarifa: sportsarena_tz
Bumbuli nakuheshimu sana na kukubali mno kwa Kazi yako ya Uandishi wa Habari tokea ukiwa Mwananchi ila sijui zile Akili zako Kubwa ulizokuwa nazo ulipofika hapo Yanga SC ulipo zimetokomelea wapi.
Bumbuli leo kabisa Wewe ni wa kusema kuwa Simba SC inataka Kuwaumiza vibaya Wachezaji wenu Yanga SC na Kuwatafutia Kadi ili wakose Mechi yenu na wao Simba SC?
Bumbuli nani asiyejua kuwa Yanga SC mlikakaa Kikao ( tena ukiwemo ) pia pamoja na Mbunge Mmoja wa Dodoma na Waziri Mmoja wa Wizara Muhimu Tanzania huku mkipata Maagizo ya kutoka kwa Mstaafu namba 4 na Namba 2 wa sasa katika Serikali ya Rais Samia kuwa ili 'Kuwakomoa' Simba SC katika Msimu huu dawa ni Kuwaumizia tu Wachezaji wao maarufu na muhimu ili wawe na Majeruhi wengi?
Bumbuli binafsi kama KEROZENE nikuambie tu kuwa 90% ya Wachezaji wa Simba SC na Yanga SC ni Marafiki zangu na wapo Wachezaji Wawili wa Yanga SC yako ( tena Waandamizi kabisa ) wamenithibitishia huu Mpango Mkakati wenu wa 'Kimafia' dhidi ya Simba SC halafu leo hii ulivyo Mnafiki na Roho ya Kichawi unakimbilia Kujihami na Kujishtukia kuwa Simba SC inataka Kuwahujumu. Huoni hata Aibu tu Hassan Bumbuli?
Najua kwanini sasa Yanga SC mnajihami na Kujishtukia hivi mlikuwa mnatutambia hao Waganga wenu Wanne ila Simba SC imemshusha 'Mwanamume' Mmoja ambaye hazichezi tu Mechi za Simba SC bali hata zenu ameshaanza Kuzicheza na hiyo Disemba 11 amewaandalia 'Kitu' cha maana ambacho KEROZENE naamini kuwa Kitawasambaratisheni na Mtavurugana kuliko Maelezo.
Na kukuonyesha kuwa safari hii wana Simba SC wote kuelekea Mechi yetu nanyi Mimi KEROZENE ambaye nilijiweka Kando kwa Shughuli zangu tukuka za 'Umafia' wa Soka la Bongo kwa Hasira Kali nilizonazo juu yenu nimeamua kurudi na kwa Kujiamini kabisa hapa hapa JamiiForums nakuambia Wewe Hassan Bumbuli kuwa anzeni Kuzipunguza Goli 3 ambazo zipo tayari na hata kama mkijitahidi Kuzifuta ( Kuzipunguza ) zitakuwa 2 - 1 ila iwe isiwe Yanga SC tarehe 11 Disemba 2021 anaenda Kufa ( Kufungwa ) na Simba SC kwa Mkapa.
.
🗣"Tutakuwa makini zaidi kwenye mechi yetu dhidi ya Mbeya Kwanza, tunajua mipango iliyopo, tutafanya hivi kujiweka katika nafasi salama kwa sababu tunahofia kupata kadi za njano na kupelekea baadhi ya nyota kuukosa mchezo dhidi ya Simba hapo Desemba 11, hili tumeshalifanyia kazi,"
.
"Tumebaini janja janja za wapinzani wetu kuwatafutia kadi za njano wachezaji wetu nyota, au kufanyiwa rafu za makusudi akiwamo, Khalid Aucho na wengine ili kushindwa kucheza mechi ijayo dhidi ya Simba,”
.
"Tumegundua na tunatarajia mechi yetu dhidi ya Mbeya Kwanza itakuwa na mabadiliko katika kikosi, baadhi ya nyota watapumzishwa kwa ajili ya kujiandaa na pambano letu dhidi ya Simba, tunawahakikishia mashabiki wetu tutarejea na pointi tatu kutoka kwa Mbeya Kwanza halafu Desemba 11, tabu iko pale pale dhidi ya Simba," amesema Hassan Bumbuli.
Taarifa: sportsarena_tz
Bumbuli nakuheshimu sana na kukubali mno kwa Kazi yako ya Uandishi wa Habari tokea ukiwa Mwananchi ila sijui zile Akili zako Kubwa ulizokuwa nazo ulipofika hapo Yanga SC ulipo zimetokomelea wapi.
Bumbuli leo kabisa Wewe ni wa kusema kuwa Simba SC inataka Kuwaumiza vibaya Wachezaji wenu Yanga SC na Kuwatafutia Kadi ili wakose Mechi yenu na wao Simba SC?
Bumbuli nani asiyejua kuwa Yanga SC mlikakaa Kikao ( tena ukiwemo ) pia pamoja na Mbunge Mmoja wa Dodoma na Waziri Mmoja wa Wizara Muhimu Tanzania huku mkipata Maagizo ya kutoka kwa Mstaafu namba 4 na Namba 2 wa sasa katika Serikali ya Rais Samia kuwa ili 'Kuwakomoa' Simba SC katika Msimu huu dawa ni Kuwaumizia tu Wachezaji wao maarufu na muhimu ili wawe na Majeruhi wengi?
Bumbuli binafsi kama KEROZENE nikuambie tu kuwa 90% ya Wachezaji wa Simba SC na Yanga SC ni Marafiki zangu na wapo Wachezaji Wawili wa Yanga SC yako ( tena Waandamizi kabisa ) wamenithibitishia huu Mpango Mkakati wenu wa 'Kimafia' dhidi ya Simba SC halafu leo hii ulivyo Mnafiki na Roho ya Kichawi unakimbilia Kujihami na Kujishtukia kuwa Simba SC inataka Kuwahujumu. Huoni hata Aibu tu Hassan Bumbuli?
Najua kwanini sasa Yanga SC mnajihami na Kujishtukia hivi mlikuwa mnatutambia hao Waganga wenu Wanne ila Simba SC imemshusha 'Mwanamume' Mmoja ambaye hazichezi tu Mechi za Simba SC bali hata zenu ameshaanza Kuzicheza na hiyo Disemba 11 amewaandalia 'Kitu' cha maana ambacho KEROZENE naamini kuwa Kitawasambaratisheni na Mtavurugana kuliko Maelezo.
Na kukuonyesha kuwa safari hii wana Simba SC wote kuelekea Mechi yetu nanyi Mimi KEROZENE ambaye nilijiweka Kando kwa Shughuli zangu tukuka za 'Umafia' wa Soka la Bongo kwa Hasira Kali nilizonazo juu yenu nimeamua kurudi na kwa Kujiamini kabisa hapa hapa JamiiForums nakuambia Wewe Hassan Bumbuli kuwa anzeni Kuzipunguza Goli 3 ambazo zipo tayari na hata kama mkijitahidi Kuzifuta ( Kuzipunguza ) zitakuwa 2 - 1 ila iwe isiwe Yanga SC tarehe 11 Disemba 2021 anaenda Kufa ( Kufungwa ) na Simba SC kwa Mkapa.